Fahamu kuhusu 'Ship Bunkering'

Offshore Seamen

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2018
Posts
5,489
Reaction score
14,091
Ship Bunkering-Huu ni ujazaji wa mafuta katika meli kutoka meli moja kwenda nyingine yenye huitaji au vilainishi (lubes).Meli ujaza mafuta kama ilivyo kwenye gari ambapo gari uenda kituo cha mafuta.

Mafuta ambayo hujazwa ni Diesel ya kawaida na Diesel nzito(Heavy Fuel Oil) pamoja oil za kulainishia mashine.

Ship bunkering ufanyika kwa aina mbili.

1. Gari kubwa ya mafuta kwenda bandarini
Hapa lori la mafuta huenda bandarini na kushusha mafuta kwenye meli husika. Hii hufanyika sana kwenye meli ndogo,boti za abiria na meli za uvuvi.

Hii Tanzania imekuwa ikifanya na makampun ya mafuta kama Total, Puma na Oilcom.

2. Meli ya mafuta kwenda kujaza meli nyingine
Meli yenye mafuta huenda kando ya meli kubwa kuijaza mafuta na hii ufanyika baharini kwa meli zile ambazo haziwezi kuingia bandarini kwa sababu za ukubwa au kutokana na kuendelea na safari.

Hii ufahamika kama ship to ship bunkering. Miaka ya nyuma Tanzania tulikuwa tunafanya hii kupitia kampuni ya GBP. Kwa sasa hii haifanyiki na kusini mwa Africa meli kubwa hutegemea kujaza mafuta pwani za Angola na Africa kusini.

Biashara hii ni kubwa maana meli kubwa huitaji maelfu ya tani za mafuta na vilainishi (lubes).Uuzaji wa mafuta kwa meli umerahisha kupatikana ajira,kodi na mafuta kwenye nchi wanazofanya ship bunkering.

 
Mkuu unapenda sana mambo ya bahari

Inapendeza sana
 
sawa mkuu,jamaa yako ndio namalizia malizia bunker pande za meditranian,heavy fuel low sulpher 1700 cubic metres 😃

 
Tanzania huwa inarudi nyuma kwanini lakini ? Hao GBP ilikuwa wakaondoka ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…