Eti wataalam, ndoto hii ina maana gani?

Eti wataalam, ndoto hii ina maana gani?

Mr Bluetooth

Senior Member
Joined
Aug 23, 2022
Posts
123
Reaction score
230
Natumai mpo salama..

Nimeota ndoto nipo sehemu kama shuleni ama chuoni au mafunzoni nikawa ni mwanafunzi ninaefanya vizuri kiasi kwamba kuna mwalimu akawa ananipenda sana kama mwanafunzi wake bora, akawa ananiita tunakaa pembeni na ananifundisha mimi peke yangu lile suala kuna mwanafunzi mwenzangu akawa halipendi. Alichokifanya akaenda kwenye idara ya usalama kama vile polisi au takukuru kunisingizia kesi ya kutoa rushwa.

Siku nimekaa na mwalimu nawaona askari na watu wengine wakiambatana na yule mwanafunzi anaenichukia wamekuja kunikamata kwamba nina kesi ya kujibu, mara ghafla nikamuona mama angu mkubwa amekuja ananiambia nenda ukajibu tu mwanangu usiogope nikasema sawa naomba nikamuage mwalimu pale alipokaa.

Nikaenda kumuaga mwalimu nae akanipa maneno ya kunijaza ujasiri nisihofie huko wanakonipeleka nitarudi , nilivyorudi kwa wale watu waliokuja kunikamata nikamwambia yule mwanafunzi mwenzangu alienichongea kesi kwamba "jamaa nikirudi sitokuacha salama"

Wakati tunatoka mke wangu akawa amekuja eneo lile tukapishana nae tulivyofika nje kidogo nikaambiwa mkeo amefariki huko ndani alivyosikia umekamatwa, nikaanza kulia na nililia sana njia yote nakopitishwa kuelekea kituo cha polisi, nikiwa njiani nikawaona watu wawili mke na mume wake (hawa ni majirani) wamekaa wakiambizana 'yule analia mkewe amefariki' na wananiangalia bila hisia zozote yaani ni kama hawasikitishwi wala hawashangai ila wanaangalia tu yale yanayonitokea wakati huo mimi bado ninalia kwa kumpoteza mke wangu.

Ni nini maana ya hii ndoto?

NB: Ni kweli nimeoa.
 
Itakua mkeo anaoujauzito na upo uwezekano kipindi cha ujauzito utapitia magumu mengi lakini utapewa moyo
 
Nimeota ndoto nipo sehemu kama shuleni ama chuoni au mafunzoni nikawa ni mwanafunzi ninaefanya vizuri kiasi kwamba kuna mwalimu akawa ananipenda sana kama mwanafunzi wake bora, akawa ananiita tunakaa pembeni na ananifundisha mimi peke yangu lile suala kuna mwanafunzi mwenzangu akawa halipendi.

Huenda ikawa kuna mambo ambayo umejifunza kuyafanya na unafanikiwa (biashara au kilimo), lakini yupo mtu ambaye ulijifunza/unajifunza au unashirikiana naye kufanya kitu hicho hicho kimoja lakini yeye mambo yanmuendea mrama na kaanza kujenga chuki...
 
siku nimekaa na mwalimu nawaona askari na watu wengine wakiambatana na yule mwanafunzi anaenichukia wamekuja kunikamata kwamba nina kesi ya kujibu,

Kwenye ulimwengu wa kiroho, askari wa polisi mara nyingi humaanisha mapepo wabaya ambao hutumwa na watesi kuja kukukamata na kukuweka kifungoni...
 
mara ghafla nikamuona mama angu mkubwa amekuja ananiambia nenda ukajibu tu mwanangu usiogope nikasema sawa naomba nikamuage mwalimu pale alipokaa.

Nikaenda kumuaga mwalimu nae akanipa maneno ya kunijaza ujasiri nisihofie huko wanakonipeleka nitarudi

Ondoa hofu, huu ndio ujumbe uliopo hapa...

Hofu ni dalili ya kushindwa
 
Wakati tunatoka mke wangu akawa amekuja eneo lile tukapishana nae tulivyofika nje kidogo nikaambiwa mkeo amefariki huko ndani alivyosikia umekamatwa, nikaanza kulia na nililia sana njia yote nakopitishwa kuelekea kituo cha polisi,

Kuota kifo juu ya mtu mwingine si jambo jema, maana huashiria kifo cha mwili, kifo cha kiroho au kunyauka kiuchumi...
 
Baadhi ya watu walio Karibu na wewe hawafurahishwi na mafanikio yako.

1. Itumie hii ndoto kubaini
Kagua mahusiano yako na majirani/ marafiki/ ndugu hapo mwanzo maisha yakiwa ya kawaida na sasa ambapo umepiga hatua, je mahusiano yanaimarika kwa wote Au baadhi mahusiano yanakatika taratibu?

