Chief Ortambo Ikumenye
JF-Expert Member
- Nov 16, 2017
- 247
- 503
Watu watajiuliza hii ninayoiita ‘Law of Pressure’ ni kitu gani?
Kisayansi, unapokutana na maada (Matter) mfano wa lijiwe likubwa na ukatakiwa uweze kulitawanyisha vipande vipande, huwa ni kazi ngumu sana ikiwa ulichonacho mkononi ni nyundo ndogo tu.
Kwa tafsiri ya picha, CCM inawakilisha hilo jiwe kubwa ambalo limejiimarisha kwenye siasa za Tanzania na wameweza kukita mizizi yao kwenye serikali na vyombo vya dola (yaani inakuwa ni ngumu sana kutenganisa hivo vitu vitatu). Hii imekuwa ikiwapa faida kwenye chaguzi za kufanya chochote wakitakacho kujihakikisha ushindi (hata hizi chaguzi zinazokuja karibuni, sitegemei mabadiliko yeyote suala la CCM kushinda, hata CHADEMA hilo wanalielewa). Halafu sasa huyo mtu mwenye kinyundo kidogo naichukulia kama ndo chama cha CHADEMA, wao wanajua kabisa kwamba ni ngumu sana kuisambaratisha CCM, ‘lakini sio kwamba ni jambo lisilowezekana’.
Kwa mbinu za kisayansi, jiwe hilo linaweza kuvunjwa na kusambaratishwa endapo likiwa subjected to pressure, japo sio investment ya miaka miwili au mitatu, yaweza kuchukua muda mrefu, lakini pia yaweza kuchukua muda mfupi kulingana na mazingira na reaction mbali mbali wakati pressure ikiwa applied.
Kwa mtu mwenye nyundo, applying pressure kwenye jiwe kama hilo, maana yake ni kuanza kulikagua sehemu zenye muonekano wa kuwa dhaifu (Vulnerable areas) kama vile nyufa n.k, kisha sasa ku apply constant pressure kwenye kila sehemu ambayo ni dhaifu. Na namna ya ku apply pressure maana yake ni kuanza kuligonga hilo jiwe kila siku sehemu zote zenye ufa. Zoezi hili linahitaji determination and discpline, kwamba, unawezaje kuamka kila siku asubuhi kuligonga lijiwe likubwa kwa kutumia kanyundo kadogo? Swali hilo ndo linatupeleka kujibu lile swali la ‘Ni kwanini ni CHADEMA tu inayotamkwa kila siku kwenye midomo ya watu miaka nenda rudi angali kuna vyama vya upinzani zaidi ya 16?’ Jibu lake pia lipo kwamba, labda ni chama pekee kinachoamini kwamba jiwe linaweza kuvunjwa endapo kama ukiwa determined na discpline ya ku apply pressure kila siku bila kujali kama jiwe linavunjika ama halivunjiki.
Matokeo ya Ku apply Constant Pressure kwenye Jiwe
Guaranteed, kutakuwa na tofauti kwenye jiwe ikiwa litagongwa mara elfu moja (1000) na tofauti itazidi kuonekana mgongaji akizidi kugonga. Kuna nyufa ambazo zitaanza kuongezeka na kujiachia au jiwe litaanza kujimega kidogo kidogo. Kwenye hii process, naona kabisa mgongaji akijikusanyia faida tatu kadri anavyoligoga jiwe;
CHADEMA na Law of Pressure
Hichi ndicho wamekuwa wakikifanya CHADEMA kwa miaka 15 iliyopita na wanaendelea kukifanya mpaka sasa. Kutafuta vulnerabilities kwenye mfumo wa dola wa CCM na kutengeneza ‘Narratives’ za kuanza ku ‘attack’ mfumo.
