LIKUD
JF-Expert Member
- Dec 26, 2012
- 18,037
- 33,681
Said Mwamba a.k.a Kizota alikuwa ni mchezaji mahiri kwa klabu ya Dar Es salaam Young Africans na timu ya taifa ya Tanzania. Watu wengi hawafahamu kwa nini mchezaji huyu aliitwa ' Kizota '.
Kizota ni jina la ukumbi wa mikutano ya Chama Cha Mapinduzi uliopo mjini Dodoma.
Vikao na mikutano mingi inayo fanyika katika ukumbi wa Kizota huwa ina ongozwa na Mwenyekiti wa Chama.
Kama hiyo haitoshi, vikao hivyo vilikuwa vinaongozwa kwa mujibu wa falsafa ya " Zidumu Fikra Sahihi za Mwenyekiti wa Chama ".
Hivyo basi kila mara mwenye kiti wa chama alipokuwa alipokuwa akitoa hoja, katibu wa kikao alikuwa akiwauliza wanachama " KUNA SWALI HAKUNA SWALI" ., wananchi waliitikia " HAKUNA SWALI !"
Back To Said Mwamba Kizota.
Said Mwamba alisajiliwa na Yanga mwaka 1986. Mechi yake ya kwanza ilikuwa ni dhidi ya CDA ya Dodoma na ilichezwa katika uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.
Unaambiwa siku hiyo mpira ulimkubali kweli Kizota. Basi jamaa alikuwa kila akifanya tukio uwanjani, shabiki mmoja anawauliza wenzake " JAMANI KUNA MWENYE SWALI"..Watu nao walijibu " HAKUNA SWALI"
Kwa mfano, kuna ngoma moja, jamaa alichukua boli, akaweka gambani, akatuliza chini, akafanya mipango, adui akaja, akapigwa kanzu halafu ngoma ikaoshwa mbele.
Mashabiki wa upande mmoja wakawauliza wenzao " KUNA MWENYE S WALI " wenzao wakajibu ' HAKUNAAA"
BASI KUANZIA SIKU, HIYO SAID MWAMBA, AKAWA ANAITWA " KIZOTA !"