Entrepreneurship spirt katika jamii mara nyingi hutegemeana na haya mambo

Entrepreneurship spirt katika jamii mara nyingi hutegemeana na haya mambo

CHASHA FARMING

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2011
Posts
7,872
Reaction score
9,263
ENTREPRENEURSHIP SPIRT KATIKA JAMII MARA NYINGI HUTEGEMEANA NA HAYA MAMBO


UTAMADUNI WA JAMII HUSIKA

1.
Watu ambao traditinaly ni wafanya baishara mara nyingi husasaidia sana kuhamasiha ujasirimali
- Chukulia mfano wa Wachaga na Wahindi, Wachanga wengi traditionally ni wafanya baishara na utaona kwamba hata kizazi chao kingi hukimbilia kwenye Ujasirimali,
- Wahindi nao Mara nyingi ni watu wa Ujasirimali, na that is why hata watoto wao wanavyo kuwa vyuoni huwezi wakuta sijui wanasoma Education, Sijui Socilology, Mara sijui Community Development, Mostly utawakuta wakisoma, Acounting, Business, Marketing na IT, na Uhandisi.


2. Watu wengi hujikuta wanaingia katika Kundi La Ujasirimali kutokana na Utamaduni wa Jamii yao Kuhimiza kujitegemea, kuna Makabira swala la kujitegemea huanza kwa motto so mara nyingi motto anavyo kuwa anakuwa na mentality ya Kujitegemea kwa kila kitu


3. UTAMADUNI WA KUNUNUA(CONSUMERISM CULTURE)
Huu ni utamaduni wa watu kupenda kununua sana vitu, na hivyo ku encourage jamii hiyo kuwa wajasirimali, Na kuna baadhi ya Jamii manunuzi kwao ni kama anasa Fulani na mara nyingi watu huwa ni wagumu sana
SO RETURN FROM BUSINESS INAPO KUWA KUBWA KULIKO RETURN FROM JOBS AUTOMATICALY JAMII YA PALE WENGI WATAKUWA WAJASIRIMALI


4. JAMII YA WAPENDA KUAJILIWA
Mara nyingi jamii ya wapenda kujiliwa huhamasisha hata watoto wao watafute kazi, hivyo kuua ndoto za watoto wao hata kama walikuwa na mpango wa kuja kuwa wajasirimali
Mara nyingi wazazi huhamasisha watoto kusoma na kuja kuwa wafanyakazi wazuri, na huwambia Biashara ni za watu walio feli shule


5. UTAMADUNI WA KUBANA MATUMIZI
Utamaduni wa Kubana matumizi nao hufanya watu wengi kuona Ujasirimali kama si ishu, na mara nying return ya Jobb huwa kubwa kuliko return from Business


6. UTAMADUNI WA KUTO PENDA KUFANYA KAZI
Kuna watu kwao kazi ni kama Gereza na mara nyingi utawakuta ni watu wa kukaa vibarazani au kupiga story tu, Jamii kama hii ni Nadra sana kupata watu wenye spirit ya Ujasirimali, kwa sababu jamaa ile watu sio hard workers.


JINSI SIASA INAVYO WEZA KUJENGA AU KUBOMOA ENTREPRENERSHIP SPIRT

1. Nchi isiyo kuwa na mtengemano wa kisiasa mara nyingi huwa vunja moyo watu wenye muelekeo wa kujiajiri au kuwa wajasirimali, mara nyingi watu huhofia mali zao pindi machafuko yakianza, na mara nyingi wakati wa Machafuko wano athirika zaidi ni wafanya biashara ambao mari zao huporwa

2. Jinsi Serikali inavyo weka mazingira kama Mawasiloana
Vitu kama Barabara nzuri ana miundombinu mingine huhamasisha ujasirimali

3. KODI KUBWA/KODI NDOGO
Mara nyingi Kodi zinapo kuwa nyingi huvunja watu moyo wa kuja kuwa wajasirimali kwa sababu huona ni risk kuwa Mjasirimali na mara nyingi pesa zitaishia kulipa Kodi za Nchi


