Experience yangu ya kilimo cha vitunguu ni negative

Hapo kina sehemu yamefanyika makosa labda ungetuambi wapi umekosea. Mana ukisema umevuna gunia 105 ttu kwa heka Sita haniingi akilini naamini kabisa kuwa Kuna kosa la usimamizi tu
 
Nimekuwa nikifuatilia kwa muda mrefu sana kuhusu kilimo cha vitunguu, kila mtu akitoa uzoefu wake. kila mtu anatoa taarifa zake, wengine za kutia moyo na wengine za kukatisha tamaa. Hivi ukweli ni upi jamani, maana mpaka sasa nimeshindwa kuelewa kwamba ni kilimo chenye faida au hasara?
 

poleni ila hakuna kisicho na kasoro na kwa nchi zinazoendelea hakuna taarifa za uhakika kuhusu masoko. Ulitakiwa ufanye utafiti wa bei kwa mwaka mzima zikoje, kuna mazao kipindi fulani bei nzuri na kipindi bei kutupa. Pia kuna maeneo bei nzuri, kwanini umeuza ghafla na bei chini niliwahi mkuta mama mke wamtu katoa magunia babati kaleta dar then unguja pale alikuwa anategemea kuuza hadi laki mbili na nusu kwa gunia akisubiria meza! Sijaelewa kwanini uuze haraka hivi wakati vinaweza kaa hata mwezi ukivimwaga juani. Usikate tamaa wala usiwe na haraka ya kuuza mazao yote ghafla jaribu kutafuta fursa uza nusu ukipata tenda mahoteli nk unasafirisha nk. Mimi sio mkulima wa shamba but hata mifugo ninmeona watu wakilalamika na kusema ni hasara na wengine vimewainua sana. Jipange tena
 
Mkuu father-xmas hapo napajua vizuri sana hapo niliwahi taka lima ila nikapiga hesabu nikaona bora nika pasue mbao tu!
 
Last edited by a moderator:
Pole sana mkuu,mimi naungana na wewe,kwakweli kilimo cha kutegemea soko la walaji wa moja kwa moja
ni hasara.Namaanisha kilimo kinacholipa ni kile cha kuuza viwandani ambapo unapeleka mzigo mzima na unauza.
bila risk ya kuharibikiwa na bidhaa yako.
Binafsi nina uzoefu na kilimo cha mihogo,nilikodi shamba na kulima kule kisarawe,ukweli mihogo ilikubali
msimu wa kuvuna ukawa ni wakati wa mwezi wa ramadhani,ukweli ni kwamba wanunuzi wa jumla wanaokuja shambani wanataka wakulalie,niliamua kuuleta muhogo mwenyewe mjini nikajikuta napata hela ya wachimbaji na mafuta ya gari na kubaki na mihogo iliyokosa soko nimetengeneza unga nakula mwenyewe.
Wenyeji wananiambia mwakani soko linaweza kuwa zuri nisikate tamaa.
Nilichogundua ni kwamba wenyeji wananufaika na hiyo mitaji yetu hivyo hata siku moja hawawezi kukukatisha tamaa
maana wao ndo wanalima unawalipa,wanapalilia unawalipa,wanavuna unawalipa.soko unatafuta wewe
uwe umepata umekosa wao hawana hasara wanakusubiri msimu ujao.
Kwa ufupi kilimo cha kutegemea soko la mtu kwa mtu na risk,labda mazao ambayo tayari yana viwanda vya kusindika.
 
pana ka ukweli za kuambiwa changanya na zako pia unavyozidi kuongeza ukubwa wa mtaji hasara inapungua, ila kwa mitaji midogo kusafirisha mbali cost.
 

Mkuu pole,

Mchana huu niko Iringa mjini nimefika mara moja kisha narudi porini. Niko na jamaa yangu mmoja, yy alilima pawaga karibu na kijiji cha Mloa, nimetoka huko leo. Ni kwamba jamaa wanalia pia, kitunguu kimewaliza. Wakati napandisha huku Iringa na mdau wangu mmoja alinionyesha plot yake ya vitunguu swaumu pale Isele/Masukanzu Ilula. Kijana aliyekuwa pembeni alisema Ruaha mwaka huu ni kilio sana kwa kitunguu maji.

Waliolima mahindi pia hali sio nzuri, mpunga ni mwingi balaa. Naomba usikate tamaa, ila angalia sana manpower unayotumia. Leo jioni nitakuwa na jamaa, nitajaribu kumuuliza nini kimetokea ghafla. Nikupongeze sana kwa kurudisha feedback.
 
Malila mashamba ya miti bado yanapatikana? kuna jamaa alinielekeza kwako,
 
Last edited by a moderator:
pole sana mkuu father-xmas iyo ndiyo changamoto ya ujasiriamali..mimi apo ruaha mbuyuni nimewahi kulima misimu miwili il amwaka huu machale yalinicheza nikabadili upepo...

1. Ruaha mbuyuni mashamba yake mengi yamechoka na system ya umwagiliaji ni hovyo sana...inawezekana izo ekari 6 zilikua ule upande mbovu ninaoujua.

2.Kilimo cha mbuyuni kinatakiwa timing kwa maana ya kuwahi mapema kuvuna,i.e uvune may au june tar 5 mwisho.

3.bei ya mwaka huu imeshuka sana;na wala haitaki kupanda haielewek sababu ila mara nyingi miez hiyo bei huwa ipo chini.
4.The best option ni kuhifadhi chanjani usubiri bei ipande..ila kitunguu cha chanjani ni kile kinachovunwa kuanzia mwezi wa nane na tisa...

5.pole sana.umeanza na shamba kubwa sana.anza na ekari 2 kwnza..pia pamoja na usimamiz wako inawezekana hukupata mtaalamu mzuri wa kukushauri ...maana kitunguu huwa kinaonekana mapema kwmba kuna kitu ama la....niPM nikupatie kijanamwaminifu ruaha
 
Last edited by a moderator:
Kujiingiza kwenye kilimo ni sawa na kubet roho yako porini kwenye simba na dubu huku ukitegemea kutoka salama.
 
Kujiingiza kwenye kilimo ni sawa na kubet roho yako porini kwenye simba na dubu huku ukitegemea kutoka salama.

Sio kweli... kilimo kinahitaji elimu na maarifa mbali mbali ili ufikie mafanikio. Kama mtu unakurupuka na kujiingiza kwenye kilimo bila elimu na kufuata kanuni za kilimo bora utapata hasara na kwakuwa hauna elimu hautajua hasara imesababishwa na nini...mwisho wa siku utabakia kusema kilimo ni sawa na kubeti..
 

Wanapaita Itipi
 
Hapo kina sehemu yamefanyika makosa labda ungetuambi wapi umekosea. Mana ukisema umevuna gunia 105 ttu kwa heka Sita haniingi akilini naamini kabisa kuwa Kuna kosa la usimamizi tu

Mkubwa katika usimamizi nilikua makini.
Tatizo SOKO.
Mtu unalima kwa gharama kuubwa halafu unaishia kuuza gunia elfu 30.
Inasikitisha sana.
 

Asante mkuu.
Hali kwa sasa inakatisha sana tamaa.
Kila unayeongea nae analalamika.
Waliojaribu kusafirisha ndio wameishia kujuta maana madalali nao wanalalia sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…