Kama wapo ambao mahusiano yanakatika bila sababu za msingi, fatilia ni Kwa sababu zipi.

2. Kwanini akusingizie kesi ya Rushwa????
Mazingira yako ya utafutaji yanaweza kupelekea wewe kutoa au kupokea rushwa???? Kama Jibu ni ndio uwe na tahadhari unaweza kutoa au kupokea rushwa Alafu hili jambo likajitokeza japo kwenye ndoto ulisingiziwa.

3. Kutoongozana na ndugu zako huko ulikopelekwa.
Kwanini ndugu hawakuwa tayari kuongozana na wewe huko unakopelekwa?? Mahusiano yako na ndugu yakoje??

4. Majirani kutosikitishwa na kifo cha mkeo.
Mahusiano yako na Majirani yakoje???

5. Mwalimu kutoongozana nawewe ulipopata changamoto japo anakupenda.
Kwenye maisha yako kuna watu wanaonesha wanakupenda na kukupa ushirikiano hili uwe nalo makini, hawa watu pengine wanafanya hivi kwa masirahi yao Binafsi na hawana upendo wa kweli. Likitokea tatizo wanaweza kukutelekeza
 
Natumai mpo salama..

Nimeota ndoto nipo sehemu kama shuleni ama chuoni au mafunzoni nikawa ni mwanafunzi ninaefanya vizuri kiasi kwamba kuna mwalimu akawa ananipenda sana kama mwanafunzi wake bora, akawa ananiita tunakaa pembeni na ananifundisha mimi peke yangu lile suala kuna mwanafunzi mwenzangu akawa halipendi. Alichokifanya akaenda kwenye idara ya usalama kama vile polisi au takukuru kunisingizia kesi ya kutoa rushwa.

Siku nimekaa na mwalimu nawaona askari na watu wengine wakiambatana na yule mwanafunzi anaenichukia wamekuja kunikamata kwamba nina kesi ya kujibu, mara ghafla nikamuona mama angu mkubwa amekuja ananiambia nenda ukajibu tu mwanangu usiogope nikasema sawa naomba nikamuage mwalimu pale alipokaa.

Nikaenda kumuaga mwalimu nae akanipa maneno ya kunijaza ujasiri nisihofie huko wanakonipeleka nitarudi , nilivyorudi kwa wale watu waliokuja kunikamata nikamwambia yule mwanafunzi mwenzangu alienichongea kesi kwamba "jamaa nikirudi sitokuacha salama"

Wakati tunatoka mke wangu akawa amekuja eneo lile tukapishana nae tulivyofika nje kidogo nikaambiwa mkeo amefariki huko ndani alivyosikia umekamatwa, nikaanza kulia na nililia sana njia yote nakopitishwa kuelekea kituo cha polisi, nikiwa njiani nikawaona watu wawili mke na mume wake (hawa ni majirani) wamekaa wakiambizana 'yule analia mkewe amefariki' na wananiangalia bila hisia zozote yaani ni kama hawasikitishwi wala hawashangai ila wanaangalia tu yale yanayonitokea wakati huo mimi bado ninalia kwa kumpoteza mke wangu.

Ni nini maana ya hii ndoto?

NB: Ni kweli nimeoa.
Kuna matukio makuu matatu kwenye ndoto yako. Mwalimu anayekufundisha na kumuelewa sana (vizuri), watu kukupeleka police, na kukutana na watu wanaokuangalia tu wakati unamlilia mkeo. Una marafiki wa kweli, ambao hawa unaoongea nao vizuri na wanakupa ushauri mzuri na kukusaidia pale upatapo shida. Hawa ndio yule mwalimu unayemuelewa akikufundusha. Lakini una jamaa wengine wana urafiki na wewe wa kinafiki. Ukipata, wanajifanya kukupongeza, wakati kumbe mioyoni wanachukia mafanikio yako. Kwenye kundi hili, wapo na ambao wanasema "huyu siku akipata matatizo, nitamuacha kama simjuwi, hata ushauri sitampa. Hawa ndio wale waliokupeleka police, na waliokuangalia tu wakati unamlilia mkeo bila hata kukupa pole au faraja ya aina yoyote. Hata hivyo, hili tukio la mwisho la kufiwa, ni roho chafu, hivyo, kemea kwa imani (dini) yoyote unayoshikilia.
 
nikiwa njiani nikawaona watu wawili mke na mume wake (hawa ni majirani) wamekaa wakiambizana 'yule analia mkewe amefariki' na wananiangalia bila hisia zozote yaani ni kama hawasikitishwi wala hawashangai ila wanaangalia tu yale yanayonitokea wakati huo mimi bado ninalia kwa kumpoteza mke wangu.

Kuna watu wameandaliwa kufurahia kukwama au matatizo yako na watu hao si wa mbali bali karibu yako...
 
Back
Top Bottom