Fahamu jinsi matapeli wanatumia noti ya Shilingi 500 kuibia watu

Nyanda Banka

JF-Expert Member
Joined
Mar 14, 2023
Posts
304
Reaction score
1,054
Huenda sio Mara yako ya kwanza kukutana na matangazo ya kwamba hizi noti zinatafutwa na zinanunuliwa kwa bei kubwa Sana. Huu ni utapeli ambao unafanyika kwa njia zifuatazo👇🏿

👉Baada ya wewe kuzitafuta na kuwa nazo mfano mbili, utampgia huyo aliyesema anazinunua, labda moja Tsh 20k, hivyo atakupa kwa zote mbili elfu 40. Na akishazinunua atakuambia umtafutie na zingine nyingi ili umpe na kwamba Ana shida nazo Sana.👇

👉Baada ya hapo yeye huyohuyo atatuma mtu mwingine (tapeli mwenzake) ambao wapo kundi moja atakupigia simu na kukuambia kuwa anazo hizo noti za Tsh 500, hata 10 hivi.

👉🏿Wewe kwa kuwa ulishapata mteja na unajua ni wa uhakika utafanya juu chini upate pesa uzinunue hata kwa elfu 10. Kila moja, Kama anazo 10 utampa laki 1.

👉Baada ya kuzipata utampgia mteja wako aliekuahidi uzitafute utakuta hapatikani kabisa kwenye simu.

👉Na hapo ndio utakapokuwa umetapeliwa.😀

 
Haki ya mungu watu wabunifu sana.
 
🤣🤣 Utapeli unaitaji Capital, kama ilivyo kwenye biashara.
 
Serikali inaenda kuzitoa kwenye mzunguko
Ondoa shaka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…