Faida za kumiliki hisa za Vodacom

PIA HAWA WANAHISA ZA KAWAIDA WANAPATA HAKI YA KUSHIRIKI VIKAO VYA WANAHISA NA KUPIGA KURA ILHAL PREFERED SHAREHOLDER HAWANA HAKI YA KUPIGA KURA KWENYE VIKAO
 
Mkuu inaonyesha una uelewa mkubwa na mambo ya hisa, kwa faida ya wengi hebu tupe tofauti ya ORDINARY na PREFERENCE shares, Faida na hasara ya kila moja pamoja na gharama za kila moja(Kama zinatofautiana).
kuna mdau kaelezea vizuri,fatilia page ya nne utaona alivyochambua hili suala ila kwa bei Ordinary shares ni bei chee sana ambazo kila mtu anaeeza kuzimiliki hata mtu wa kipato cha chini lakin Preferencial shares zenyew ziko bei juu ndio maana hata kweny makampuni mengi makubwa unaeza kuta mtu anahisa 4% ,mwingine 44% ambapo hisa moja tu utakuta ni bilions of money lakini ukiwaangalia unakuta n watu weny vipato vyao so huo ndio unakua mfano mzuri wa preference shares
 
Bado hujanielezea nikaridhika...
 
Wakuu samahani naomba kujua zaidi kuhusu hii offer ya kununua hisa na vodacom....... Naomba u shee chochote unachokijua kuhusu hii offer..... Kwa mfano what should i expect nikinunua hisa 100 zenye thamani ya tsh 85k na mengine karibuni
EXPECT GAWIO KULINGANA NA HISA 100 UTAKAZOZINUNUA KAMA KAMPUNI IKIPATA FAIDA NA IKAAMUA KUWAGAWIA KAMA GAWIO PIA EXPECT KUPEWA "0" KAMA GAWIO ENDAPO KAMPUNI ITAPATA HASARA PIA UKIONA HII NI BIASHARA KICHAA UNAWEZA PIA KUZIUZA HISA ZAKO KULINGANA NA BEI ITAKAYOKUA SOKONI KWA WAKATI HUSIKA KAMA ITAKUA 850 AU 500 AU 1500 KWA HISA,NAPO PIA UKIKUTA BEI IKO CHINI YA ULIONUNULIA BAS EXPECT HASARA NA PIA UKIKUTA BEI IKO JUU ZAID YA ULIONUNULIA EXPECT FAIDA KWENYE HICHO KILICHOZIDI.
 
Baadaa ya kukutana na mabandiko mengi sasa nimeshawishika kuwekeza na Vodacom.

Kuna Sera ya Gawio la Hisa kila kampuni inapopata faida wateja wa Hisa tunapata gawio ambalo hutolewa katika asilimia 50 ya faida hugawanya kwa wamiliki baada ya sisi wamiliki wa Hisa kufikiana makubaliano ya pamoja na wamiliki wa hisa na kila gawio litatolewa kulingana na idadi ya Hisa unazozimiliki.

Unatakiwa ufahamu ukimiliki hisa unahesabika kama wewe ni mmoja wa wamiliki wa kampuni hivyo basi pale kampuni inapopata faida kuna gawio ambalo unapata kulingana na idadi ya Hisa zako.

Kwa mfano Kampuni ya Vodacom ikitangaza inagawa gawio la sh. 20 Kwa kila hisa moja kila mtu atapata shilingi 20 kulingana idadi ya hisa zake.

Lakini kumbuka gawio sio lazima kupatikana kila mwaka, Kwa upande wa Vodacom imewekeza zaidi ya shilingi bilioni 660 kutanua matumizi ya mtandao Kwa kipindi cha miaka mitatu hivyo hapa tunaweza kuona kwamba gawio litapatikana kila mwaka kutokana na kampuni imejitanua na kujiimarisha vya kutosha.

Zipo kampuni nyingine za mawasiliano ambazo ni Changa hazipati faida ama ipo kwenye kujitanua hivyo kila Faida inayopatikana itawekwa kwenye kwenye kupanua kampuni.

Vodacom inatoa huduma zake nchini Kwa zaidi ya miaka 17 ni inaaminika Kwa uweledi na ufanisi wa kazi zake na hapa ndipo Faida ilipo kuwa utanunua hisa kwenye mikono salama.

