pombe kali
JF-Expert Member
- Jun 28, 2014
- 282
- 561
Ni kitu cha ajabu na kushangaza, nina kimashine changu nyumbani ambacho kinatumia petrol, miaka yote nimekuwa nikinunua mafuta kwenye vituo
Siku za hivi karibuni nilienda kituo cha mafuta fulani nikaambiwa kuwa wamekatazwa na EWURA kuuza mafuta kwenye vidumu, nikaomba kumuona msimamizi wa kituo akaniambia kuwa hilo ni agizo. Nikamuuliza kwa generator yangu nitawezaje kujaza mafuta? Akanijibu kuwa natakiwa nilibebe Generator ndiyo niende nalo hapo kituoni
Nikaenda kituo kingine na majibu niliyopata ni yale yale, nikakutana na watu kadhaa ambao magari yao yamezima barabarani na wamekuja na vidumu ambao pia waliambiwa hawaruhusiwi kuweka mafuta kwenye vidumu
Ombi langu kwa mamlaka husika ni kuomba ufafanuzi rasmi kwa siye ambao tunatumia mashine ambazo hazitembei na tunahitaji kuweka mafuta.
Mhudumu lete bia nyingine
Pia soma > KERO - Mafuta ya Petroli kuuzwa kwenye madumu kisha kusafirishwa katika magari ya Abiria sio salama, EWURA -Dodoma mpo?
Siku za hivi karibuni nilienda kituo cha mafuta fulani nikaambiwa kuwa wamekatazwa na EWURA kuuza mafuta kwenye vidumu, nikaomba kumuona msimamizi wa kituo akaniambia kuwa hilo ni agizo. Nikamuuliza kwa generator yangu nitawezaje kujaza mafuta? Akanijibu kuwa natakiwa nilibebe Generator ndiyo niende nalo hapo kituoni
Nikaenda kituo kingine na majibu niliyopata ni yale yale, nikakutana na watu kadhaa ambao magari yao yamezima barabarani na wamekuja na vidumu ambao pia waliambiwa hawaruhusiwi kuweka mafuta kwenye vidumu
Ombi langu kwa mamlaka husika ni kuomba ufafanuzi rasmi kwa siye ambao tunatumia mashine ambazo hazitembei na tunahitaji kuweka mafuta.
Mhudumu lete bia nyingine
Pia soma > KERO - Mafuta ya Petroli kuuzwa kwenye madumu kisha kusafirishwa katika magari ya Abiria sio salama, EWURA -Dodoma mpo?