Pre GE2025 Esther Bulaya: Bado ninaongea lugha ya CHADEMA, ninakipenda hiki chama

Pre GE2025 Esther Bulaya: Bado ninaongea lugha ya CHADEMA, ninakipenda hiki chama

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

The Watchman

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
896
Reaction score
1,427
"Mimi bado ninaongea lugha ileile ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na bado ninaongea lugha ya demokrasia, sasa suala la uanachama au kutokuwa mwanachama ni la maamuzi ya vikao, sasa kwenye jambo hilo, tutaenda kuongea kwenye vikao, kwasababu sisi tulikwenda mahakamani na kudai uanachama ni ishara ya kukipenda chama chako bayana, kwani si kuna vyama vingi, vingine? Mimi ni mwanachama na ninakipenda hiki chama na ninataka uanachama, nikaenda mahakamani, na mahakamani mtu unaenda ukiona haki ipo mahali kwingine? Mahakama ilitoka hukumu kwamba hawa hawakufukuzwa kihalali kwahiyo mahakama ikaamuru baraza kuu liwasikilize tena, bado baraza kuu likiitishwa huko ndipo tutaongea",- Bulaya.

Mbunge wa Viti Maalum Esther Bulaya akizungumza siku ya Jumatatu Februari 24, 2025 kupitia kipindi cha Power Breakfast cha kituo cha habari cha Clouds FM.

Soma pia: Pre GE2025 Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
1740380305448.png
 
"Mimi bado ninaongea lugha ileile ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na bado ninaongea lugha ya demokrasia, sasa suala la uanachama au kutokuwa mwanachama ni la maamuzi ya vikao, sasa kwenye jambo hilo, tutaenda kuongea kwenye vikao, kwasababu sisi tulikwenda mahakamani na kudai uanachama ni ishara ya kukipenda chama chako bayana, kwani si kuna vyama vingi, vingine? Mimi ni mwanachama na ninakipenda hiki chama na ninataka uanachama, nikaenda mahakamani, na mahakamani mtu unaenda ukiona haki ipo mahali kwingine? Mahakama ilitoka hukumu kwamba hawa hawakufukuzwa kihalali kwahiyo mahakama ikaamuru baraza kuu liwasikilize tena, bado baraza kuu likiitishwa huko ndipo tutaongea",- Bulaya.

Mbunge wa Viti Maalum Esther Bulaya akizungumza siku ya Jumatatu Februari 24, 2025 kupitia kipindi cha Power Breakfast cha kituo cha habari cha Clouds FM.

Soma pia: Pre GE2025 Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
View attachment 3247570
Mimi mwenzenu jamani huyu mdada,sio tuu namkubali kichizi,bali kiukweli, 。。。,, naomba nisimalizie,, ila nimeanza kumzimikia long time toka yuko CCM Mbunge wa CCM, Esta Bulaya, ni mbunge pekee aliyesaini petition ya Zitto ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu! Chadema ikomppteza itakuwa imepoteza kitu kikubwa,na wasipoamua mapema kuwasamehe,hawa watatu,Halima Mdee,Ester Bulaya na Ester Matiko,watagombewa kama mpira wa kona na majimbo yao,wakosimama kupitia chama chochote,wana tusua!。
P
 
Back
Top Bottom