Fahad Ag Almahmoud, Kiongozi wa CSP, Auliwa katika Shambulio la Jeshi la Mali

Fahad Ag Almahmoud, Kiongozi wa CSP, Auliwa katika Shambulio la Jeshi la Mali

Strong ladg

Senior Member
Joined
Jul 15, 2021
Posts
170
Reaction score
445
Jeshi la Mali limefanikiwa kumuua kiongozi wa juu wa kundi la kigaidi linalowashambulia raia katika eneo la kaskazini la nchi huyo.

Katika taarifa iliyotolewa kupitia televisheni ya taifa, jeshi la Mali limesema lilifanikiwa kumuua Fahad Ag Al Mahmoud pamoja na viongozi wengine muhimu saba mnamo tarehe 1 Disemba 2024 baada ya kuwashambulia kwa droni.

Jeshi la Mali limefanikiwa kupata ushindi dhidi ya magaidi tangu lichukue madaraka baada ya mapinduzi. Ushindi muhimu na unaokumbukwa zaidi ni kukombolewa kwa mji wa Kidal mnamo Novemba 2023 ambao ulikuwa umeshikiliwa na magaidi kwa takribani miaka 10.

Majeshi ya Ufaransa pamoja na yale ya kulinda amani ya umoja wa mataifa hayakufanikiwa kupata ushindi dhidi ya magaidi licha ya kuwepo nchini Mali kwa karibu miaka kumi.

Picha: Kiongozi aliyeuwawa.
CHANZO: Shirika la habari la Mali( ORTM)

 

Attachments

  • 20241201_170146.jpg
    20241201_170146.jpg
    63.1 KB · Views: 5
Kabisaa. Mali hakuna kiwanda cha silaha, wao wanazitoa wa
Kabisa na ndo mujue dunia ilivyo,awa wazungu wakipigana na hawa wanaowaita magaidi, uwezi Kuta wakimtafuta au kutaka kujua tu nani anaowapa silaha , ilo swali uliojiuliza dunia inajitahidi kulipuuza lakini ni swali linalohitaji majibu ya kueleweka haswa
 
Jeshi la Mali limefanikiwa kumuua kiongozi wa juu wa kundi la kigaidi linalowashambulia raia katika eneo la kaskazini la nchi huyo.

Katika taarifa iliyotolewa kupitia televisheni ya taifa, jeshi la Mali limesema lilifanikiwa kumuua Fahad Ag Al Mahmoud pamoja na viongozi wengine muhimu saba mnamo tarehe 1 Disemba 2024 baada ya kuwashambulia kwa droni.

Jeshi la Mali limefanikiwa kupata ushindi dhidi ya magaidi tangu lichukue madaraka baada ya mapinduzi. Ushindi muhimu na unaokumbukwa zaidi ni kukombolewa kwa mji wa Kidal mnamo Novemba 2023 ambao ulikuwa umeshikiliwa na magaidi kwa takribani miaka 10.

Majeshi ya Ufaransa pamoja na yale ya kulinda amani ya umoja wa mataifa hayakufanikiwa kupata ushindi dhidi ya magaidi licha ya kuwepo nchini Mali kwa karibu miaka kumi.

Picha: Kiongozi aliyeuwawa.
CHANZO: Shirika la habari la Mali( ORTM)

Ugaidi utaendelea kuitesa dunia. Hata nchi zenye amani kama Tanzania tukiendelea kufumbia macho mauaji ya kiholela tunafungulia mlango wa ugaidi ktk nchi. Wahusika wajitathmini na kuchukuwa hatua stahiki.
 
Ugaidi utaendelea kuitesa dunia. Hata nchi zenye amani kama Tanzania tukiendelea kufumbia macho mauaji ya kiholela tunafungulia mlango wa ugaidi ktk nchi. Wahusika wajitathmini na kuchukuwa hatua stahiki.
Chanzo Cha ugaidi Ni Nini?
 
Makundi ya wazungu haya
Haya makundi yalitoka Libya baada kuanguka kwa utawala Kanali Muamar Gadafi. Na sio wote ni Magaidi wengine ni Separatists wanataka kuunda Taifa lao wenyewe wanaliita Azawad.
 
Chanzo Cha ugaidi Ni Nini?
1. Kundi linalo asi serikali baada ya kuona wanateswa na kunyanyaswa na serikali iliyopo madarakani bila hatia au kwa uonevu ( hapa ndipo tanzania tutaelekea baada ya watu kuchoka na kupata pa kuanzia)

2. Kundi ambalo linaona serikali haitaki kukidhi matakwa yao yaweza kuwa matakwa ya kisiasa au ya kiimani wakati fulani hata kiuchumi hivyo wana ishinikiza serikali kutekeleza matakwa yao kwa mtutu wa bunduki ( hii kwa tanzania bado bado sana ila tukilemaa na tukawaendekeza baadhi ya watu wenye misimamo mikali ya siasa na misimamo mikali ya dinii watatupeleka huko)

Hayo ndiyo mambo makuu yanayo chochea kutokea kwa ugaidi , na hapa inaweza ikawa ugaidi ukaanzia ndani nchi kisha kupata nguvu toka nje ya nchi au makundi yafananayo au ukaanzia nje na ukaingizwa ndani ya nchi.
 
Yule Junta alifanya makosa kuachana na yale makubaliano na wale Watuareg.

Baada ya kuona Mamluki wa Wagner wamewasili Mali akajiona kuwa yeye ndiye yeye.
 
