faida za maji ya bahari ni zipi kiafya n.k

PesaNdogo

JF-Expert Member
Joined
Jun 19, 2013
Posts
1,994
Reaction score
1,291
Habari zenu, nliwahi kusikia watu wakiongea kwamba maji ya bahari yana faida kiafya ukiogelea na pia Nimeona watu wakihangaika kuchota na vibubu vyao. Je kuna matumizi yake spesho?
 
Habari zenu, nliwahi kusikia watu wakiongea kwamba maji ya bahari yana faida kiafya ukiogelea na pia Nimeona watu wakihangaika kuchota na vibubu vyao. Je kuna matumizi yake spesho?

[h=1]Qur-aan Inavyoeleza Juu ya Bahari na Mito[/h]
Wanasayansi wa zama hizi wamegundua kuwa mahali ambapo bahari mbili tofauti hukutana, kuna kizuizi baina yake. Kizuizi hiki huzigawa bahari mbili hizo kiasi kwamba kila bahari huwa na joto lake, kiwango cha chumvi na msongamano.[21] Kwa mfano, maji ya bahari ya Mediterranean ni yenye uvuguvugu, yana chumvi na msongamano mdogo yakilinganishwa na maji ya bahari ya Atlantiki. Pindi maji ya Mediterranean yaingiapo Atlantiki katika kizingiti cha Gibraltar, huingia mamia kadhaa ya kilomita ndani ya Atlantiki katika kina cha kadiri ya mita 1000 yakiwa pamoja na sifa zake za uvuguvugu, kiwango uchumvi na uchache wa msongamano. Maji ya Mediterranean huimarika katika kina hiki [22] (angalia mchoro namba 13)



Umbo namba 13: Maji ya bahari ya Mediterranean yanavyoingia Atlantiki kupitia kizingiti cha Gibraltar yakiwa na sifa yake ya uvuguvugu, uchumvi na msongamano, kwa sababu ya kizuizi kinachoyatofautisha. Kipimo cha joto ni katika nyuzi joto za Selisiasi (S[SUP]o). (Marine Geology, Kunen, uk. 43, kukiwa na kuweka nyongeza kidogo)[/SUP]
[SUP]
[/SUP][SUP]Ingawa kuna mawimbi makubwa, mikondo yenye nguvu na kupwa na kujaa katika bahari hizi, hazichanganyiki wala kuvuka kizuizi hiki.[/SUP][SUP]Qur-aan ilieleza kuwa kuna kizuizi baina ya bahari mbili, hazichupi mipaka. Allaah amesema: "Anaziendesha bahari mbili zikutane; Baina yao kipo kizuizi, zisiingiliane." (Qur-aan, 55:19-20)[/SUP][SUP]Lakini pindi Qur-aan inapozungumzia kigawanyi baina ya maji baridi na ya chumvi, hutaja kuwepo kwa "kitenganishi kizuiacho" na kizuizi pamwe. "Naye Ndiye Aliyezipeleka bahari mbili, hii tamu mno, na hii ya chumvi chungu. Na akaweka baina yao kinga na kizuizi kizuiacho." (Qur-aan, 25:53)[/SUP][SUP]Mtu anaweza kuuliza, kwa nini Qur-aan imetaja kitenganishi pindi izungumziapo chenye kugawanya baina ya maji baridi na ya chumvi, lakini haikukitaja wakati inapozungumzia juu ya chenye kugawanya kati ya bahari hizi mbili?[/SUP][SUP]Sayansi ya zama hizi imegundua kuwa katika milango wa mto ambapo maji baridi (matamu) na maji chumvi hukutana, hali kwa namna fulani ni tofauti na kinachopatikana mahali ambapo bahari mbili hukutana. Imegundulika kwamba kinachotofautisha maji baridi na maji baridi katika milango bahari ni "ukanda wa pycnocline kukiwa na alama ya kutokukuwepo muendelezo wa msongamano unaotenganisha baina ya tabaka mbili."[23] Kitenganishi hiki (ukanda wa utengano) una uchumvi ulio tofauti na maji baridi na maji chumvi[24](angalia umbo namba 14).[/SUP]

[SUP]
[/SUP]
[SUP]
[/SUP][SUP]Umbo namba 14: Sehemu iliyokatwa kwa urefu ikionesha uchumvi (semu moja kati ya elfu [SUP]0[/SUP]/[SUB]00[/SUB]katika mlango bahari. Hapa tunaweza kuona kitenganishi (ukanda wa utengano) baina ya maji baridi na ya chumvi. (Introductory Oceanography, Thurman, uk. 301, kukiwa na nyongeza kidogo)
[/SUP]
[SUP]Maelezo haya yamegundulika hivi karibuni tu, kwa kutumia vifaa vilivyoendelea sana kwa kupima joto, uchumvi, msongamano na kuyeyuka kwa oksijeni, n.k. Jicho la mwanaadamu haliwezi kuona tofauti iliyopo baina ya bahari mbili zenye kukutana. Halikadhalika, jicho la mwanaadamu haliwezi kuona mgawanyo wa maji katika milango bahari katika namna tatu: maji baridi, maji chumvi, na kitenganishi (ukanda wa utengano).[/SUP]



 
maji ya Bahari ni dawa kila maradhi wewe kama upo Dares-Salaam fanya kila mwezi uwe unakwenda kuogelea baharini hata mikosi mikosi ya mwilini mwako itakuondokea ukioga maji ya bahari yana siri kubwa sana hata waganga wa kienyeji wanayatumia maji ya bahari.
 
asante kwa maelekezo @MziziMkavu@
kwa hiyo to be specific maradhi ya mwilini yanayoweza kushughuliwa na maji ya baharini ni yap?
 
asante kwa maelekezo MziziMkavu
kwa hiyo to be specific maradhi ya mwilini yanayoweza kushughuliwa na maji ya baharini ni yap?
Maradhi ya ngozi ukiwa nayo wewe kaoge maji ya bahari maradhi mengine ni siri yangu sio kila kitu ninaweza kukiweka hapa mkuu samahani.
 
Maradhi ya ngozi ukiwa nayo wewe kaoge maji ya bahari maradhi mengine ni siri yangu sio kila kitu ninaweza kukiweka hapa mkuu samahani.
Sasa mkuu kwa nini ufanye siri mkuu, tufumbue macho na sisi tupone mkuu

Au hata kwa njia ya PM tu mkuu
 
MziziMkavu asante kwa somo;
Naomba tu hayo maradhi ya siri yako ili tushare.
 
Last edited by a moderator:
da mi nilishangaa siku kulitokea mafuriko dar pale daraja la sarenda maji ya mvua yalikuwa yakiingia baharini yanarudishwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…