JINSI UCHUMI WA NCHI UNAVYO WEZA KUHAMASISHA UJASIRIMALI AU KUTO KUHAMASISHA

1. Purchesing Power ya Jamii husika, mara nyingi hali ya kununu inapo kuwa juu hata Ujasirimali nao utakuwa juu, ni vigumu sana watu kwenda kuwekeza katika jamii au nchi ambayo purchasing power iko low sana, Nchi ambyo wanachi wake hawana utamaduni wa kununu sana kutoakna na hali ya kiuchumi ya Nchi husika hu ua Ujasiriamali


2. MIFUMUKO YA BEI
Hii inapo kuwa juu, huua kabisa Ujasirimali kwa sa babu watu hawanunui tena bidhaa kwa kuhofia bei na wafanya biashara hufikia kufunga biashara zao, so kwa staili hii ujasirimali unakuwa ni ndoto


3. Sunsatance Economy
Katika Nchi ambayo ni Substance Economy ni vigumu sana kukuta Namba kubwa ya Ujasirimali, katika uchumi wa aina hii mara nyingi watu hutumia kile wanacho zarisha wenyewe.
Mfano: wakulima wa Mahindi- wengi wanalima kwa ajili ya kula
Ufugaji wa Kuku: Watu hufaga kuku wao wenyewe kwa ajili ya Kuchinja
Katika huu uchumi entreprenership opportunity huwa ni chache sana
NA HII NDO TATIZO KUBWA SANA KWA NCHI NYINGI ZA AFRICA IKWEMO TANZANIA
 
hapo kwenye jamii ya wanao penda kuwa wafanyakazi ndo ugonjwa mkubwa wa taifa hili.
 
Mkuu Chasha, ​hii nondo ilivyoshiba utaamini imechangiwa na watu watatu tu. Ila ingekua ule ujasiriamali wa Nyuki na Asali ya kitanzania ungekuta tuna michango sio chini ya 400. Hapa huhitaji kujua kama tunaenda mbele nyuma. Jibu liko wazi.
 
Mkuu Chasha, ​hii nondo ilivyoshiba utaamini imechangiwa na watu watatu tu. Ila ingekua ule ujasiriamali wa Nyuki na Asali ya kitanzania ungekuta tuna michango sio chini ya 400. Hapa huhitaji kujua kama tunaenda mbele nyuma. Jibu liko wazi.

Mkuu hawawezi changia kwa sababu sijapost thread ya kuuza Komputa au Simu, au kuuliza nitafungua vipi Baa ya kuuza Pombe,

Mkuu umenikumbusha Juzi kati nilikuwa na Ongea na wakenya Fulani, kwa kweli wanashangaa sana sisi Watanzania, na wanadai tumelala vibaya mno na kubakia kulaumu Kenya kwamba inafaidi, sana, Na katika maongezi nikagundua ni kwa nini kumbe Kenya ni Moja ya Top Five wanao ongoza kwa kuwekeza Tanzania,

Kwa kifupi tunayo kazi kubwa kabisa, na si ya kitoto kabisa, ni kazi kubwa mno, wenzetu wako mbali sana na si kwa sababu wanasaidiwa na serikai yao no hata kwao ishu za Mikopo hazina tofauti sana na Bongo,

So mkuu wala usimumize kichwa,hii Ndo Tanzania bana
 
Chasha aminia mkuu.. Uko juu

Uendelee kubarikiwa kwa kushare nasi.

Kwa kusoma nondo za namna hii ndipo watu tunaendelea kuwaka hasira za kutaka kujiajiri.

Bravo Mkuu

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Mchango mzuri sana mkuu, Ubarikiwe. Hii ni darasa ambayo watu walipaswa walipe kwanza cho chote getini ndo waipate. Sasa wanapata bure JF. Tunawashukuru sana hata hawa JF founders.
 
Mchango mzuri sana mkuu, Ubarikiwe. Hii ni darasa ambayo watu walipaswa walipe kwanza cho chote getini ndo waipate. Sasa wanapata bure JF. Tunawashukuru sana hata hawa JF founders.

Mkuu ni kweli kabisa, Hii elimu kwingine inalipiwa.Ila kama unavyo jua Huku kwetu bado tuko kwenye Transition ya kutoka Socilism to Capitalism, so inabidi itolewe bure kabisa
 
Kwa wanafunzi walifeli ndo ilikuwa mahali pake hapa, tatizo watalaimishwa kurudia mitihani
 
Back
Top Bottom