afyakliniki
Senior Member
- Nov 21, 2018
- 125
- 81
EPUKA MATUMIZI HOLELA YA DAWA/MADAWA.
Unaamka asubuhi kichwa kinauma kwa kuwa una haraka ya kuwahi kazini unaamua kunywa dawa za kutuliza maumivu na kuwahi kazini, Mchana wakati unapata chakula unahisi maumivu kama ya asubuhi unamwambia mfanyakazi mwenzio yeye anakujibu kuwa "Ni Malaria hiyo", jioni ukiwa nyumbani unahisitena hali ile ile unamuambia mke/mume wako anakujibu "Si Umeze Dawa za Malaria" nawe bila kipingamizi unameza hizo dawa mpaka zinaisha lakini bado unahisi maumivu ya kichwa yapo.. Wengi wetu tumekua na tabia ya KUMEZA Dawa bila Ushauri wa wataalam wa Afya, Bila Vipimo ili kujua Tatizo/Ugonjwa na wengine Humeza Dawa bila mpangilio.. Hiyo yote tunaita "MATUMIZI HOLELA YA MADAWA"
Mara nyingi dawa zinazomezwa kiholela hutuliza tu dalili za ugonjwa ila sio kuuondoa kabisa, Mfano unapohisi maumivu ya kifua na ukaamua kumeza dawa za kutuliza maumivu itakusaidia kuondoa maumivu (tena kwa kipindi kifupi) lakini tatizo hasa liliopelekea maumivu yale unakua hujalikabili.
Matumizi ya madawa kiholela yana madhara mengi sana kuanzia madhara madogo ndani ya mwili na hata kupelekea kifo, matumizi holela pia hujenga USUGU wa vijidudu vya magonjwa dhidi ya dawa husika.
Hivyo basi wataalam wa tiba na madawa kutoka afyakliniki Wanakushauri wewe Mwanafamilia kutotumia Dawa pasi na Ushauri Wa kitaalam au vipimo toka katika kituo kinacho husika.
Asante na Karibu.
Unaamka asubuhi kichwa kinauma kwa kuwa una haraka ya kuwahi kazini unaamua kunywa dawa za kutuliza maumivu na kuwahi kazini, Mchana wakati unapata chakula unahisi maumivu kama ya asubuhi unamwambia mfanyakazi mwenzio yeye anakujibu kuwa "Ni Malaria hiyo", jioni ukiwa nyumbani unahisitena hali ile ile unamuambia mke/mume wako anakujibu "Si Umeze Dawa za Malaria" nawe bila kipingamizi unameza hizo dawa mpaka zinaisha lakini bado unahisi maumivu ya kichwa yapo.. Wengi wetu tumekua na tabia ya KUMEZA Dawa bila Ushauri wa wataalam wa Afya, Bila Vipimo ili kujua Tatizo/Ugonjwa na wengine Humeza Dawa bila mpangilio.. Hiyo yote tunaita "MATUMIZI HOLELA YA MADAWA"
Mara nyingi dawa zinazomezwa kiholela hutuliza tu dalili za ugonjwa ila sio kuuondoa kabisa, Mfano unapohisi maumivu ya kifua na ukaamua kumeza dawa za kutuliza maumivu itakusaidia kuondoa maumivu (tena kwa kipindi kifupi) lakini tatizo hasa liliopelekea maumivu yale unakua hujalikabili.
Matumizi ya madawa kiholela yana madhara mengi sana kuanzia madhara madogo ndani ya mwili na hata kupelekea kifo, matumizi holela pia hujenga USUGU wa vijidudu vya magonjwa dhidi ya dawa husika.
Hivyo basi wataalam wa tiba na madawa kutoka afyakliniki Wanakushauri wewe Mwanafamilia kutotumia Dawa pasi na Ushauri Wa kitaalam au vipimo toka katika kituo kinacho husika.
Asante na Karibu.