Mambo kama maandamano madogo madogo, kampeni za hapa na pale, kudai katiba mpya etc etc zimekuwa nyingi sana kwa CHADEMA
Mimi najua kabisa hata ndani ya CHADEMA watakuwa wanajua kabisa ya kwamba, maandamano kwa set up ya nchi hii hayafui dafu, lakini wao wamekuwa wakiyafanya anyway kwasababu wanajua kabisa kupitia maandamano kuna cheche na counteractions lazima zitokee. Unamsikia leo Msemaji wa Jeshi la Polisi ametia mguu, kuyaita kwamba maandamano yaliyopangwa ni batili, maana yake ni kwamba, CHADEMA ninayoijua mimi, hii kwao pia ni ushindi mkubwa, kwasababu unaona kabisa either kuna possibility ya mtifuano kati ya CHADEMA na POLISI au POLISI wakubali kuyaruhusu off which ni ushindi kwa CHADEMA ukizingatia kauli mbiu ya maandamano yenyewe ‘SAMIA MUST GO’ nayo imekaa pabaya sana kwa serikali na CCM ukizingatia kwamba uchaguzi wa serikali za mitaa unakaribia.
Utaona pia baada ya utekaji na mauaji ya Ali Kibao, CHADEMA wakaja na bango la kusema waziri Masauni na IGP wajiuzulu kwalengo la uwajibikaji, lakini wao wanajua fika kabisa kwamba hata kama watajiuzulu Masauni na IGP, sio kwamba eti ndo mifumo ya kuendesha hizi taasisi utabadilika, ila kwao wao CHADEMA kujiuzulu kwa hawa watu maana yake ni ushindi mwingine kwao kwamba hawa walifanya uhalifu, na usishangae wakaja na kauli ya kuwafungulia mashitaka. Hapo hapo unasikia ya kwamba, hawataki tena polisi kuchunguza hili tukio wanawataka ‘Scotland Yard etc etc’, maana yake ni kwamba wanajua kabisa haya hayawezi kutekelezwa lakini kwao CHADEMA itawafanya wazidi kupata space za ku apply more pressure.
Makosa ya CCM
Kosa la kwanza walilofanya viongozi wa CCM ni kudhani kwamba itafika mahali CCM na CHADEMA wataongea lugha moja. Na hii approach CCM waliijaribu sana kipindi cha hayati Magufuli kwa kutumia nguvu kubwa ya fedha kununua makada wa CHADEMA wakiamini kwamba wataidhoofisha, lakini, taswira ninayoiona kwa sasa ni ya tofauti sana, ni kwamba kuna muelekeo wa CHADEMA kuendelea kuwa na viongozi ngangari kadri siku zinavyokwenda.
Kosa la pili la CCM ni kwamba, kwa miaka mingi wamekuwa wakijipambanua zaidi kuwakosoa CHADEMA badala ya kuangalia objectivity ya narrative zinazoibuliwa na CHADEMA na pia upepo wa hizo narratives kwenye jamii ya wapiga kura umekaaje.
Endapo kama CCM wangechagua kuwa upande wa objective zaidi, isingewalazimu kutumia nguvu kubwa kupambana na kila hoja ya CHADEMA. Maana yake ni kwamba kuna issues ambazo zinaanzia kwa watu wasio hata wanasiasa wa CHADEMA mfano mambo kama vikokotoo vya mafao ambavyo vinagusa watumishi wengi. Just kwa sababu CHADEMA wanapinga kikokotoo, haikuwa na ulazima kwa CCM kuwapinga na kusema kikokotoo ni kizuri. Matokeo yake public inasimama na CHADEMA na CCM inajikuta ikipata aibu ya kushindwa kwenye hoja. Ilihali kama, wangechagua kuwa objective, wasingejikuta kwenye hiyo hali ya kukaa upande wa kushindwa.
Mfano mwingine wa kusikitisha kwenye tukio la hivi majuzi la kutekwa na kuuawa kwa Ali Kibao, nikasoma ujumbe wa mwenyekiti wa Umoja Vijana wa CCM akijaribu kutoa statement ya dhihaka na kebeki kwa tukio ambalo lime raise public tension badala ya kuwa upande wa public na kutoa comforting statement yeye aliishia kuandika hivi <<INANIPA UKAKASI KUONA WAKWANZA KUTUPA TAARIFA ZA UTEKAJI NDIO WA KWANZA KUTUPA TAARIFA ZA VIFO”.>> kitu ambacho kwangu ilikuwa ni unncecessary na inazidi kuwa expose zaidi CCM kwamba hata viongozi wao wakubwa wameshindwa minyukano na pressure za CHADEMA.
