Enzi zako weekend kama hii ulikuwa unawaza kwenda kiwanja gani?

Enzi zako weekend kama hii ulikuwa unawaza kwenda kiwanja gani?

Zero IQ

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2016
Posts
13,959
Reaction score
24,935
Weekend ndio hiyo inaanza, kila mtu alikuwa na enzi zake,
Kuna ambao enzi zao zimepita kwa sababu ya umri na wengine ni kwa sababu ya majukumu,

Kuwa mzee hakukufanyi usikumbuke Enzi zako,
Kuna wazee, watu wazima tunakutana nao viwanja mpaka leo, wengine wakikumbushia Enzi zao na wengine wakiendeleza enzi,

Je Enzi zako weekend kama hii ulikuwa unawaza kwenda kiwanja gani Kabla ya kubanwa na majukumu au umri kukutupa mkono?

Tukumbuke Enzi.

Cc Zero IQ
 
Bahati mbaya sijawahi kuwa mpenzi wa viwanja
Weekend(ambayo kwangu mara nyingi ilikuwa ni jumapili tu) nilikuwa naitumia kula na kulala siku nzima
 
Kwanza nilikuwa naanza kunywa bia baa ya kitaa kuanzia saa sita mchana.

Saa kumi nahamia bar moja hivi kuangalia mpira

Saa mbili usiku najongea live band mpaka saa sita au saba usiku.

Saa saba tunasogea La Chalz kumalizia bia.

Saa kumi nageuka ghetto mwenyewe kulala.

Kesho yake tunafanya shughuli za kimaendeleo.

" we were once young and stupid," Hashim Sipunda Rungwe.
 
Back
Top Bottom