Fahamu kuhusu Sport Fishing

Fahamu kuhusu Sport Fishing

Offshore Seamen

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2018
Posts
5,489
Reaction score
14,091
Sport Fishing ni Uvuvi wa Samaki katika bahari, Maji ya ziwa, bwawa au mto Kwa ajili ya kujifurahisha, burudani au Mashindano. Hii ni aina tofauti na Uvuvi wa Samaki wa biashara na kujikimu, huu ni rahisi Sana mtu anayevua anaweza akawa kwenye Boti ndogo au pembezoni mwa bahari/Ziwa/bwawa/mto.

images (9).jpeg


Mvuvi hutumia zana za kawaida kama fimbo yenye mshipi(rod and reel), ndoano, chambo (baits), mkuki wa kuvulia au mtego mdogo wa uvuvi.

images (7).jpeg


Pichani ni Rod and Reel(Hiyo fimbo na mashine ya kusogezea mshipi au Kamba ya ndoano, na artificial baits (chambo za plastic)

Sport Fishing unapofanya lazima uwe na kibali na kinatolewa na wizara ya Uvuvi pia Kuna Sheria zake na maeneo ambayo unaruhusiwa iwe baharini au ziwani.

images (3).jpeg


Baadhi ya mataifa makubwa Duniani kila mwaka hufanya Mashindano ya uvuvi na Kuna chombo kinachosimamia na kutoa tuzo pia kutunza rekodi ambacho kinaitwa International Game Fish Association (IGFA). Hawa pia wanashirikiana na Serikali na Mamlaka mbalimbali Duniani kulinda na kutunza mazingira na viumbe wa majini.

IGFA_Museum_Front_Name.JPG


Sport Fishing ni zaidi ya utalii na haina madhara kwa Samaki au mazingira ya Bahari au Ziwa. Mtu hata akimvua Samaki mdogo anaruhusiwa kumrudisha Tena na Sasa Kuna vifaa vya kisasa pia Sheria na kibali kinamkataza mtu kuondoka na baadhi ya Samaki kama wametunzwa Kwa kazi maalumu.

Kwa Sheria ya uvuvi ya Tanzania ya mwaka 2003, Sport Fishing naona imeongelewa kidogo sana kwenye page ya 22 kifungu (t) kwenye Mamlaka ya Director of Fisheries vitu anavyoweza kuzuia visifanyike kama vinahatarisha uvuvi.

Kama Sheria itaboreshwa itaruhusu utalii wa Sport Fishing kufanyika maeneo mengi na kutoa fursa kwa watu wengi.
 
Mkuu hivi ni Sport fishing (uvuvi wa kimichezo) au Spot fishing (uvuvi mdogo)
 
Mkuu hivi ni Sport fishing (uvuvi wa kimichezo) au Spot fishing (uvuvi mdogo)
Ni Sport Fishing, Uvuvi mdogo(Subsistence Fishing) huu ni Kwa ajili ya kujikimu mvuvi huvua Kwa ajili ya kuuza Samaki na chakula. Uvuvi mdogo lengo ni kujikimu anaweza akatumia boti ya kuchonga isiyotumia injini au akavua kando ya bwawa,Ziwa,mto au bahari.
 
Sport Fishing ni Uvuvi wa Samaki katika bahari, Maji ya ziwa, bwawa au mto Kwa ajili ya kujifurahisha, burudani au Mashindano. Hii ni aina tofauti na Uvuvi wa Samaki wa biashara na kujikimu, huu ni rahisi Sana mtu anayevua anaweza akawa kwenye Boti ndogo au pembezoni mwa bahari/Ziwa/bwawa/mto.

View attachment 2092223

Mvuvi hutumia zana za kawaida kama fimbo yenye mshipi(rod and reel), ndoano, chambo (baits), mkuki wa kuvulia au mtego mdogo wa uvuvi.

View attachment 2092224

Pichani ni Rod and Reel(Hiyo fimbo na mashine ya kusogezea mshipi au Kamba ya ndoano, na artificial baits (chambo za plastic)

Sport Fishing unapofanya lazima uwe na kibali na kinatolewa na wizara ya Uvuvi pia Kuna Sheria zake na maeneo ambayo unaruhusiwa iwe baharini au ziwani.