Udhaifu wa CCM utawapa shida vyombo vya ulinzi
Kama nilivyoanza kwa kusema kwamba ni vigumu kutenganisha kati ya CCM, Serikali, na Vyombo Vya Ulinzi, inamaana kubwa kwamba endapo CCM ikiendelea kujidhihirisha kwamba wameshindwa kupambana na CHADEMA kwenye medani za hoja maana yake ni kwamba watawapa shida sana jeshi la polisi na vyombo vya ulinzi.
Kibaya zaidi nachokiona kikitokea kwa kipindi kifupi kijacho ni endapo pia kama hawa vijana waliotekwa watashindwa kupatikana maana yake nao watakuwa wameuawa. Hiyo maana yake itaibua kuongezeka kwa pressure kubwa kutoka CHADEMA na jumuia ya kimataifa, ukizingatia ya kwamba tayari mauaji ya Kibao yamewazindua wakubwa wa dunia ambao its obvious bado Tanzania hatuna kinga dhidi yao.
Hivyo nachokiona ni kwamba, iwe iwavyo, haya maandamano waliyoyapanga CHADEMA tarehe 23 ni kete ngumu sana kwa CCM, Serikali, na Vyombo vya Ulinzi na zinaenda kuwa siku 10 tough sana ambazo nategemea zitakuwa na matamko mengi sana kutoka CCM, Vyombo vya Ulinzi na Serikali na mbali na hayo nategemea kuona surprises kubwa kabla ya terehe 23 yenyewe na baada ya hapo.
Jicho la kifalsafa na Chief Ortambo!
Kisayansi, unapokutana na maada (Matter) mfano wa lijiwe likubwa na ukatakiwa uweze kulitawanyisha vipande vipande, huwa ni kazi ngumu sana ikiwa ulichonacho mkononi ni nyundo ndogo tu.
Kwa tafsiri ya picha, CCM inawakilisha hilo jiwe kubwa ambalo limejiimarisha kwenye siasa za Tanzania na wameweza kukita mizizi yao kwenye serikali na vyombo vya dola (yaani inakuwa ni ngumu sana kutenganisa hivo vitu vitatu). Hii imekuwa ikiwapa faida kwenye chaguzi za kufanya chochote wakitakacho kujihakikisha ushindi (hata hizi chaguzi zinazokuja karibuni, sitegemei mabadiliko yeyote suala la CCM kushinda, hata CHADEMA hilo wanalielewa). Halafu sasa huyo mtu mwenye kinyundo kidogo naichukulia kama ndo chama cha CHADEMA, wao wanajua kabisa kwamba ni ngumu sana kuisambaratisha CCM, ‘lakini sio kwamba ni jambo lisilowezekana’.
Kwa mbinu za kisayansi, jiwe hilo linaweza kuvunjwa na kusambaratishwa endapo likiwa subjected to pressure, japo sio investment ya miaka miwili au mitatu, yaweza kuchukua muda mrefu, lakini pia yaweza kuchukua muda mfupi kulingana na mazingira na reaction mbali mbali wakati pressure ikiwa applied.
Kwa mtu mwenye nyundo, applying pressure kwenye jiwe kama hilo, maana yake ni kuanza kulikagua sehemu zenye muonekano wa kuwa dhaifu (Vulnerable areas) kama vile nyufa n.k, kisha sasa ku apply constant pressure kwenye kila sehemu ambayo ni dhaifu. Na namna ya ku apply pressure maana yake ni kuanza kuligonga hilo jiwe kila siku sehemu zote zenye ufa. Zoezi hili linahitaji determination and discpline, kwamba, unawezaje kuamka kila siku asubuhi kuligonga lijiwe likubwa kwa kutumia kanyundo kadogo? Swali hilo ndo linatupeleka kujibu lile swali la ‘Ni kwanini ni CHADEMA tu inayotamkwa kila siku kwenye midomo ya watu miaka nenda rudi angali kuna vyama vya upinzani zaidi ya 16?’ Jibu lake pia lipo kwamba, labda ni chama pekee kinachoamini kwamba jiwe linaweza kuvunjwa endapo kama ukiwa determined na discpline ya ku apply pressure kila siku bila kujali kama jiwe linavunjika ama halivunjiki.
