Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 76,107
- 160,001
Matembele ni mboga maarufu sana, pia ni mboga yenye virutubisho sana,
Lakini matembele yana faida nyingi katika miili yetu.
FAIDA ZA MBOGA YA MATEMBELE KWA UFUPI
1: Matembele yana madini ya chuma. Madini haya ndiyo muhimu katika utengenezaji wa damu, kwa hiyo mtu anapotumia matembele anakuwa anaongeza kiwango cha damu mwilini. Watu wenye upungufu wa damu na kina mama wajawazito wanashauriwa kula matembele kwa wingi.
2: Matembele yana vitamini A ambayo husaidia kuimarisha macho na hivyo kumsaidia mtu kuona vizuri hasa hasa nyakati za usiku.
3: Matembele yana vitamini C Ambayo humlinda mtu asipate kiseyenye (scurvy). Vitamini C huimarisha ngozi na fizi, unapotumia matembele fizi zako na ngozi huimarika na huzuia kuvuja damu kutoka kwenye fizi.
4: Matembele yana protini ambayo husaidia katika kuimarisha misuli na kusaidia katika ukuaji wa mwili. Wape watoto matembele ili wakue vizuri.
5: Matembele yanasaidia kuongeza damu kwa wingi mwilini ikiwa utayachemsha na kula na maji yake kila siku
6: Matembele yanasaidia kuongeza nuru na kuboresha Afys ya macho
7: Matembe yanasafisha damu na kutoa mafuta machafu
8: Kamba lishe zilizo kwenye matembele ni chanzo cha kupata choo kikubwa vizuri
Kwani zinaboresha mfumo wa usagaji ( digestion)
MATAYARISHO
ILI UPATE FAIDA HIZI NI BORA UKAWA UNACHEMSHA MATEMBELE YENYEWE TUU UKAWEKA NYANYA NA VITUNGU NA CHUMVI KWA MBALI
UKATUMIA BAKULI KUBWA MOJA KILA SIKU
ANGALIZO
KWA MTU MWENYE VIDONDA VYA TUMBO HAYAMFAI AU GESI NYINGI
Lakini matembele yana faida nyingi katika miili yetu.
FAIDA ZA MBOGA YA MATEMBELE KWA UFUPI
1: Matembele yana madini ya chuma. Madini haya ndiyo muhimu katika utengenezaji wa damu, kwa hiyo mtu anapotumia matembele anakuwa anaongeza kiwango cha damu mwilini. Watu wenye upungufu wa damu na kina mama wajawazito wanashauriwa kula matembele kwa wingi.
2: Matembele yana vitamini A ambayo husaidia kuimarisha macho na hivyo kumsaidia mtu kuona vizuri hasa hasa nyakati za usiku.
3: Matembele yana vitamini C Ambayo humlinda mtu asipate kiseyenye (scurvy). Vitamini C huimarisha ngozi na fizi, unapotumia matembele fizi zako na ngozi huimarika na huzuia kuvuja damu kutoka kwenye fizi.
4: Matembele yana protini ambayo husaidia katika kuimarisha misuli na kusaidia katika ukuaji wa mwili. Wape watoto matembele ili wakue vizuri.
5: Matembele yanasaidia kuongeza damu kwa wingi mwilini ikiwa utayachemsha na kula na maji yake kila siku
6: Matembele yanasaidia kuongeza nuru na kuboresha Afys ya macho
7: Matembe yanasafisha damu na kutoa mafuta machafu
8: Kamba lishe zilizo kwenye matembele ni chanzo cha kupata choo kikubwa vizuri
Kwani zinaboresha mfumo wa usagaji ( digestion)
MATAYARISHO
ILI UPATE FAIDA HIZI NI BORA UKAWA UNACHEMSHA MATEMBELE YENYEWE TUU UKAWEKA NYANYA NA VITUNGU NA CHUMVI KWA MBALI
UKATUMIA BAKULI KUBWA MOJA KILA SIKU
ANGALIZO
KWA MTU MWENYE VIDONDA VYA TUMBO HAYAMFAI AU GESI NYINGI


