Eti Crown CC 2490 ni gari sahihi ya kuanzia maisha kwa watu wa kipato cha chini?

DIKASHWA

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2016
Posts
378
Reaction score
964
Kuna sehemu Facebook nimeona thread ya jamaa anajita mtaalamu wa magari anajinadi eti ni bora tukaachana na vibaby walker tujikite kwenye crown jini mla mafuta, binafsi ametoa chai nyingi, je hii ni kweli au ndo wale mafundi wa chini ya mwembe gari limeharibika shokapu anakimbilia kufungua engine?

UNAJUA MAGARI YANA MFAAA MTU WA HALI YA CHINI??
UNAJUA GARI GANI AMBAYO HAINA MECHANICAL PROBLEMS?
UNAJUA GARI YENYE CC NDOGO YANAGHARIMU ZAID PESA KULIKO YA KAWAIDA??

FUATILIA UZI HUU

Watu wengi wamekuwa vipofu kujiuliza gari ipi ni sahihi kununua kwa gari yake ya kwanza , lakini kabla hujaanza kujikuna kichwa hebu tuweke dondoo za vigezo husika vya kujiuliza.

1. Ubora wa injini
2. Uimara wa body ikiwa mpya na baada kupata misukosuko
3. Matumizi ya mafuta
4. Safety, yaani usalama wa gari
5. Historia la gari husika.
6. Rangi
7. Matumizi, vijijini
8. Gharama ya vipuri
7. Mengineyo

Unaponunua gari jaribu kurejea hayo, usiangalie kigezo kimoja kutoa maamuzi, kwa mfano matumizi ya mafuta unanunua gari mbovu, kisa gari haili mafuta yaani CC chini, sasa jamani gari unataka ile kashata au bagia?

Twendeni taratibu, anaetengeza injini na gari lenyewe ni department tofauti ila anae tengeza body huchangua gari hii tufunge injini gari ili afaulu , ndupo utakuja kujua gari moja ina injini tofauti, kwa sababu tofauti, kukidhi uimara na ulaji mdogo zaidi.

Utakuta IST inafungwa injini karibu 3 tofauti, zipo 1NZ, 2NZ au hata 1az, kila moja ina sababu kwanini wamefunga ikiwa 2Nz unaweza kuikuta na 4wD ili kuhimili nguvu ya 4WD.

Au kama MARK 11 zipo mpaka zina 1Jz au 1G vvti. Sasa marufuku kuikumu gari zile mbovu, basi hebu uliza gari ile ina injini gani.

Familia ya NZ, yaani kina 1Nz au 2NZ zimejizolea umaarufu mkubwa kwa matumiz ya mafuta, ndo maana watu wamekimbilia 1ST haili mafuta , No No sema 1NZ haili mafuta, na imefungwa magari lukuki kama SPACIO, RAUM, OPPA, ALLEX, RUNEX hata VITS, magari yote hayo yamefungwa familia ya NZ kama 1NZ au NZ.

Sasa ukitaka kuchagua gari angalia pia body ya gari , hapo ndo utaamua sasa mimi napenda ulaji mdogo wa mafuta , na napenda familia ya NZ , je nichague mke yupi, mnene,mwembamba,au mfupi ila wote wanawake na wana ladha tofauti hapo naona msomaji umefurahi kusikia radha tofauti. Na hapo ndo utajua utamu wa RAUM, SPACIO NA IST ILA INJINI MOJA.

NIFUPISHE HABARI

GARI AMBAYO IMEKIDHI SIFA KWA MTU ANAENZA MAISHA ni Toyota Mark 11 au GX110 gari hii ikiwa imefungwa 1G vvti , haki ya mungu ni pick ndogo, body vumilivu,injini iliyo shinda tuzo toka mwaka 2000 mpaka 2004.

Teknolojia ilipokuja CROWN CC 2490 imekuja kushika nafasi kwa magari ya kisasa, mfumo wake una VVTI 4, hivo mafuta mule kama kina familia ya NZ, mafuta kidogo mno, sema bei kidogo changamoto sio rafiki kwa maskini aanzae kumiliki gari.

Vigezo vingine tutaendelea kuviweka hapa.
 
Gx110 unasema ni nzuri kwa anayeanza maisha? Unajua bei ya indicator yake ya nyuma?
 
GX 110 au Mark II grand haina indicator inayojitegemea, bali ina taa Complete ambayo ina Revarse Light, Brake Light na Indicator Complete vilivyoungana kwa pamoja
Gx110 unasema ni nzuri kwa anayeanza maisha? Unajua bei ya indicator yake ya nyuma?
 
Ni kuanza na Jeep Grand Cherokee. Hapo maisha yataenda swadata.
 
Asipite tu kidukulilo humu..

Mkuu RRONDO unasemaje hapa
Mr Kichuguu popote ulipo
Gari ni mashine yenye magurudmu manne ambayo inaweza kuendeshwa barabarani kutoka sehemu moja hadi sehemu nyingine wakati muendeshaji wake amekaa ndnai yake. Vinginevyo kuhusu aina ya gari rangi yake na mambo kadhaa ni utashi wa kila mtu. Magufuli anayeenedshwa kwa BMW hamzidi Pope Francis anayeendeshwa kwa kigari kidogo cha Fiat 500L; wote watafika safari zao tu.
 
Kweli kabisa kiongozi, kwa maoni yangu kwa mtu anayeanza maisha ningemshauri atumie gari za Toyota- thamani chini ya milioni 10 na zenye injini isiyozidi Cc 1500.

Kwanza hatoinunua kwa pesa nyingi, mara nyingi zina km chache, vipuli vyake vipo kwa bei nafuu kila sehem na vinaingiliana wakati mwingine, mafuta ni wastani wa km 18 mpaka 22 kwa lita kutegemea na gari na uendeshaji n.k

Gari hizo ni kama
1. IST -10m
2. Sienta -9m
3. Raum -10m
4. Ractis - 9m
5. Fun Cargo- 8.5
6. Porte- 8.8m
7. Vitz- 9m
8. N.k

Kwa msaada zaidi tupigie 0746267740 Kimomwe Motors waagizaji wa Magari kutoka Japan.
 
Nasisitiza tena Crown in Taxi huko Japan. So, usijivimbishe kwenye crown ukajiona mjanja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…