Matokeo ya Ku apply Constant Pressure kwenye Jiwe
Guaranteed, kutakuwa na tofauti kwenye jiwe ikiwa litagongwa mara elfu moja (1000) na tofauti itazidi kuonekana mgongaji akizidi kugonga. Kuna nyufa ambazo zitaanza kuongezeka na kujiachia au jiwe litaanza kujimega kidogo kidogo. Kwenye hii process, naona kabisa mgongaji akijikusanyia faida tatu kadri anavyoligoga jiwe;
- Kila nyundo inamegua jiwe kipande kidogo, japo kuna wakati mgongaji pia anaweza kujeruhiwa na vipande vidogo vidogo vikamrukia machoni, lakini haibadili ukweli kwamba jiwe linazidi kumeguka.
- Jiwe linavyogongwa linazidi kupata moto na kunaweza kutokea reaction ndani ya jiwe ambayo inaweza kuzidi kulidhoofisha jiwe.
- Mgongaji anaweza kukutana na ufa ambao una uwezo wa kusambaratisha jiwe kwa nyundo moja (Kama falsafa ya wachimba dhahabu, kwamba pale unapofikiria kuacha kuchimba unajikuta ukiendelea kupiga baruti mwamba ukiamini mali i karibu na usikate tamaa mapema)
CHADEMA na Law of Pressure
Hichi ndicho wamekuwa wakikifanya CHADEMA kwa miaka 15 iliyopita na wanaendelea kukifanya mpaka sasa. Kutafuta vulnerabilities kwenye mfumo wa dola wa CCM na kutengeneza ‘Narratives’ za kuanza ku ‘attack’ mfumo.
Mambo kama maandamano madogo madogo, kampeni za hapa na pale, kudai katiba mpya etc etc zimekuwa nyingi sana kwa CHADEMA
Mimi najua kabisa hata ndani ya CHADEMA watakuwa wanajua kabisa ya kwamba, maandamano kwa set up ya nchi hii hayafui dafu, lakini wao wamekuwa wakiyafanya anyway kwasababu wanajua kabisa kupitia maandamano kuna cheche na counteractions lazima zitokee. Unamsikia leo Msemaji wa Jeshi la Polisi ametia mguu, kuyaita kwamba maandamano yaliyopangwa ni batili, maana yake ni kwamba, CHADEMA ninayoijua mimi, hii kwao pia ni ushindi mkubwa, kwasababu unaona kabisa either kuna possibility ya mtifuano kati ya CHADEMA na POLISI au POLISI wakubali kuyaruhusu off which ni ushindi kwa CHADEMA ukizingatia kauli mbiu ya maandamano yenyewe ‘SAMIA MUST GO’ nayo imekaa pabaya sana kwa serikali na CCM ukizingatia kwamba uchaguzi wa serikali za mitaa unakaribia.
Utaona pia baada ya utekaji na mauaji ya Ali Kibao, CHADEMA wakaja na bango la kusema waziri Masauni na IGP wajiuzulu kwalengo la uwajibikaji, lakini wao wanajua fika kabisa kwamba hata kama watajiuzulu Masauni na IGP, sio kwamba eti ndo mifumo ya kuendesha hizi taasisi utabadilika, ila kwao wao CHADEMA kujiuzulu kwa hawa watu maana yake ni ushindi mwingine kwao kwamba hawa walifanya uhalifu, na usishangae wakaja na kauli ya kuwafungulia mashitaka. Hapo hapo unasikia ya kwamba, hawataki tena polisi kuchunguza hili tukio wanawataka ‘Scotland Yard etc etc’, maana yake ni kwamba wanajua kabisa haya hayawezi kutekelezwa lakini kwao CHADEMA itawafanya wazidi kupata space za ku apply more pressure.
