Eti mwanzilishi wa JamiiForums ni Mzungu?

Inawezekana swali hili lilishawahi kuulizwa, lakini kwa faida yangu na wengine wanaoguswa kujua hili ninaomba majibu ya swali hili, NI NANI MWANZILISHI NA MMILIKI WA JF? MAKAO MAKUU YA JF YAPO WAPI? NA MWISHO JE NI KWANINI JF APP. HAIKUBALI MFUMO WA FREE DATA KAMA ILIVYO KWENYE JF WEBSITE?
 
jf ni jukwaa huru la kutoa ya moyoni ,unapouliza kuwa ni ya nani we nani alikushawishi uingie humu ikiwa huelewi maana ya hili jukwaa.unamtafuta mmiliki iweje ,kama ni ushauri wapo watu humu ndani uliza ujibiwe ,usitumike vibaya kudumaza mawazo ya wanajamii .
 
Ntakujibu suala la data hayo mengine jukwaa la pongezi na malalamishi nafikiri utapata watu sahihi wa kukujibu.

Free data za jamiiforums zinatolewa na kampuni inayoitwa 0.internet.org ambayo inamilikiwa na facebook.

Hii website yenyewe ndio bure na sio jf wala mwananchi wala olx wala website nyengine unayoiona pale.

Chunguza ukiingia kwenye website inakuwa hivi

Jamiiforums-com.0.internet.org/tech-gadget

Hapo haupo jf bali upo 0.internet.org ila unapata tu data za jf. Nina wasiwasi sijui kama tupo safe tukivisit hio website maana ipo kama proxy hivi.

Ile app nayo mule mule ni ya tapatalk na hakuna makubaliano tapatalk iwe bure hivyo lazima uchajiwe hela
 
Ndugu Popomtata

https://www.jamiiforums.com/jf-chit-chat/836606-eti-mwanzilishi-wa-jamiiforums-ni-mzungu-2.html

https://www.jamiiforums.com/habari-...e-melo-mwanzilishi-mwenza-wa-jamiiforums.html

Kuhusu JF
Who are WE?
JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.
Where are we?We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.


For anything related to this site please Contact us.
 
Last edited by a moderator:
jf ni secrety society,huwez jua makao makuu yake wala mmiliki wake. wengi watakao kujib ni makanjanja tu. huwez mpata, hata huyo invinsible ambae katoa welcome note katika kila thread huwez ukamfaham hata kidogo,

ila kuna mods ambao tupo nao humu na hawa mara nying huwa ni wachangiaj wa kwanza hasa thread ambazo huwa ndo zimeandikwa halaf ikapita dakika kadhaa wao huwa wanachangia kiuchokoz ili kuziupdate na watu wengne wazifuatilie. kwa upande wangu ndio hayo mkuu
 

JF founders ni Maxence Melo na Mike Mushi, funga domo lako kama hujui kitu.
 
itakuwa vyema ukiwatafuta na kuwauzia wazo hilo la kuuza Hisa maana naona wewe umenufaika vya kutosha mkuu
 
WaanzilishI wa jamii forums ni Mike mushi na Maxence Melo ( Mchaggavna Mhaya)

Yeah. Ni hao uliowataja. Mmoja namfahamu vizuri kwa kuwa ni mdau wa Civil Engineering pale DIT,lakini ana mudu vizuri sana kazi za Taking off na uandaaji wa Claims/ Valuation Certificates(Quantity Surveyors/Building Economists wanaelewa vizuri.

Hata hivyo miaka fulani hivi akaanza kupenda sana mambo ya IT kwa wakati huo kabla haijaboreshwa na kuitwa ICT. Hapo akaanzisha Jambo Forums. Huyu si mwingine ni kijana Maxence Mello!

Mello kaka bravo,endelea. Mello unakumbuka Block IV pale DIT?
 
Last edited by a moderator:
Kama mjuavyo watu wengi walioanzisha na kumiliki mitandao ya kijamii ni maarufu hasa na matajiri pia.

Je maisha ya CEO wa JF yakoje?

1. Utajiri wake dollar Billion ngapi?
2. Maisha yake?
3. Familia yake, mke, watoto?
4. Hisa zake kwenye makampuni mengine?
5. Elimu yake?

Kiufupi ni uchambuzi kama ambavyo tunaona kwa ma CEO wengine.
 
Net worth 600m Tsh
 
Sio swali baya......na nadhani kuna umuhimu wakujua ni kiasi gani anafaidika na ongezekk la watumiaji wa jf kila siku...
 

Ila kaka Max ana mke jembe kwa kweli.
Mwanamke alikuwa nae bega kwa bega wakati wa kesi yake Kisutu.
Tulikuwa twakutana nae Kisutu.

Maxence Melo ukimuacha wifi yetu, tunaandamana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…