Faida za pilipili kichaa kiafya

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Pilipili kichaa inaweza kustawi sehemu mbalimbali na inahitaji siku 100 za ukuwaji.
Hustawi zaidi kwenye mazingira ya joto na unyevunyevu.Mmea huu hukua kufikia urefu wa futi mbili hadi nne.

Ina wingi wa
vitamini A
pia ina vitamini B,
vitamini E,
vitamini C,
Riboflavin,
Potassium,
Manganese.

- Jamii nyingi hususa Marekani na bara la Asia wana historia ya kutumia pilipili kichaa kama tiba.

Ni dawa yenye nguvu sana na matumizi mengi,
hutumika sana kwa kusafisha damu na
kutoa sumu mwilini,
pia hutumika kusisimua mzunguko wa damu na
kuweka sawa uwiano wa tindikali(acid)mwilini.

Pilipili kichaa imetumika kwa maradhi tofauti tofauti ikiwemo moyo,
gauts,
kupooza
homa,
kikohozi,
tonsilatis,
kichefuchefu
hemorhoids

kwa miaka mingi huko Asia na mashariki ya mbali.

MAAJABU YA PILIPILI KICHAA;
1. Kutibu kidonda-
Hii inaweza kuwa ni ajabu kwa walio wengi lakini ni tiba liyothibitishwa na imekuwa ikitumika miaka kadhaa iliyopita katika nchi mbalimbali.Sio tu kuzuia kutokwa na damu katika kidonda cha kujikata kama ilivyozoea kutumiwa na wengi huko majumbani kwa miaka mingi bali pia huzuia fangasi na bakteria kuingia katika uwazi wa kidonda hicho hutumika pia kuondoa sumu mwilini

2.Hufanya mwili kuweza kutumia vyema virutubisho vipatikanavyo kutokana na chakula

3.Husaidia uyeyushaji wa mafuta mwilini/Kuchoma mafuta

4.Pilipili ina antioxidants muhimu kama beta carotene,ina wingi wa vitamini A,C na K hebu tuziangalie vitamini hizo: a.Vitamini A husaidia kuweka sawa kinga ya mwili pia hutukinga na kansa na magonjwa ya moyob.Kazi ya vitamini C-ni kuzuia strock,magonjwa ya moyo,macho na kansa mbalimbali.

Miili ya binadamu haiwezi kujitengenezea vitamini C,hivyo basi tunaweza kupata vitamini C kupitia chakula.c.Vitamini K-Husaidia katika ukuwaji wa mifupa,pia ni muhimu katika mzunguko wa damu.Pilipili zote huwa na Capsaicin ambayo kazi yake ni kupunguza maumivu,kuzuia kansa na magonjwa ya moyo.

5.Inasaidia sana kusawazisha sukari kwenye damu

6.Huwasaidia watu wanene(over weight) au wanaougua ugonjwa wa kisukari.Hii ni kwa mujibu wa watafiti katika chuo kikuu cha Tasmania uliochapishwa katika American Joarnal of Clinical Neutition mwezi julai 2006.

7.Inasaidia kwa kiasi kikubwa kudhibiti kwa kiasi kikubwa INSULIN kwa 60% baada ya kula chakula

8.Husaidia kupunguza maumivu na uvimbe kwenye tezi na vilevile huwasaidia wagonjwa wa RHEMATOID na ARTHRITIS kupata nafuu

9.Husaidia kuondoa mkusanyiko wa damu sehemu moja mwilini

10.Husaidia kufungua kwa haraka na kwa ufanisi pua zilizoziba kwa mafua na kukufanya upumue kwa urahisi.

11.Husaidia kupunguza uwezekano wa kupatwa na saratani ya utumbo.

12.Husaidia kuongezeka kiwango cha METABOLIC ambayo husaidia kuchoma mafuta

13.Husaidia kuongezeka kwa kiwango cha METABOLIC kwa 23% ndani ya masaa matatu.

14.Husaidia kupunguza cholestro na kupunguza kiasi cha fibrin katika damu.


Chanzo: masengwa blog
 
Naweza fanya yoooote ila hilo la kuweka PILIPILI kichaa kwenye kidonda kibichiiii aseee niache kidogo
 
Asante sana itabidi nianze kuzitafuta.
 
Vipi kuhusu kuongeza nguvu za kiume?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jaman acheni quote Uzi mrefu huu..tchaa!
 
PILIPILI KICHAA NIMOJA YA TIBA KTK SUALA LA TENDO LANDOA ,,YAAN INASAIDIA KUUFANYA UUME KUSIMAMA HARAKA HARAKA NA WENYE NGUVU ......
 
Miss zomboko kwenye kuweka pilipili kichaa kwenye kidonda kibichi mmm!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…