Epuka jinsi uwezavyo kuweka tatoo mwilini mwako

Epuka jinsi uwezavyo kuweka tatoo mwilini mwako

fazili

JF-Expert Member
Joined
Jun 10, 2011
Posts
16,427
Reaction score
22,418
Kadiri uwezavyo nakushauri kijana epuka sana kuchora tatoo katika mwili wako. Kuna mambo mengi yamejificha nyuma ya uchoraji wa tatoo katika mwili wa binadamu. Tatoo hata kama unachora tatoo ya msalaba au kitu unachofikiri ni kitakatifu, ulichofanya ni kitu kibaya na hakitakuacha salama. Tatoo zote ni alama au lugha inayowakilisha jambo fulani katika ulimwengu wa giza. Tatoo ni signature za shetani mwilini mwako. Epuka kuchora tatoo kwa gharama yoyote ile!
1738763296404.png
 
Kadiri uwezavyo nakushauri kijana epuka sana kuchora tatoo katika mwili wako. Kuna mambo mengi yamejificha nyuma ya uchoraji wa tatoo katika mwili wa binadamu.
Tatoo hata kama unachora tatoo ya msalaba au kitu unachofikiri ni kitakatifu, ulichofanya ni kitu kibaya na hakitakuacha salama. Tatoo zote ni alama au lugha inayowakilisha jambo fulani katika ulimwengu wa giza. Epuka kuchora tatoo kwa gharama yoyote ile! View attachment 3226165
Mambo gani mkuu tuelekeze tusijekuangamia
 
Kadiri uwezavyo nakushauri kijana epuka sana kuchora tatoo katika mwili wako. Kuna mambo mengi yamejificha nyuma ya uchoraji wa tatoo katika mwili wa binadamu. Tatoo hata kama unachora tatoo ya msalaba au kitu unachofikiri ni kitakatifu, ulichofanya ni kitu kibaya na hakitakuacha salama. Tatoo zote ni alama au lugha inayowakilisha jambo fulani katika ulimwengu wa giza. Tatoo ni signature za shetani mwilini mwako. Epuka kuchora tatoo kwa gharama yoyote ile! View attachment 3226165
Pichani hapo ni wahuni wa El Salvador.... Naangaliaga halafu nafananisha na panya road huku....😂🤣🤣🤣🤣😂😂 Huenda wanaendana lakini🤷🏿‍♂️🤷🏿‍♂️🤷🏿‍♂️🤷🏿‍♂️

 
Nilishangaa kuona ana tattoo pajaji ya kipepeo🙏🙏🙏! Na nyuma ya juu ya makalio pameandikwa eat all 😂😂

Sikuelewa icho kiinglish
 
Huu ni mtazamo potofu.
Jamii mbalimbali zimejichora alama mwilini kwa maelfu ya miaka.
Wengine hutumia hina, wengine matope, wengine utomvu wa miti, wengine kama wamakonde na oromo wanajichanja chale kwa mpangilio fulani.

Huo ushetani ni kipengele unachokileta wewe tajirii..
 
Sasa Yesu mwenyewe alikuwa na tatoo kwenye kitabu cha Ufunuo 19.
Na mnadai Issa Bin Mariam ndiyo Yesu.

Au huyo Yesu / Issa ndiye ibilisi mwenyewe.
 
Maishani hujui la mbele.
Unaweza kujikuta umepata nafasi kwenye moja ya majeshi yetu tattoo ikakutema.
Jamaa mmoja ana tattoo kazini sasa kazini almost tuna t-shirt ya kila siku from Monday to Friday rangi tofauti na suti . Sasa jamaa kuficha tattoo inambidi Kila siku avae suti au akivaa t-shirt lazime avae na koti juu .
Ni mateso sana. Anaficha ila Dunia haina siri siku moja jamaa mmoja aliziona
 
Watazania tunapenda maisha ya kupeana vitisho kwa mambo ya kufikirika tu
 
Back
Top Bottom