English to become medium from STD III from 2013


Hi ndio nimesema kuna watu watasifu haya maamuzi ya kisiasa lakini serikaliinakwepa kma si gharama basi majukumua yake ya kusomesha watoto wa wakulima sababu wanajua watoto wao wanapata elimu bora.

Serikali inatakiwa kuadress tatizo halisi . Na wataalam wapo kama hiyo asasi je ndivyo walivyopendekeza hivyo kuwa tatizo lhata kama ni english peke litaisha kwa style hiyo.???!!!!
 
Yaani ina sikitisha sana yaani kingereza ndiyo elimu, haya ndiyo
matatizo ya kumaliza madarasa bila ya kuelimika.

Sifa moja tuliyonayo Tanzania ni kuwa na lugha yetu ya asili.
Hakuna nchi yeyote Afrika ambayo iliweka kipaumbele katika
matumizi ya lugha ya Taifa. Hiki ni kitu ambacho najivunia
popote niendapo (kwamba lugha yangu mama ni kiswahili).

Tuache kujidanganya hapa, suala la kutumia kiswahili mpaka
darasa la saba ni kujenga utaifa. Hata kama mtoto atakuja
kujifunza kiingereza baadae teyari anakuwa na uwezo wa
kufikiri kama Mtanzania.

Kuna tatizo kubwa la kisaikolojia katika utumiaji wa lugha za
wenzetu katika elimu ya mwanzo, hiyo ni sawa na kuikana
asili yako.

Ikumbukwe ya kwamba lugha ni sehemu ya utamaduni, kwahiyo
unapoondua lugha yako katika elimu ya awali unaondoa
utamaduni wa yule mtoto. Hii inaleta madhara kwa kuwa mtoto
anaanza kufikiri utamaduni wa wengine ni bora, kwahiyo yeye
anajiona kama anamapungufu.

Kuhusu suala la kutumia kingereza kuanzia darasa la tatu huu
ni uvivu wa kufikiri kwa baadhi ya wahusika. Hawa watu hawataki
kuchapisha vitabu na kubuni njia mpya za ufundishaji na
kutafuta njia mbadala (kiingereza). Hii ni sawa na kumtafuta
mchawi wakati tatizo ni uongozi mbovu
. Kingereza kimefika
hapo kilipo kwasabau wenye lugha walikuna vichwa na kufika
hapo walipo.

Hivyo basi hatuhitaji hicho kiingereza kwasababu kiingereza
ni utamaduni tuu. Sasa wanataka watoto waanze kujifunza
maneno kama sleet, frost, snow na ice vitu ambavyo havipo
kwenye mazingira yetu. Kwanini wasijifunze tumbili, ngedere,
nyani na sokwemtu wanyama ambao wakienda shambani
kwa bibi wapo?

Sasa kwa kuwafundisha sleet na frost si ndiyo tunaanza
kuwafundisha kukariri wakati bado wadogo? Wenzatu wakitaja
hayo maneno sleet na frost wanaelewa bila hata maelezo
zaidi kama vile sisi tunavyo elewa tukisema ngedere na nyani.
 

Nakuunga mkono mkuu!
 
implementation ya hiyo kitu ngumu... ukienda upcountry hata hapa dar walimu wengi bado ni wale wa UPE

Siyo UPE tu ndugu kwa taarifa yako walimu wengi background ya kiingereza siyo nzuri!
Mie namshauri kwanza waziri ahakikishe kwanza walimu wanamudu hiyo lugha na ndipo mkakati uanze, kwa ujumla hili liko kisiasa zaidi ila kwa kiutendaji ni ngumu mno hasa kwa public schools.
 
Wazo ni sana, sema itabidi walimu wote wa shule za msingi wapigwe english kozi kwanza manake wengi wao kiingereza kinawapa shida saana. Haitakuwa na maana kwa watoto wetu kufundishwa na maimunas...

Naunga mkono hoja.
 
Ujinga mtupu, swala sio kufundisha kiingereza kuanzia Primary. Hii issue ya EAF itawamaliza watanzania. EAF haina interest na Watanzania ni agenda ya mafisadi .... ...... .....
 
Matatizo ya msingi ya kiingereza hayatakwisha hadi pale tatizo la msingi ktk sekta ya elimu litakapokwisha. Nalo ni elimu kusimamiwa na watu FAILURES in education. Kwamba tumelazimishwa kuamini kuwa ualimu ni kwa walioshindwa mitihani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…