View attachment 2092225

Baadhi ya mataifa makubwa Duniani kila mwaka hufanya Mashindano ya uvuvi na Kuna chombo kinachosimamia na kutoa tuzo pia kutunza rekodi ambacho kinaitwa International Game Fish Association (IGFA). Hawa pia wanashirikiana na Serikali na Mamlaka mbalimbali Duniani kulinda na kutunza mazingira na viumbe wa majini.

View attachment 2092222

Sport Fishing ni zaidi ya utalii na haina madhara kwa Samaki au mazingira ya Bahari au Ziwa. Mtu hata akimvua Samaki mdogo anaruhusiwa kumrudisha Tena na Sasa Kuna vifaa vya kisasa pia Sheria na kibali kinamkataza mtu kuondoka na baadhi ya Samaki kama wametunzwa Kwa kazi maalumu.

Kwa Sheria ya uvuvi ya Tanzania ya mwaka 2003, Sport Fishing naona imeongelewa kidogo sana kwenye page ya 22 kifungu (t) kwenye Mamlaka ya Director of Fisheries vitu anavyoweza kuzuia visifanyike kama vinahatarisha uvuvi.

Kama Sheria itaboreshwa itaruhusu utalii wa Sport Fishing kufanyika maeneo mengi na kutoa fursa kwa watu wengi.

Wenye interest na shughuli hiyo tuwasiliane PM niwasaidie kupata vibali na connection zingine.

Maisha yanahitaji furaha sana msijibane bane
 
Wenye interest na shughuli hiyo tuwasiliane PM niwasaidie kupata vibali na connection zingine.

Maisha yanahitaji furaha sana msijibane bane
Mwezi ujao nitakuunganisha na mtu anataka kuja kufanya hii biashara yupo nje, anatafuta kibali katika Ziwa.
 
Ni Sport Fishing, Uvuvi mdogo(Subsistence Fishing) huu ni Kwa ajili ya kujikimu mvuvi huvua Kwa ajili ya kuuza Samaki na chakula. Uvuvi mdogo lengo ni kujikimu anaweza akatumia boti ya kuchonga isiyotumia injini au akavua kando ya bwawa,Ziwa,mto au bahari.
Kwa kukazia tu, uvuvi huu wa kujikimu, (mdogo mdogo), wa akina yakhe, unaitwa artisanal fishing
 
Wenye interest na shughuli hiyo tuwasiliane PM niwasaidie kupata vibali na connection zingine.

Maisha yanahitaji furaha sana msijibane bane
Unaweza ukashare pia namba ya utolewaji vibali watu waelewe. Mimi nitakutafuta pia kama mteja wangu wa boti anataka hii biashara, sikutaka kwenda Wizarani direct maana anadema dema kuwekeza huwa kwenye kutoa ushauri tunamsaidia mteja na namna ya kupata vibali katika Mamlaka tofauti.
 
Kwa kukazia tu, uvuvi huu wa kujikimu, (mdogo mdogo), wa akina yakhe, unaitwa artisanal fishing
Sahihi Mkuu, Mimi huwa napenda neno Subsistence Fishing ila wale wavuvi ndio naona neno zuri kuwaita Artisanal Fisherman lugha ya Malkia ni Pana.

Burudani tosha maisha Yao ni usanii kuanzia boti zao,nyavu,vikapu wakivua Samaki wa kula na kuuza anapeleka chombo Pwani hataki shida.
 
Sahihi Mkuu, Mimi huwa napenda neno Subsistence Fishing ila wale wavuvi ndio naona neno zuri kuwaita Artisanal Fisherman lugha ya Malkia ni Pana.

Burudani tosha maisha Yao ni usanii kuanzia boti zao,nyavu,vikapu wakivua Samaki wa kula na kuuza anapeleka chombo Pwani hataki shida.
Noma sana. Na moja kati ya vitu hawataki kuelewa ni pale ukiwaambia kwamba watumie njia endelevu za uvuvi maana rasilimali iliyopo baharini inaweza kwisha wakakosa kitoweo.

Wao wanaamini kwamba bahari ni kubwa mno na mwenyezi Mungu kaweka samaki wengi mno kwa ajili yao.
 
Noma sana. Na moja kati ya vitu hawataki kuelewa ni pale ukiwaambia kwamba watumie njia endelevu za uvuvi maana rasilimali iliyopo baharini inaweza kwisha wakakosa kitoweo.