Sasa nimewekeza katika Hisa za Vodacom
 
•Unalalamika sana kuhusu mshahara hautoshi bali kuna njia rahisi ya kutengeneza pesa chukua kalamu na Karatasi nikueleze kuhusu Hisa za Vodacom.

Mwaka huu kampuni ya Voda inauza share zake kwa shilingi 850 kwa kipande tu na watu wengi bado hawajasanuka kuhusiana na dili hii.

Kwa Mfano kazini unapata mshahara wa laki 5 (500,000) unaweza kufunga roho na kununua vipande 500 Kwa 425,000 tu. Thamani ya kipande inaweza kupanda maradufu na kukuletea faida ambayo usingeweza kuipata kama ungewekeza hiyo hela sehemu nyingine
Thamani ya Hisa huongezeka kila wakati soko la Vodacom ni la uhakika

Chukulia mfano umenunua vipande 500 leo kwa shilingi 850 tu mwakani vipande vya hisa vikapanda bei na kuuzwa shilingi 2000, ongezeko la shilingi 1150 ambazo kama unaamua kuuza hisa zako kwa shilingi 2000 leo hii ungekuwa na kitu kama milioni moja (1,000,000). Kupanda kwa bei ya hisa kunaongeza utajiri wako kama utaamua kununua na kuuza hisa zako baada ya kipindi cha muda fulani.

Pesa ambazo zingetosha kabisa kununua nyumba Masaki na Gari la ndoto yako

Jifunze kukataa kulalamika nenda kanunue Hisa za Vodacom kwa shilingi 850 tu then matokeo yake utayapa!
 

Maisha yangekua rahisi hivi kila mtu angekua tajiri. Amna kitu kama icho kabisa.
 

Hivi hizo preference shares za vodacom zinauzwa kiasi gani sasa hivi?
 
kiwango cha chini cha kununua ni hisa 100
 
Ni utaratibu upi unatumika kumuelewesha mtu wa kawaida kuwa kampuni imepata hasara!??
 
Ni utaratibu upi unatumika kumuelewesha mtu wa kawaida kuwa kampuni imepata hasara!??
Kila kampuni ambayo ni public yaanio inauza shares inabidi itoe financial statements zake hadharani huo ndo utaratibu.
 
Kwa ninavyoona TZ sasa hivi kununua shares ukitegemea kupata dividends haileti maana, kwa sababu hela hizo hizo ukiziweka fixed deposit utapata faida kubwa zaidi na huko hakuna riosk ya kupoteza principle unless benki ife.
Pia Voda hawajaahidi dividends yoyote, ninachoona ni kuwa wanasema "watajitahidi" 50% ya profits igawiwe kama dividends.

Vodacom wanauza shares zaidi ya millioni 500 so kuna maswali kama kutakuwa na lile ongezeko la thamani katika IPO kama lililotokea DSE walipouza shares.

Growth ya Vodacom itatoka wapi? Teyari ni namba moja Tanzania na kuna ushindani mkubwa sana, kweli wataweza kupanua soko? Bila growth hakuna sababu ya kuamini kuwa shares zao zitakua thamani.

Mwisho hawa Vodacom wamelazimishwa kuuza shares kwa hiyo uhusiano wao na shareholders sijui utakuwaje.
 
Huwezi kuwa tajiri kama huna nidhamu nzuri ya kutumia hela yako vizuri.

Na ulichokiongea hapo ni kauli za vijiweni wakati wa kunywa kahawa.
Mpe Tsh.200, Aongeze kahawa kashata nakuja kulipia..Ucpate shida kumwelimisha asiyetaka kuelewa ndugu.
[HASHTAG]#wachamambo[/HASHTAG] yavijiwevyakahawakwenyemamboyamsingi.
 
Well said mkuu....
 
Reactions: efn
Ukitaka kununua hisa lazima uwasiliane na brokers, ndio hao wataalamu wenyewe.
Brokers ni mawakala ambao wanapata commission baada ya kuuza shares kwahiyo ushauri wao utakua wa upande mmoja ambao unawanufaisha wao.
 
Hizo hisa za voda ni individual pekee au mpaka vikundi vinaweza faidika?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…