Hii ni post ya ya mhe Nape ya 23 May 2024 akimrushia tusi mwananchi.
Waziri Nape anamdhalilisha sana mhe rais kwa tabia yake ya kutukana watu mitandaoni. Yeye kama waziri wa Habari na Mawasiliano alipaswa kuwa mfano mwema wa matumizi mazuri na salama ya mitandao. Lkn Nape mara nyingi amekuwa akijbizana na wananchi kwa matusi.
Mhe rais anadhalilika kwa vile Nape anatoa picha mbaya kwa jamii kuwa rais anateua watu wa hovyo, wenye tabia mbaya ya kutukana hovyo. Na hiii linanisukuma kuamini kuwa Nape ni miongoni mwa mawaziri waliokemewa na Makonda kuwa waache kumtukana mhe rais.
Kwa hulka yake hii Nape atatoa wapi uhalali wa kukemea vijana wadogo wanaoandika matusi mitandaoni? Hawa vijana huwa mara nyingi wanakamatwa na kushughulikiwa na dola lkn kwann mhe Nape hakamtwi??