Falsafa ya MATAGA - Make Tanzania Great Again

Falsafa ya MATAGA - Make Tanzania Great Again

zimmerman

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2011
Posts
1,644
Reaction score
3,176
Wale wanaobeza wengine kwa kuwaita MATAGA wanafanya hivyo wakielewa hata maana ya neno MATAGA "Make Tanzania Great Again"?
Taifa lilikuwa linaielekea kubaya hadi 2015, na watu tulitaka mwelekeo mpya wa nchi yetu.
Doctrine ya MATAGA ni kujenga nchi yenye sifa zifuatazo:

Viongozi watakaoweka maslahi ya taifa kwanza, badala ya kuifanya Tanzania shamba la bibi.
Nchi itakayozalisha Made in Tanzania za kutosha, badala ya kujenga uchumi wa kichuuzi.
Nchi itakayojitosheleza kinishati.
Nchi yenye miundombinu bora ya usairishaji wa nchi kavu, majini na angani.
Nchi yenye sauti, kwamba kiongozi wa Tanzania akitamka Afrika na dunia nzima isikie -- kama Nyerere alivyokuwa.
Nchi ya wachapakazi, wazalishaji na inayojitosheleza kichakula na kwa mahitaji mengine ya msingi.
Nchi tajiri, na inayoukataa umaskini akilini hadi kivitendo.
Nchi yenye uthubutu wa kunia na kufanya makubwa.

Ninatazamia siasa za Tanzania kuelekea 2025 zitawagawa watanzania katika makundi haya mawili.
Kundi la kwanza ni kundi linaloamini katika falsafa ya MATAGA, kwamba Tanzania ina potential, na ikithubutu inaweza.
Kundi la pili ni kundi la wanaojikunyata, wanaoamini bila kudra kutoka Washington au Beijing, basi hatuwezi.

Kwa wale mtakaowania 2025 tunarudia kusema tena spirit ya Hayati Magufuli haijafa!
 
Wale wanaobeza wengine kwa kuwaita MATAGA wanafanya hivyo wakielewa hata maana ya neno MATAGA "Make Tanzania Great Again"?
Taifa lilikuwa linaielekea kubaya hadi 2015, na watu tulitaka mwelekeo mpya wa nchi yetu....
Nia haikuwa mbaya ila utekelezaji ulikuwa mbovu kupita kiasi. Nadhani shida kubwa ilikuwa aina ya watu waliohusika kumshauri Rais namna ya kutekeleza miradi hiyo. Viwanda vyenyewe mpaka sasa havionekani, miradi mingi iliambatana na ukiukwaji wa taratibu ulioleta hasara pamoja na kuzalisha kesi zisizokuwa na tija.

Kuna task force zilijipa kazi ya kuzunguka nchi nzima kazi ikiwa ni kuwatia adabu wafanyabiashara kwa kuwabambikia kodi feki. Kuna watu walikuwa wanamshauri Rais wakijiita "thinking tanks" nadhani wanapaswa kuitwa ni "sinking tanks" kwani ndio walioshauri kununua ndege kwa cash, kujenga miundo mbinu mikubwa kwa fedha za ndani badala ya kutumia PPP.

Ili Mama apige hatua, lazima asafishe magenge yaliyo ndani ya serikali ambayo yaliasisiwa na mwendazake.
 
Wale wanaobeza wengine kwa kuwaita MATAGA wanafanya hivyo wakielewa hata maana ya neno MATAGA "Make Tanzania Great Again"?
Taifa lilikuwa linaielekea kubaya hadi 2015, na watu tulitaka mwelekeo mpya wa nchi yetu...
Magufuli kaahajiondokea na kila kitu wewe unaonekana kama mwendawazimu tu.

Habari ya Tanzania kwa sasa ni mama Samia tuuuuu.
 
Wale wanaobeza wengine kwa kuwaita MATAGA wanafanya hivyo wakielewa hata maana ya neno MATAGA "Make Tanzania Great Again"?
Taifa lilikuwa linaielekea kubaya hadi 2015, na watu tulitaka mwelekeo mpya wa nchi yetu....
Baada ya Ku"Make Tanzania Great Again " ndio akaigeuza akaifanya "Make Sukuma Gang Great Again"
 
Wale wanaobeza wengine kwa kuwaita MATAGA wanafanya hivyo wakielewa hata maana ya neno MATAGA "Make Tanzania Great Again"?
Taifa lilikuwa linaielekea kubaya hadi 2015, na watu tulitaka mwelekeo mpya wa nchi yetu.
Doctrine ya MATAGA ni kujenga nchi yenye sifa zifuatazo:

Viongozi watakaoweka maslahi ya taifa kwanza, badala ya kuifanya Tanzania shamba la bibi.
Nchi itakayozalisha Made in Tanzania za kutosha, badala ya kujenga uchumi wa kichuuzi.
Nchi itakayojitosheleza kinishati.
Nchi yenye miundombinu bora ya usairishaji wa nchi kavu, majini na angani.
Nchi yenye sauti, kwamba kiongozi wa Tanzania akitamka Afrika na dunia nzima isikie -- kama Nyerere alivyokuwa.
Nchi ya wachapakazi, wazalishaji na inayojitosheleza kichakula na kwa mahitaji mengine ya msingi.
Nchi tajiri, na inayoukataa umaskini akilini hadi kivitendo.
Nchi yenye uthubutu wa kunia na kufanya makubwa.

Ninatazamia siasa za Tanzania kuelekea 2025 zitawagawa watanzania katika makundi haya mawili.
Kundi la kwanza ni kundi linaloamini katika falsafa ya MATAGA, kwamba Tanzania ina potential, na ikithubutu inaweza.
Kundi la pili ni kundi la wanaojikunyata, wanaoamini bila kudra kutoka Washington au Beijing, basi hatuwezi.

Kwa wale mtakaowania 2025 tunarudia kusema tena spirit ya Hayati Magufuli haijafa!

Umesahahu falsafa ya Mauaji na utekaji pia vitisho.
Kifupi MATAGA ni UDIKTETA UCHWARA
 
Back
Top Bottom