Fahamu namna ya kupika matembele

Fahamu namna ya kupika matembele

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
Miongoni mwa mboga za majani ninazopenda ni pamoja na tembele, leo ngoja niwashirikishe jinsi ya kuyapika matembele.

Pishi hili ni kwa wale wenye Maisha ya kawaida kabisa ambao tunapika bila vipimo (tunakadiria lakini msosi unakuwa mtamu balaa).

1590669958680.png

Mahitaji:
  • Matembele mafungu mawili ( hapa inategemea na mahitaji)
  • Nyanya tatu
  • Kitunguu cha wastani kimoja
  • Kariti moja( sio lazima sana)
  • Hoho( ukipenda sio lazima sana)
  • Mafuta kiasi
  • Chumvi kiasi
Jinsi ya kutayarisha.
  • Chukua matembele yako yachambue vizuri kutoa vinyuzi kwenye mikia yake kwa kuvunja mkia wake na kuvuta kile kivyuzi kwa kuwa huwa yanakua magumu kama usipotoa.
  • Waweza kuyaweka juani yanyauke kidogo kama ukipenda sio lazima sana(mimi hupendelea yaliyonyauka)
  • Yasafishe vizuri matembele yako, kisha andaa viungo vyako kwa kuanza upishi.
Kupika.
  • Weka mafuta kiasi cha vijiko viwili kwenye sufuria na weka jikoni( hapa inategemea na wingi wa mboga uliyonayo)
  • Mafuta yakipata moto weka vitunguu na kanga mpaka view kahawia.
  • Weka nyanya zako ulizokatakata na kanga kisha weka karoti kanga kisha weka hoho kama unayo kaanga mpaka mchanganyiko uwe sawa.
  • Weka chumvi na uendelee kukaanga mpaka mchanganyiko uwe sawa na uive ila usitumie muda mrefu ili usije kukauka.
  • Weka matembele yako geuza geuza na kisha ufunike.
  • Tumia dakika tano mpaka saba kisha funua na geuza kisha onja chumvi na kama iko sawa epua ili mboga isiive sana kutunza vitamini vyake.
Waweza kula na ugali au chochote kile upendacho.

 
Naipenda mboga pia, ila kuwe na dagaa au samaki pembeni, Kuna matembele makavu yanachanganywa na dagaa na karanga alooo kwa wali tamu sana, Nimekumbuka nyumbani ghafla,
[emoji39][emoji1786]
 
Ila na wewe sio kwa karoti hizo, imekua kama majani yaliyoota maua.
[emoji2960][emoji2960]
 
Mkuu umesahau kandimu au limao.tembele liwe na dagaa au samaki wakavu(kukaanga) pembeni,kilo ya ugali haitoshi kwa mtu mmoja kama mimi.
 
Matembele, majani ya maboga ni mboga nazopenda sana na kupika mara kwa mara.
Kuna mboga inaitwa "mashasha" sijui mashona nguo nilikula juzi kwa mara ya kwanza aiseeee tamu sana nayo.
Nitajifunza mapishi yake.
 
Back
Top Bottom