EXIM bank yaingia Mkataba wa miaka mitatu na ZATI

Blasio Kachuchu

JF-Expert Member
Joined
Sep 7, 2016
Posts
366
Reaction score
243
21 Februari 2025, Zanzibar – Benki ya Exim imeingia mkataba wa miaka mitatu na Chama cha Wawekezaji wa Utalii Zanzibar (ZATI) kwa lengo la kukuza na kuinua sekta ya utalii Zanzibar. Mkataba huo ulisainiwa na Mkuu wa Kitengo cha Fedha kutoka benki ya Exim, Shani Kinswaga pamoja na Mwenyekiti wa Chama cha Wawekezaji wa Utalii Zanzibar (ZATI), Suleiman Ally, ukishuhudiwa na Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale, Mhe. Mudrick Soraga.

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…