KAGAMEE
JF-Expert Member
- Dec 20, 2013
- 4,457
- 5,454
Habar wakuu,bila shaka hakuna atakayebisha kuwa Kigoma imejariwa kuwa na wachezaji wazuri na tegemeo.Lakini wachezaji wengi wameponzwa na uongoz wa michezo mkoa.Kuna mtendaji mkuu ambaye ni Karibu kwa sasa anaitwa MBUYA huyu amekuwa akipokea rushwa kutoka kwa baadhi ya timu zenye pesa na kukaa meza moja na marefa na kuumaliza mchezo mezani.Mfano juzi juzi nilikuwa nusu fainali ya kutafuta timu ya kucheza fainali ili kupata timu ya mkoa kati ya RED STAR VS MUNANILA STAR marefa walionesha mazingira yote ya Rushwa kwa kutoa kadi ,magoli yasiyofaa,pembeni nilikuwa nmesimama na mtu wa TAKUKURU alionekana kushangazwa na maamuzi ya Refa dk zote 90,nikamuuliza kama unashangaa ww na Mimi nitafanyaje?kwann TAKUKURU msiingilie kati?alibak kucheka tu .Pia katibu huyu amekuwa akitambia watu kuwa ataipitisha timu aipendayo na hata timu ikionewa haina pa kwenda kwa sababu ana connection na viongozi juu.Timu zote za mkoa wa Kigoma zinapanga kukutana kufanya vikao vya siri juu ya hatima ya timu zao.
Rai yangu,naomba viongozi wa ngazi za juu muangalie chama cha moira mkoa wa Kigoma kwa jicho pevu.Viongozi,marefa wanapokea rushwa waziwazi bila kuogopa hata kasi ya Magufuli.Refa maarufu kwa kupokea rushwa ni RAMBO huyu makocha wanamjua kama mi mlevi sana,ukimpata tu 5000 basi NYEUPE atakwambia ni NYEUSI (Nina ushahidi)
VIONGOZI WA TFF MKIKAA KIMYA BASI MTASHUHUDIA MAKUU AU KUSIKIA MAKUU WAKITENDEWA HAWA VIONGOZI WA MICHEZO MKOA.
Rai yangu,naomba viongozi wa ngazi za juu muangalie chama cha moira mkoa wa Kigoma kwa jicho pevu.Viongozi,marefa wanapokea rushwa waziwazi bila kuogopa hata kasi ya Magufuli.Refa maarufu kwa kupokea rushwa ni RAMBO huyu makocha wanamjua kama mi mlevi sana,ukimpata tu 5000 basi NYEUPE atakwambia ni NYEUSI (Nina ushahidi)
VIONGOZI WA TFF MKIKAA KIMYA BASI MTASHUHUDIA MAKUU AU KUSIKIA MAKUU WAKITENDEWA HAWA VIONGOZI WA MICHEZO MKOA.