Europa League Final: Sevilla yatwaa ubingwa baada ya kuifunga Inter Millan 3-2

DonDonald

JF-Expert Member
Joined
Feb 14, 2011
Posts
2,533
Reaction score
2,709
Timu ya soka ya Sevilla ya Spain usiku huu imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Europa baada ya kuifunga timu ya Inter Millan kwa magoli 3-2

Magoli ya Sevilla yalifungwa na De Jong (2) na Carlos wakati magoli ya Inter yalifungwa na Lukaku (P) na Godin

Habari zaidi kufuatia.
 
Na wameshinda kibabe.

Wameanza kutiwa kamba.

Wakasuluhisha. Wakaongeza. Inter wakasuluhisha.

Sevilla wameongeza cha tatu.

Simba na Sevilla zilitoka nne tano. Man U akaja na akili za penati akaumbuka. Katika kucheza na Sevilla Simba ni bora kuliko Man U.
 
Hii kwa sisi wachumi kuna nadharia ya Kiuchumi inaitwa "Transitivity axiom"

If A=B and
B=C therefore
A=C

Kama Simba alifungwa na Sevilla kwa utofauti wa magoli machache na Sevilla akamfunga Man U kwa tofauti ya magoli mengi basi
Unaweza kuhitimisha kwa kusema Simba ni bora kuliko Man U.

Under Ceteris Peribus.

GGMU[emoji123][emoji123]
 
Mpira una maajabu sana, watu wengi waliweka matumaini yao kwa Inter kushinda mechi ya leo


Duh we jamaa kweli unashangaza, alieweka matumaini kwa inter atakua sio mfuatiliaji wa mpira au hajui mpira. King of europa utamlinganisha na inter au klabu yoyote kutoka uingereza!

They've done it

Sevilla win the Europa league for the sixth time
2006
2007
2014
2015
2016
2020
 

Kabla ya kunishangaa mkuu, soma kwanza post #4 ya mada hii, halafu uone mfano mmoja kwanini nilisema Inter alikuwa anapewa nafasi kubwa ya kushinda pambano la leo
 


Ile ni friendly mechi tu, haina uzito wala advantage kwa sevilla, ndio maana hawakujituma, jamaa walirelux sana.
 
Sevilla hili ni kombe lao.Ukiingia nao finali unaumbuka
Anhaa sisi Arsenal tuliingia fainali Europa na kocha ambaye ilisemekana hilo ni kombe lake.

Kilichotupata tunakijua.

Mambo ya hilo kombe langu (Kama Arsenal FA) hamna hayo ni kujiandaa na juhudi ndiyo zitakuokoa.

Kwa Sevilla niliyoiona ikicheza mpaka kukutana na Man U na Inter inavyoperform kipindi hichi huku Lukaku na Lautaro wakiwa hot ningekua sipo sahihi kusema Sevilla atashinda.

Kwa kuangalia quality ya team overall ilibidi niipe Inter same na waliopiga kura Livescore, wakaipa Inter 50% Sevilla akapewa 25%.
 
Kwenye kujadili timu kwa ssa Arsernal achana nayo.Ukweli Ni kwamba Real Madrid na Uefa ,Sevilla na Europa Ni wafalme wa makombe hayo.
 
Kwenye kujadili timu kwa ssa Arsernal achana nayo.Ukweli Ni kwamba Real Madrid na Uefa ,Sevilla na Europa Ni wafalme wa makombe hayo.
Kwahiyo Real Madrid ndiyo inacheza na PSG vile? Au wanacheza na Bayern?
 
Umenikumbusha Economics; Under ceteris peribus.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…