Eti ni kweli mtwara bei ya vyakula inakuwaga juu

Moneyowner

JF-Expert Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
1,423
Reaction score
1,252
Kuna mdau mmoja kanidokeza na kulalamikia maisha ya mtwara kuwa yapo juu hasa upande wa vyakula tofauti na sehemu yoyote tz.
Wenyeji haya ni ya kweli, kwa jicho la ujasiriamali nahisi kuna fursa.
 
Kuna mdau mmoja kanidokeza na kulalamikia maisha ya mtwara kuwa yapo juu hasa upande wa vyakula tofauti na sehemu yoyote tz.
Wenyeji haya ni ya kweli, kwa jicho la ujasiriamali nahisi kuna fursa.
Huyo anaesema hivyo ameshatembea mikoa yote ya tz? Mwambie aende arusha kwanza
 
Labda miaka hii, nimekaa mtwara 2009 na 2010, mimi na jamaa angu tulikuwa tunaenda kula kwenye Cafeteria ya wahindi ilikuwa maeneo ya stendi kuu, wali dagaa shilingi mia tano!
 
Labda miaka hii, nimekaa mtwara 2009 na 2010, mimi na jamaa angu tulikuwa tunaenda kula kwenye Cafeteria ya wahindi ilikuwa maeneo ya stendi kuu, wali dagaa shilingi mia tano!
Hee 500/=? Ubora wa chakula vipi?
 
Huyo anaesema hivyo ameshatembea mikoa yote ya tz? Mwambie aende arusha kwanza
Huu mkumbo kwamba Arusha sijui maisha magumu sijui vitu ghali huwa unaniboa kinoma, yaani ni ulimbukeni fulani watu wanaaminishana...

Kila sehemu kuna vitu bei chee na bei ghali kulingana na uwezo wako na mahitaji yako, Arusha nimeishi pia, sijaona cha ugumu wala nini ni sawa tu na Mbeya, ukitaka vitu ghali utapata na ukitaka vitu bei rahisi utapata..
 
Nadhani labda wenyeji ni ma mwinyi sana hawalimi mazao ya chakula wao ni koroshow tu kwahiyo vyakula wanaimport kutoka mikoa mingine
 
Nadhani labda wenyeji ni ma mwinyi sana hawalimi mazao ya chakula wao ni koroshow tu kwahiyo vyakula wanaimport kutoka mikoa mingine
Mkuu SingleFather, Mtwara misosi ya kutosha tu, kwanza wakati wa chai, ukiagiza chochote, iwe cha na chapati au chai na vitumbua, unapewa na bakuli la maharage, tena yametiwa nazi, for free!

Ila kama unapenda kitimoto, utapata tabu, hapatikani popote hadi kanisani tu, kule Roman.
 
Si kweli kitimoto imejaa kibao kwenye bar za mitaani
 
Mtwara kwa upande wa chakula sio sana, but mavazi ni hatari
 
Labda kwa Mtwara mjini,kama mwezi mmoja nyuma nilikuwa huko katika mji wa masasi kiukweli vyakula vyao ni bei rahisi sana
 
Upo sahihi Mkuu....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…