Engineer Godfrey Kasekenya Nimependa unavyoifahamu jiografia ya nchi yetu

Engineer Godfrey Kasekenya Nimependa unavyoifahamu jiografia ya nchi yetu

saigilomagema

JF-Expert Member
Joined
Jun 5, 2015
Posts
4,683
Reaction score
7,222
Mhandisi Godfrey Kasekenya naibu waziri wetu wa uchukuzi na ujenzi sekta ya ujenzi. Jana ulikuwa unasain mkataba wa ujenzi wa barabara ya Karatu-Mbulu-Haydom-Nduguti-Gumanga-Ibaga-Sibiti-Meatu-Lalago-Maswa. Siku zote huwa nafurahi ukijibu maswali bungeni hasa ukitaja meneo yanakopita barabara za nchi hii. Kuna mtu mpaka asome kwenye kijikaratasi mi naonaga ni aibu

Hasa vijana wa siku hizi ni wazembe sana hakuna mfano, kijana akiingia tu kwenye basi ni simu na earphone ni usingizi. Anaweza kupita hiyo barabara hata mara kumi kesho mwulize km anajua chochote kuhusu hiyo njia. Vijana wa siku hizi n i hovyo kabisa, ni wazembe waliopitiliza.

Ila mlichokosea km serikali barabara ingeanzia Karatu siyo Mbulu maana Karatu ndiko ilikoishia lami ya kutoka Arusha na ndiko barabara inakoanzia, Engineer km wewe umesoma mahesabu unashindwaje kujua simple logic km hii. Kingine kipande cha kutoka Garbabi-Labay mbona mmeiruka? Ujenzi huu wa vipande vya kurukaruka kumfurahisha mbunge fulani haufai. Halafu Km 25 ni ndogo sana kwa Taifa kubwa km la kwetu. Sasa ni vipande vipande vidogo vya lami vinasaidia nini? Kwanini mnaona wananchi mazuzu kiasi hicho?
 
Back
Top Bottom