Faida na tahadhari za mboga za spinach kwa afya

Faida na tahadhari za mboga za spinach kwa afya

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2021
Posts
577
Reaction score
2,595
Spinach ni mboga yenye faida nyingi kwa afya ya binadamu. Baadhi ya virutubusho vinavyopatikana kwenye mboga hii husaidia mwili kusafirisha vizuri hewa ya Oxygen, kutoa kinga dhidi ya magonjwa, kuongeza uzalishwaji wa damu pamoja na kuboresha afya ya macho, ngozi, nywele na mifupa.

6DAB681F-C477-42C4-B398-7048AD66E57A.jpeg

Pamoja na uwepo wa faida lukuki zitokanazo na mboga hii, watu wenye changamoto ya ugonjwa wa figo huwa hawashauriwi kuitumia kwa kiasi kikubwa kwa kuwa huwa na wingi wa chumvi za Oxalate ambazo husababisha kutengenezwa kwa mawe kwenye ogani (organ) hizo.

Aidha, watu wenye tatizo la kuganda kwa damu kwenye mishipa hushauriwa kupata kwanza ushauri wa daktari kwani mboga hii huwa na kiasi kingi cha vitamini K ambayo huathiri utendaji kazi wa dawa zao, pamoja na kuongeza ukubwa wa tatizo hivyo kuhatarisha zaidi afya.

Chanzo: Medical News Today
 
Asante kwa ushauri mzuri tumeuchukua tutauchunguza kama una ukweli ndani yake.
 
Spinach ni mboga yenye faida nyingi kwa afya ya binadamu. Baadhi ya virutubusho vinavyopatikana kwenye mboga hii husaidia mwili kusafirisha vizuri hewa ya Oxygen, kutoa kinga dhidi ya magonjwa, kuongeza uzalishwaji wa damu pamoja na kuboresha afya ya macho, ngozi, nywele na mifupa.

View attachment 2473662

Pamoja na uwepo wa faida lukuki zitokanazo na mboga hii, watu wenye changamoto ya ugonjwa wa figo huwa hawashauriwi kuitumia kwa kiasi kikubwa kwa kuwa huwa na wingi wa chumvi za Oxalate ambazo husababisha kutengenezwa kwa mawe kwenye ogani (organ) hizo.

Aidha, watu wenye tatizo la kuganda kwa damu kwenye mishipa hushauriwa kupata kwanza ushauri wa daktari kwani mboga hii huwa na kiasi kingi cha vitamini K ambayo huathiri utendaji kazi wa dawa zao, pamoja na kuongeza ukubwa wa tatizo hivyo kuhatarisha zaidi afya.

Chanzo: Medical News Today
Spinach ni asidi haifai kuliwa na binadamu madhara yake ni makubw akuliko daida zake.

Dr Sebi: Why No Spinach, No Tofu, No Carrot​

 
MORINGA, MILK, CARROTS, SPINACH - LISTEN CAREFULLY TO Dr. SEBI WARNING
MLONGE,MAZIWA YA NG'OMBE,KAROTI NA MCHICHA NI ASIDI HAZIFAI KULIWA KILA SIKU ZINA MADHARA KWA BINADAMU

 
hii ni moja ya mboga ambayo sio salama kwa sasa kwa kuwa walaji wanaipenda sana na kuchangia kwa wakulima wengi kupunguza uaminifu katika zao hili.
wengi wanatumia mbolea za viwandani na madawa ili itoke ikiwa na majani mazuri.
ukiweza hakikisha unanunua spinachi iliyoliwa na wadudu kwakuwa mdudu hali sumu. japo nilimwambia muuzaji mmoja akadai kwa utani ataanza kuzitoboa na punch.
ndio maana tunashauriwa eneo la kujenga lisizidi asilimia 40 ili vitu kama mbogamboga viwepo nyumbani mwako vikiwa na usimamizi mzuri.
 
Back
Top Bottom