1. Kundi linalo asi serikali baada ya kuona wanateswa na kunyanyaswa na serikali iliyopo madarakani bila hatia au kwa uonevu ( hapa ndipo tanzania tutaelekea baada ya watu kuchoka na kupata pa kuanzia)

2. Kundi ambalo linaona serikali haitaki kukidhi matakwa yao yaweza kuwa matakwa ya kisiasa au ya kiimani wakati fulani hata kiuchumi hivyo wana ishinikiza serikali kutekeleza matakwa yao kwa mtutu wa bunduki ( hii kwa tanzania bado bado sana ila tukilemaa na tukawaendekeza baadhi ya watu wenye misimamo mikali ya siasa na misimamo mikali ya dinii watatupeleka huko)

Hayo ndiyo mambo makuu yanayo chochea kutokea kwa ugaidi , na hapa inaweza ikawa ugaidi ukaanzia ndani nchi kisha kupata nguvu toka nje ya nchi au makundi yafananayo au ukaanzia nje na ukaingizwa ndani ya nchi.
Nani anawapa silaha magaidi? Nani anawapa mafunzo? Nani anawapa chakula? Nani anawatibu wakiumia? Sawa tuseme sipendi serikali kama sina silaha naweza kufanya chochote? siwezi. Na kama wanachukia serikali kwanini wanaua raia? Mfano magaidi wa Syria wanapinga serikali lakini cha kushangaza wanaua raia! Kwanini wasiende ikulu kumuua Rais? Au walipue ofisi za serikali ? Wanaua raia ambao Hata hawahusiki. Wanataka Nini?
 
Yule Junta alifanya makosa kuachana na yale makubaliano na wale Watuareg.

Baada ya kuona Mamluki wa Wagner wamewasili Mali akajiona kuwa yeye ndiye yeye.
Junta alikuta asilimia 40 ya nchi inashikiliwa na magaidi na Kila Siku walikuwa wanazidi kuchukua eneo jipya wakati viongozi wanasiasa wanawategemea Ufaransa wawaue magaidi. Ilikuwa sehemu ya makubaliano kwamba hao magaidi waendelee kuchukua sehemu ya nchi kila siku? Simtetei Junta lakini nawaza labda hisia zilimzidi akaona maamuzi pekee ni kuwapiga pasipo kukumbuka makubaliano? Sijui kwa kweli.
 
1. Kundi linalo asi serikali baada ya kuona wanateswa na kunyanyaswa na serikali iliyopo madarakani bila hatia au kwa uonevu ( hapa ndipo tanzania tutaelekea baada ya watu kuchoka na kupata pa kuanzia)

2. Kundi ambalo linaona serikali haitaki kukidhi matakwa yao yaweza kuwa matakwa ya kisiasa au ya kiimani wakati fulani hata kiuchumi hivyo wana ishinikiza serikali kutekeleza matakwa yao kwa mtutu wa bunduki ( hii kwa tanzania bado bado sana ila tukilemaa na tukawaendekeza baadhi ya watu wenye misimamo mikali ya siasa na misimamo mikali ya dinii watatupeleka huko)

Hayo ndiyo mambo makuu yanayo chochea kutokea kwa ugaidi , na hapa inaweza ikawa ugaidi ukaanzia ndani nchi kisha kupata nguvu toka nje ya nchi au makundi yafananayo au ukaanzia nje na ukaingizwa ndani ya nchi.
Hupaswi kuwaita magaidi Ila waasi.
 
Junta alikuta asilimia 40 ya nchi inashikiliwa na magaidi na Kila Siku walikuwa wanazidi kuchukua eneo jipya wakati viongozi wanasiasa wanawategemea Ufaransa wawaue magaidi. Ilikuwa sehemu ya makubaliano kwamba hao magaidi waendelee kuchukua sehemu ya nchi kila siku? Simtetei Junta lakini nawaza labda hisia zilimzidi akaona maamuzi pekee ni kuwapiga pasipo kukumbuka makubaliano? Sijui kwa kweli.
Kuna Kikundi kimoja kinapogania More Autonomy kwenye eneo lao Touregs na kuna kundi lingine lingine ambalo ni Magaidi.

Hilo kundi linalotaka More Autonomy lilikuwa limekubaliana na Serikali ya Bamako tatizo la Junta kayafuta makubaliano kwa kupewa Kiburi na ujio wa Wagner.
 
Jeshi la Mali limefanikiwa kumuua kiongozi wa juu wa kundi la kigaidi linalowashambulia raia katika eneo la kaskazini la nchi huyo.

Katika taarifa iliyotolewa kupitia televisheni ya taifa, jeshi la Mali limesema lilifanikiwa kumuua Fahad Ag Al Mahmoud pamoja na viongozi wengine muhimu saba mnamo tarehe 1 Disemba 2024 baada ya kuwashambulia kwa droni.

Jeshi la Mali limefanikiwa kupata ushindi dhidi ya magaidi tangu lichukue madaraka baada ya mapinduzi. Ushindi muhimu na unaokumbukwa zaidi ni kukombolewa kwa mji wa Kidal mnamo Novemba 2023 ambao ulikuwa umeshikiliwa na magaidi kwa takribani miaka 10.

Majeshi ya Ufaransa pamoja na yale ya kulinda amani ya umoja wa mataifa hayakufanikiwa kupata ushindi dhidi ya magaidi licha ya kuwepo nchini Mali kwa karibu miaka kumi.

Picha: Kiongozi aliyeuwawa.
CHANZO: Shirika la habari la Mali( ORTM)

Good job
Chinja hao makobazi ndugu zake Malaria 2
 
Back
Top Bottom