Makosa ya CCM
Kosa la kwanza walilofanya viongozi wa CCM ni kudhani kwamba itafika mahali CCM na CHADEMA wataongea lugha moja. Na hii approach CCM waliijaribu sana kipindi cha hayati Magufuli kwa kutumia nguvu kubwa ya fedha kununua makada wa CHADEMA wakiamini kwamba wataidhoofisha, lakini, taswira ninayoiona kwa sasa ni ya tofauti sana, ni kwamba kuna muelekeo wa CHADEMA kuendelea kuwa na viongozi ngangari kadri siku zinavyokwenda.
Kosa la pili la CCM ni kwamba, kwa miaka mingi wamekuwa wakijipambanua zaidi kuwakosoa CHADEMA badala ya kuangalia objectivity ya narrative zinazoibuliwa na CHADEMA na pia upepo wa hizo narratives kwenye jamii ya wapiga kura umekaaje.
Endapo kama CCM wangechagua kuwa upande wa objective zaidi, isingewalazimu kutumia nguvu kubwa kupambana na kila hoja ya CHADEMA. Maana yake ni kwamba kuna issues ambazo zinaanzia kwa watu wasio hata wanasiasa wa CHADEMA mfano mambo kama vikokotoo vya mafao ambavyo vinagusa watumishi wengi. Just kwa sababu CHADEMA wanapinga kikokotoo, haikuwa na ulazima kwa CCM kuwapinga na kusema kikokotoo ni kizuri. Matokeo yake public inasimama na CHADEMA na CCM inajikuta ikipata aibu ya kushindwa kwenye hoja. Ilihali kama, wangechagua kuwa objective, wasingejikuta kwenye hiyo hali ya kukaa upande wa kushindwa.
Mfano mwingine wa kusikitisha kwenye tukio la hivi majuzi la kutekwa na kuuawa kwa Ali Kibao, nikasoma ujumbe wa mwenyekiti wa Umoja Vijana wa CCM akijaribu kutoa statement ya dhihaka na kebeki kwa tukio ambalo lime raise public tension badala ya kuwa upande wa public na kutoa comforting statement yeye aliishia kuandika hivi <<INANIPA UKAKASI KUONA WAKWANZA KUTUPA TAARIFA ZA UTEKAJI NDIO WA KWANZA KUTUPA TAARIFA ZA VIFO”.>> kitu ambacho kwangu ilikuwa ni unncecessary na inazidi kuwa expose zaidi CCM kwamba hata viongozi wao wakubwa wameshindwa minyukano na pressure za CHADEMA.
Udhaifu wa CCM utawapa shida vyombo vya ulinzi
Kama nilivyoanza kwa kusema kwamba ni vigumu kutenganisha kati ya CCM, Serikali, na Vyombo Vya Ulinzi, inamaana kubwa kwamba endapo CCM ikiendelea kujidhihirisha kwamba wameshindwa kupambana na CHADEMA kwenye medani za hoja maana yake ni kwamba watawapa shida sana jeshi la polisi na vyombo vya ulinzi.
Kibaya zaidi nachokiona kikitokea kwa kipindi kifupi kijacho ni endapo pia kama hawa vijana waliotekwa watashindwa kupatikana maana yake nao watakuwa wameuawa. Hiyo maana yake itaibua kuongezeka kwa pressure kubwa kutoka CHADEMA na jumuia ya kimataifa, ukizingatia ya kwamba tayari mauaji ya Kibao yamewazindua wakubwa wa dunia ambao its obvious bado Tanzania hatuna kinga dhidi yao.
Hivyo nachokiona ni kwamba, iwe iwavyo, haya maandamano waliyoyapanga CHADEMA tarehe 23 ni kete ngumu sana kwa CCM, Serikali, na Vyombo vya Ulinzi na zinaenda kuwa siku 10 tough sana ambazo nategemea zitakuwa na matamko mengi sana kutoka CCM, Vyombo vya Ulinzi na Serikali na mbali na hayo nategemea kuona surprises kubwa kabla ya terehe 23 yenyewe na baada ya hapo.
Jicho la kifalsafa na Chief Ortambo!