Eti unalazimisha kupendwa……..Thubutuu…………!

Mtambuzi

Platinum Member
Joined
Oct 29, 2008
Posts
8,809
Reaction score
15,421


Kama unatamani kufanikiwa katika uhusiano wa kijamii, ni muhimu ukakubali ukweli kwamba si kila mtu atakupenda, si kila mtu atavutiwa na ujio wako na hasa kwa mara ya kwanza. Kila mtu anacho kifurushi cha sifa za vitu anavyopenda na asivyopenda ambavyo alivitengeneza siku nyingi.Usidhani una haja ya kujilaumu kama uliyeshindwa iwapo inaonekana mtu fulani hakupendi au havutiwi nawe.

Kama kuna mtu anayekuchukia, sababu ya kukuchukia huko huenda ikawa na uhusiano mdogo na wewe ama huenda isiwe inahusiana kabisa na wewe. Huenda mtu huyo anakuchukia kutokana na kudhani unamuogopa ama kumkwepa, kuona haya ama kuonekana kutokuwa tayari kukaa naye na kuzungumza naye ama kutokuwa katika kiwango kimoja na yeye. Kwa kifupi huenda wewe na mtu huyo, ni watu tofauti msioweza kwenda pamoja hivi sasa.

Usijisikie vibaya na kuanza kujiweka kando na kuwa mpweke kwa kudhani kwamba dosari zako ni kubwa kuliko sifa zako. Kwa kweli, huenda baadhi ya hizo dosari zikawa na mvuto mkubwa kwa watu wengine. Unaweza kuwa umenenepeana sana, lakini ukawa na tabasamu la kuvutia na furaha katika maisha yako. Wapo watu ambao mwili wako huo mkubwa unaweza kuwavutia ama wanaweza wasiuone ama kuonekana kero kwao. Unaweza kuwa na hali mbovumbovu au afya nyondenyonde, lakini ukawa na uwezo mkubwa katika kusakata dansi na mkweli kwa marafiki zako. Ukweli ni kwamba wapo watu wanaotafuta watu wakweli ama watakaowapatia furaha, wema au waungwana na hivyo wewe kuwa na sifa za kujenga nao urafiki.

Ikiwa una shaka kwamba wewe si mzuri wa kutosha wa sura na umbo kuweza kuwavutia marafiki wapya, hasa kwa wanawake. Lazima uelewe kwamba si kila mtu anatafuta uzuri wa sura kwa marafiki zake. Jifunze kupumzisha akili yako. Badala ya kujifunga kwenye mapungufu yako, weka mkazo kwenye sifa zako bora mbele ya watu. Boresha zaidi sifa nzuri ulizo nazo kwani hizo ndizo wale wanaozipenda zitawavuta kuwa karibu na wewe na si vinginevyo.
 
Well said,katika maisha huwezi kupendwa na wote! Lazma kuna watakaokupenda na watakaokuchukia tena bila hata sababu..what is needed ni kuishi maisha yako jinsi ambavyo unaona ni sahihi cause huwezi kumfurahisha kila mtu
 
ndio maana wanasema binadamu wote ni wazuri, kwa sababu kibaya kwako ni kizuri kwa mwingine.
 
Mkuu naona leo umeamua kumwaga mambo ya western tupu! haya bana......
 
Very encouraging....hasa sisi wanawake, we should learn the sign, unalazimisha upendwe na matendo yanaonyesha vinginevyo
 
ukivuka mtazamo wa kuishi kwa ajili ya wengine na kuanza kuishi kwa ajili yako, vitu kama hivi huwa havisumbui.
 
Hii inasaidia sana kwetu tunaohudumia jamii,,,,,maana kila mtu anakua na mtazamo wake kwako,,,,hili si kwa mwanamke tu hata kwetu MALEZ
 
Naomba kutofautiana na wewe dingi (kwanza Jana umelala wapi wewe?)
Hiyo paragraph ya mwisho, I for one huwa sitafuti uzuri wa sura kwa marafiki wala mpenzi. It is the heart and compatibility that matters. So I have the ugliest friends (by the way I look more beautiful nikiwa nao, so ni double advantage hehehehe)

Jioni tutaiongea kesi yako, naona maza anakushindwa sass. Nirushie vocha kabisa kutengeneza mazingara
 
Vipi kwani? Eiyer kalikoroga? Kakutamkia hakupendi? Maana Eiyer nae full madeko sa ingine.

Yaani graph ya mapenzi inazidi kudrop kila siku, sijui anataka kuoa waziri ila kamchomolea nje kwa kuwa yeye ni LY tu! LOL
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…