Enyi wanaaume!! ndoa na ngumi wapi na wapi??

Kiteitei

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2009
Posts
1,595
Reaction score
1,540
aaaaaghrr!! niko na ka hangover ka jana, nimejipumzisha nikiwaza na kuwazua jinsi ya kureplace pesa niliyotumia jana bila mpangilio maalumu, mlangoni ngo ngo ngo, nauliza nani, naitwa jina......., ni mimi mama ....., natoka nje namkuta mke wa jirani yangu, uso umemvimba kichwani kavaaa kofia kuubwa,namuuliza kulikoni, nikahisi kapigwa nondo (niko mkoa ule almaarufu kwa nondo), naye akaniulza kwani jana hukuyasikia? nikajibu hapana... basii mdada wa watu kaanza kumwaga ya moyoni jinsi alivyopewa kichapo na mumewe wanayeishi naye miaka miwili sasa wakiwa na mtoto mmoja! mdada wa watu ameshaichukulia hali hii kama ni kawaida na ndio maisha yake ya kila siku!nimejaribu kumuhoji sababu eti kosa ni kuwa alikuwa anafua usiku! kama siku mbili hivi maji yalikuwa yamekatika!,namuuliza vipi hali hii umeshawahi kujadiliana au kulifikisha hata kwa wakubwa zenu! kajibu..yaani kwao wote wako hivyo, katikati ya maongezi anakuja mke mwenzie(mke wa shemeji yake) naye kavimba kama katiwa hamira..yeye anadai kapewa kibano juzi!!nawauliza washawahi kulifikisha mbele ya sheria, wote wanadai hapana na wanaogopa, wote wana mambo yanayofanana, jirani yangu alipewa mimba mwaka juzi akiwa form four na hakumaliza shule ikabidi aolewe, mzazi wake mmoja alishafariki na aliyebaki hana uwezo, mwenzie naye hakumaliza o level,wazazi wake wote wamefariki na hana ndugu mwenye uwezo,wote hawana kazi;hivyo waanajiona kama hawana msaada ila kilichobaki ni kuvumilia tu kipigo, nina incident nyingine inaendana na hii nikiwa dar last week.. why why sie wanaume tunawageuza ma punching bags hawa viumbe! kila mtu ana makosa but sidhani kama kipigo ndio suluhisho,niwashaurije hawa, ahh ngoja kwanza nitoke nikatafute supu washaniharibia siku hawa.
 
Hiyo ni aina mojawapo ya kuonyesha real love kwa baadhi ya makabila.
 
Mapenzi ya mbwa hayo...mpaka wang'atane ndo wapeane vitu!
Waacheni wa-enjoy mapenzi yao.
 
Mmh! jamani mapenzi gani hayo yakupigana ndio akujue kua wewe mwanamme au sababu unamletea ugali? wanaume namna hii ukiwakuta nje na vimada wanapigwa makofi na hawasema kwamkewe ndio anajitia mwanamme,hawajua kama mwanamke hapigwi kwa fimbo wala ngumi,anapigwa kwa ulimi...
 
Kumbe utamaduni wa kuwatandika wanawake bado upo! Kweli Beijing haijafanya kazi kabisa!
Wanaume wengine wasipopiga jogoo hawiki. atamtandika mwanamke weeeeee mpaka asikie mwanamke analia ndiyo anapata hamu ya kufanya mapenzi! Mkoa wa baba wa taifa unaongoza kwa hii practice!
 
ki ukweli m.me anaepiga ni mbaya mno.inasikitisha,na kama hao,hawana mtaji wowote ule,inabidi waishi nao hivyo hivyo.bora na wao,wanachukue lessons za siri siri,akikupiga kibao,na wewe unarusha ngumi ya nguvu.lakini hayo hayatokuwa maisha mazuri
 
Wanaopigwa wasipopigwa wanaongea haooo!! Ooohoooo, nendeni mitaa ya bugarika mwanza utasikia kila siku usiku mtu anaangua kilio, ikifika asubuhi watu wanacheka na ngeo. Si tulishazoea hizo kesi. Dirishani kwangu ni mwenyekiti wa mtaa wangu, kila saa 9 hadi 10 usiku utasikia kesi zikisikilizwa namimi najaribu kuchungulia kunani, huwa nawaona tu! nikikutana nao mitaani nacheka na kuwapa pole.
Ndo life style na tamaduni za kiafrica!! Sema mzungu anataka tumuige kila kitu! which is impossible.
 
Binafsi nalaani mapigo baina ya wanandoa, siyo wanaume tu kuwapiga wake zao, hata wanawake kuwapiga waume zao. Muda si mrefu uliopita kule Ruvuma wanaume wengi sana wamepoteza maisha kupitia mikono ya wake zao. Wanandoa wanaokusanya michango yetu mingi wakati wa maandalizi ya harusi zao hatutarajii wapigane kwa sababu yoyote ile. Fimbo ni maalum kwa watoto, watu ambao akili yao haijakomaa kuweza kuelekezwa na kufuata lililo jema, sasa mwanamke au mwanaume mtu mzima anapopigwa maana yake ni kwamba abadilike au hawezi kuelekezwa au ni kumaliza hasira za mpigaji?

Wanandoa kama wana hasira wapelekane kitandani wakamalizane pale kwenye 6''X6'' hiyo ndiyo halali yao. Mambo ya kupigana ni ya kishamba mno na ni dalili ya kuishiwa hoja na hatimaye kauamua kutumia nguvu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…