Sote tunatambua kuwa EWURA wamezuia mafuta ya petrol na Diesel kuuzwa kwenye madumu. Swali langu kwa wale watu ambao wana mashine zinazojienndesha kwa kutumia hiyo nishati watafanyaje?
Kwa mfano nina trekta liko shamba kilomita kadhaa je kila nitakohitaji mafuta lazima niendeshe Trekta kwenda sheli?
Nina mashine ya kupasua mawe inatumia diesel nitafanyaje ili mafuta yafike mashineni?
Nina mashina ya kusaga, kukoboa au kupukuchukuwa nafaka nafanyeje?
Tatizo kubwa mno majuzi ndo nimekutana na hii hali nilikuwa na kazi ya kupiga rangi geti la nyumba yangu tukashauriana na fundi akasema standard thiner kwa ajili ya kuchanganyia rangi ni gharama. Mbadala wake ni mafuta kwenye kutafuta mafuta sasa ilikuwa issue ikabidi twende na thinner make hakukuwa na njia mbadala.
Changamkia biashara, lazima wataruhusu madumu special.
US wanaruhusu madumu special kwa ajili ya kununulia mafuta. Tanzania itabidi tu waruhusu madumu specific.