Hapa tunapaswa kufahamu kwamba kuna mambo mengi yanaangaliwa kabla ya kupanga kiwango cha kumlipa msanii. Mathalani, kwenye filamu, mwigizaji anayecheza embarrassing scenes huwa analipwa pesa nyingi zaidi hususani kama ni staa! Leo hii Wema akicheza scenes za kumdhalilisha ni lazima umlipe maradufu kuliko kama angecheza scenes za ofisni. Hakuna asiyefahamu udhalilishaji anaoupata Diamond jukwaani... hawa Tigo nao, walifahamu kabisa what would happen kwa Diamond... katika mazingira kama hayo, unless kama mtu huifahamu vizuri entertainment industry ndipo unaweza kukataa kata kata kwamba Diamond kalipwa mkwanja mrefu!! Vyovyote iwavyo, lazima Tigo walilipia in advance embarrassment ambayo kila mtu aliitarajia kwamba Diamond angekutana nayo.
Jambo lingine ni kwamba kuna tofauti kubwa sana kati ya show zinazokuwa chini ya kampuni/promoters wa kawaida na show zilizo chini ya multinational companies kama Tigo! Don't expect kwamba pesa itakayokuwa inalipwa na Clouds kupitia Fiesta yao inaweza kuwa sawa na inayolipwa na Tigo, Airtel, Coca cola and the like! Hizi kampuni zinakuwa na reference ya viwango vyao tayari kwa level ya wasanii husika! By 2013, Tigo ingemchukulia Diamond kama Local Artist but by 2014/2015, anakuwa considered as International Artist. Hizi multinational companies zina viwango vyao kwa local and international artists. Yote kwa yote, ikiwa habari hizi za Tigo ni shocking news, what about taarifa ambazo ziliandikwa na media za Kenya kwamba Diamond alikunja $100,000 kwenye show ya Kigali?