Everton Football Club mtaa wa Narung'ombe, 1966

Everton Football Club mtaa wa Narung'ombe, 1966

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
EVERTON FOOTBALL CLUB MTAA WA NARUNG'OMBE, 1966

Mwaka wa 1966 wastani wa umri takriban sote tuliokuwa Everton ni miaka 15/16.

Kulikuwa na wenzetu mimi sina taarifa zao kabisa na kwa hakika huwa nawakumbuka:

Mashaka De Stefano, Maufi, Mazola, Jalala, Sultani, Twahir, Ali Kikoti, Hamisi Chai Ndogo, Malu...wako wengi wengine siwakumbuki.

Si rahisi kuamini kuwa lei imepita zaidi ya miaka 60.

Hii picha nimepiga Mnazi Mmoja mwaka wa 1966 na camera yangu nimeipa mgongo sasa Titi Street na nyuma ni Soko Mjinga Kisutu na pembeni mkabala na soko ni Msikiti wa Badawy sasa Rawdha.

Siku hii nakumbuka sikutaka kufanya mazoezi hapa niliposimama nawaangalia Everton wanafanya mazoezi:

Atika Kombo, Jumanne Masimenti (Guu la Ngamia), Juma Abeid (Spencer), Salim Khalil (Gordon Banks), Ahmada (Danny Blanchflour), Rashid Vava, Mohamed Awadh (Chico),Khalid Fadhil (George Young), Iddi Waziri Simba (Rumania), Rehani, Hamim, Abdallah Mkwanda (Ingemar Johansonn), Abdul Kigunya, Guy Hamza...list ni ndefu sana.

Najilaumu kwa nini sikugeuza camera yangu nikawapiga Everton mazoezini.

Mwaka wa 1967 Everton ikawa Saigon.

Screenshot_20200521-003732.jpg

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mohamed Said,
Ahsante sana mkuu kwa historia nzuri. Wengi tunafaidika na kumbukumbu zako za miaka ya nyuma. Hakika umejaaliwa kipaji cha kuhifadhi vitu vingi.

BTW Unamfuatilia askofu Magufuli na hotuba zake kwa Taifa kutoka makanisani kweli?
 
Kweli list ni ndefu, maana sijawaona akina Jafeti, john, Boniface, julius, Peter, william, Gervas e.t.c

Hii list ndefu sana jaman. Tuishie hapo [emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Sent using Jamii Forums mobile app
Tunte...
Waswahili tuna msemo, "Fumbo mfumbie mjinga, mwerevu atatambua."

Haikuwa kuwa sisi katika hali ile ya utoto tukibagua.

Everton iko Mtaa wa Narung'ombe, Kariakoo mwaka wa 1965 wapi utawatoa hao uliowataja?

Kumbuka kuwa Waingereza katika mbinu zao za wagawe uwatawale walikuwa wameweka Mission Quarter makhsusi kwa ajili ya makazi ya Wakristo na ndiyo sehemu pekee kulipokuwa na kanisa.

Haya ndugu yangu ndiyo madhara ya ukoloni.

Ndipo Hamza Mwapachu katika mkutano wa Nansio mwaka wa 1953 baina yake na Abdul Sykes na Ali Mwinyi Tambwe akamwambia Abdul kuwa ni muhimu Nyerere amsaidie achaguliwe awe President wa TAA na mwaka unaofuata 1954 waunde TANU na Nyerere aongoze harakati za kudai uhuru.

Hofu ilikuwa ni kama hii fikra yako.
Mwapachu alichelea TAA na TANU visije kuonekana ni vyama vya Waislam pekee.

Ningeweza kukueleza mengi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kweli list ni ndefu, maana sijawaona akina Jafeti, john, Boniface, julius, Peter, william, Gervas e.t.c

Hii list ndefu sana jaman. Tuishie hapo [emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Sent using Jamii Forums mobile app


Tuntemeke,
Hii ni takribani miaka 60 iliyopita ambapo ktk nchi yetu muingiliano baina ya Jamii kutoka sehemu tofauti za mikoa ilikuwa bado chini sana sana,, hvyo mikoa ilikuwa ikitawaliwa na wenyeji zaidi.

Ni kama vile mm nipost picha ya rafiki zangu ya miaka 50 iliyopita huku Bukoba asilimia kubwa ya majina itakuwa Rwegashora, Mwiga, Rweyemam, Kashaija nk ni nadra kukuta jina la Tarimo au Mwakyusa!!

Hvyo kwa watu waishio pwani miaka hiyo ni kawaida kukuta majina kama hayo aliyoyataja Mzee Mohamed
 
Kweli list ni ndefu, maana sijawaona akina Jafeti, john, Boniface, julius, Peter, william, Gervas e.t.c

Hii list ndefu sana jaman. Tuishie hapo [emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Sent using Jamii Forums mobile app
Duh! sasa weye na mzee mohamed sijui tuwape jina gani maana hata la ukongwe mmepitiliza shukrani wazee wetu tunasoma na kufaidika na kumbukumbu zenu adhimu
 
Back
Top Bottom