Erik Ten Hag atimuliwa Manchester United baada ya kipigo dhidi ya West Ham United

Erik Ten Hag atimuliwa Manchester United baada ya kipigo dhidi ya West Ham United

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Manchester United imemfuta kazi kocha Erik ten Hag kufuatia mwanzo mbaya wa msimu wa 2024/25. Klabu hiyo, maarufu kama The Red Devils, ipo nafasi ya 14 katika msimamo wa Ligi Kuu ya England baada ya kupoteza mechi nne kati ya tisa za kwanza.
1730117011832.png
Kipigo cha jana cha bao 2-1 dhidi ya West Ham United, baada ya penalti ya dakika za jioni iliyofungwa na Jarrod Bowen, ambayo ilizua utata, kimechangia kufurushwa. Uongozi wa Manchester United umechukua hatua hiyo kutokana na matokeo haya duni, wakitafuta njia mpya ya kuinua timu msimu huu.

Mkataba wake ulitarajiwa kumalizika Julai 2026, na sasa Ruud van Nistelrooy amepewa nafasi ya muda. Ten Hag alijiunga na timu mwaka 2022 na ameshinda mataji mawili: Carabao Cup 2023 na FA Cup 2024.

Pia, Soma:
+
Mkurugenzi Mtendaji wa Man United: Ten Hag ndiye kocha sahihi kwetu na tunamuunga mkono kikamilifu kwa 100%
+ ERIK TEN HAG kama ataondoka Man United basi itakuwa wameamua kumuondoa tu!
 
Kocha Erik ten Hag amefukuzwa kazi ndani ya Manchester United baada ya matokeo mabaya mfululizo yanayofanya timu hiyo kushika nafasi ya 14 katika Premier League mpaka sasa ikiwa imecheza michezo Tisa.

Mkataba wake ulikuwa unatarajiwa kumalizika Julai 2026 ambapo Nguli wa klabu hiyo, Ruud van Nistelrooy amekabidhiwa mikoba kwa muda.

Ten Hag alianza kuinoa timu hiyo Mwaka 2022, amefanikiwa kubeba mataji mawili ambayo ni Carabao Cup 2023 na FA Cup 2024.

====================

Erik ten Hag has been sacked by Manchester United after a miserable start to the season, with the Red Devils languishing in 14th place in the Premier League.

The Dutchman, who had his contract extended through to 2026 in July, is likely to pocket a significant compensation package after being axed by Sir Jim Ratcliffe and Ineos just three months into the new campaign.

Club legend Ruud van Nistelrooy will take over at Old Trafford on an interim basis, while Brentford's Thomas Frank, Sporting Lisbon's Ruben Amorim, Borussia Dortmund's Edin Terzic and ex-Barcelona boss Xavi have been linked with the role permanently.

Thomas Tuchel, who United considered in the summer, has since been named Gareth Southgate's successor by the Football Association and will take charge of England from January.

Manchester United confirmed the news in a statement on Monday, which read: 'Erik ten Hag has left his role as Manchester United men’s first-team manager.

'Erik was appointed in April 2022 and led the club to two domestic trophies, winning the Carabao Cup in 2023 and the FA Cup in 2024.

'We are grateful to Erik for everything he has done during his time with us and wish him well for the future.

'Ruud van Nistelrooy will take charge of the team as interim head coach, supported by the current coaching team, whilst a permanent head coach is recruited.'

Sunday's 2-1 defeat against West Ham proved the final straw for Manchester United's chiefs, with the club now three wins, two draws and four losses from their opening nine games of the season.

Casemiro thought he had at least rescued a point at the London Stadium when he equalised in the 81st minute to cancel out Crysencio Summerville's strike, but Jarrod Bowen's controversial stoppage-time penalty consigned Ten Hag to yet another disappointing defeat.

Significant pressure had mounted on Ten Hag ahead of the second international break of the season in October, prompting Manchester United to hold an executive meeting in London, led by Ratcliffe.

The senior leadership team opted to stick by the Dutchman, while also choosing to 'sack' legendary manager Sir Alex Ferguson from his £2.61million ambassadorial role at the club.

Source: DailyMail
 
Klabu ya Manchester United imemfuta kazi aliyekuwa kocha mkuu wa kikosi hicho Erik Ten Hag, kwa sasa kikosi hicho kitaongozwa na Ruud Van Nistelrooy kama kocha wa muda.

1730117771717.png
 
Afadhali japo maamuzi yamechelewa.viongoz walisubiri hadi damu ziwatoke masikioni ndo wachukue hatua maana walikua wanapuuza sana kelele za mashabiki.
 
Afadhali japo maamuzi yamechelewa.viongoz walisubiri hadi damu ziwatoke masikioni ndo wachukue hatua maana walikua wanapuuza sana kelele za mashabiki.
Mimi Kama mshabiki wa man united mexhi ya Westham na ya champion Europe nilitamani tutandikwe nyingi tu
 
Back
Top Bottom