Fahamu zaidi kuhusu P.I.D, dalili na madhara yake

Fahamu zaidi kuhusu P.I.D, dalili na madhara yake

Eng Kizumango

Member
Joined
Mar 17, 2021
Posts
27
Reaction score
7
P.I.D- Pelvic Inflammatory Disease.

P.I.D Ni maambukizi kwenye via vya uzazi kwa mwanamke ambayo huusisha maambukizi kwenye shingo ya kizazi(CERVICITIS),nyama kwenye mfumo wa wa uzazi(ENDOMETRITIS) na mirija ya uzazi(SALPINGITIS).

Kuna aina mbili ambayo ni chanzo cha maambukizi ya ugonjwa wa P.I.D ni NEISSERIA GONORNOAE na CHLAMYDIA TRACHOMATIC

WANAMKE ANAUPATAJE UGONJWA WA P.I.D
  • Kupitia ngono zembe
  • Kuwa na mpenzi zaidi ya mmoja
  • Kufanya mapenzi bila kutumia kinga
  • Kupitia magonjwa ya zinaa hususani kaswande na kisonono
  • Kupitia kunyonywa ukeni mara kwa mara
  • Utoaji wa mimba na kutosafishwa vizuri baada ya kutoa mimba
  • Kuweka vitu ukeni ili kuufanye uke ubane au kumvutia mpenzi wako
  • Kutumia dawa na njia za kuzuia mimba(vijiti na sindano)
  • Kuwa na U.T.I. sugu au fungus ya muda mrefu

DALILI ZA P.I.D
  • Kutokwa na uchafu mzito sehemu za siri yaweza ukawa njano, mweupe au maziwa
  • Uke kutoa harufu mbaya
  • Kuwashwa sehemu za siri
  • Maumivu ya tumbo chini ya kitovu
  • Uke kuwa mlaini sana
  • Maumivu wakati wa tendo la ndoa
  • Kuvurugika kwa hedhi
  • Kutokwa na maji maji ukeni kupita kiasi
  • Maumivu wakati wa kukojoa
  • Homa, uchovu na kizunguzungu

MADHARA YA P.I.D
  • Maumivu ya tumbo au nyonga ya mara kwa mara mara baada ya tendo la ndoa. au kipindi cha upevushaji mayai hali hii hutokana na majeraha yaliyopi katika mirija ya uzazi
  • Kusababisha majeraha ndani na nje ya mirija za uzazi ambayo hipelekea mirija kuziba
  • Kubeba mimba nje ya kizazi husababishwa yai kushindwa kufika kwenywe mji wa uzazi kupitia mirija ya uzazi
  • Ugumba kwa mwanamke
  • kupata kansa ya shingo ya uzazi

JINSI YA KUEPUKANA NA P.I.D

Japo kuwepo na tiba za kujitibu lakini unashauriwa kinga ni bore kuliko tiba hivyo zingatia yafuatayo;-
  • Epuka kufanya ngono zembe
  • Usifanye mapenzi baada ya kujifungua au mimba kutoka
  • Weka tabia ya kufanya vipimo mara kwa mara
  • Kuwa msafi na nguo zako za ndani na kula lishe bora
  • Epuka kushare nguo za ndani

UNAPOONA DALILI ZA UGONJWA HUU WAHI KUPATA MATIBABU. KWANI UGONJWA HUU NI HATARI NA HUWEZA KUKUSABABISHIA UGUMBA AU KANSA YA SHINGO YA KIZAZI

Ugonjwa wa P.I.D unatibika vizuri kabisa hivy bas kama upo tayari unaumwa na umezunguka hospitalini bila mafanikio bas wasiliana nasi kwa msaada zaidi
 
Hii kitu katika wanawake 100 nadhani ni wawili tu ndio hawana hizi dalili kwa sasa. Naona wengi wao huwa wanalalamika hizi dalili kuwa nazo.

Duh sasa hii si ni hatari sana, maana serikali wapo busy kutangaza vitu artificial kama Coronavirus ila wanaacha kutangaza vita na maradhi ambayo yanashambulia miili ya wanawake zetu na kuja waacha na majanga ya kudumu kama magonjwa ya figo na kukosa uzazi.
 
Je ukila iyo manzi haikupati iyo kitu
 
P.I.D- Pelvic Inflammatory Disease.

P.I.D Ni maambukizi kwenye via vya uzazi kwa mwanamke ambayo huusisha maambukizi kwenye shingo ya kizazi(CERVICITIS),nyama kwenye mfumo wa wa uzazi(ENDOMETRITIS) na mirija ya uzazi(SALPINGITIS)...
Hi nahitaji nna shida kuhusiana n pid,naomba kuwasiliana n wewe tfdhli🙏
 
Back
Top Bottom