Wao wanaamini kwamba bahari ni kubwa mno na mwenyezi Mungu kaweka samaki wengi mno kwa ajili yao.
"Sea never dry" Wanafata huu msemo.
Wanavua kidogo Cha Leo wanaenda kupumzika. Sisi Kwa uvuvi tunaofanya ni 19% tu Kwa upande wa Bahari, bado hatujaweza kuvuna hata nusu ya rasilimali tuliyonayo.

Nchi kama Japana,Norway wao wamevuna hasa mazao ya Bahari mpaka imekuwa exhausted na Kuna Sheria kibao za kuvua Kwa Sasa
 
"Sea never dry" Wanafata huu msemo.
Wanavua kidogo Cha Leo wanaenda kupumzika. Sisi Kwa uvuvi tunaofanya ni 19% tu Kwa upande wa Bahari, bado hatujaweza kuvuna hata nusu ya rasilimali tuliyonayo.

Nchi kama Japana,Norway wao wamevuna hasa mazao ya Bahari mpaka imekuwa exhausted na Kuna Sheria kibao za kuvua Kwa Sasa
Hakika.
Lakini pamoja na hayo, tunapaswa kuwawezesha wavuvi wetu waweze kwenda kuvua kwenye maji makuu ili wapate "samaki wa maana".

Hii pia itawafanya waachane au wapunguze presha ya kuhangaikia huku kwenye kina kifupi maana huku ndiko "critical habitats" za samaki ziliko.
Hizo critical habitats ni mazalia, malisho na maficho. Ukiziharibu hizo tu, consequences are generational.

Tuendelee kuwapa elimu juu ya uvuvi endelevu kwenye maeneo yao lakini pia tutafute namna ya kuwajumuisha kwenye medium scale na large scale (commercial) fishing.


Sijui hata hiyo TAFICO inaanza lini operations, sijui wana mipango gani ya kuwa incorporate hawa wavuvi wadogo kwenye shughuli zao.

Tuendelee kunywa mchuzi, nyama tutazikuta chini.
 
Sport Fishing ni Uvuvi wa Samaki katika bahari, Maji ya ziwa, bwawa au mto Kwa ajili ya kujifurahisha, burudani au Mashindano. Hii ni aina tofauti na Uvuvi wa Samaki wa biashara na kujikimu, huu ni rahisi Sana mtu anayevua anaweza akawa kwenye Boti ndogo au pembezoni mwa bahari/Ziwa/bwawa/mto.

View attachment 2092223

Mvuvi hutumia zana za kawaida kama fimbo yenye mshipi(rod and reel), ndoano, chambo (baits), mkuki wa kuvulia au mtego mdogo wa uvuvi.

View attachment 2092224

Pichani ni Rod and Reel(Hiyo fimbo na mashine ya kusogezea mshipi au Kamba ya ndoano, na artificial baits (chambo za plastic)

Sport Fishing unapofanya lazima uwe na kibali na kinatolewa na wizara ya Uvuvi pia Kuna Sheria zake na maeneo ambayo unaruhusiwa iwe baharini au ziwani.

View attachment 2092225

Baadhi ya mataifa makubwa Duniani kila mwaka hufanya Mashindano ya uvuvi na Kuna chombo kinachosimamia na kutoa tuzo pia kutunza rekodi ambacho kinaitwa International Game Fish Association (IGFA). Hawa pia wanashirikiana na Serikali na Mamlaka mbalimbali Duniani kulinda na kutunza mazingira na viumbe wa majini.

View attachment 2092222

Sport Fishing ni zaidi ya utalii na haina madhara kwa Samaki au mazingira ya Bahari au Ziwa. Mtu hata akimvua Samaki mdogo anaruhusiwa kumrudisha Tena na Sasa Kuna vifaa vya kisasa pia Sheria na kibali kinamkataza mtu kuondoka na baadhi ya Samaki kama wametunzwa Kwa kazi maalumu.

Kwa Sheria ya uvuvi ya Tanzania ya mwaka 2003, Sport Fishing naona imeongelewa kidogo sana kwenye page ya 22 kifungu (t) kwenye Mamlaka ya Director of Fisheries vitu anavyoweza kuzuia visifanyike kama vinahatarisha uvuvi.

Kama Sheria itaboreshwa itaruhusu utalii wa Sport Fishing kufanyika maeneo mengi na kutoa fursa kwa watu wengi.
Habari mkuu, so far kuna jamaa wanaofanya kama fishing kama game/sport hapa Tanzania?
 
Back
Top Bottom