Familia yataka haki kijana aliyedai kuvunjwa mguu na polisi

Familia yataka haki kijana aliyedai kuvunjwa mguu na polisi

Inside10

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2011
Posts
29,909
Reaction score
32,414
Screenshot_20240918-200658.jpg
Familia ya kijana aliyedai kupigwa hadi kuvunjwa mguu na askari polisi ndani ya chumba cha mahojiano, wamelitaka Jeshi la Polisi kumfikisha mahakamani mtuhumiwa huyo, ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yake.

Kijana huyo, Peter Charles (21), mkazi wa kata ya Daraja Mbili jijini Arusha, alidai kupigwa hadi kuvunjwa mguu na askari polisi, akimlazimisha kukiri kosa la kujihusisha na kucheza kamari.

Mei 29, 2024 saa moja usiku, wakiwa watatu nyumbani kwa mmoja wa rafiki yao wakitazama runinga, askari waligonga mlango na kuingia, wakajitambulisha kuwa wao ni askari, wakawabeba kuwaingiza kwenye gari walilokuja nalo.

Akizungumza na Mwananchi nyumbani kwao, leo Septemba 18, 2024, walezi wa kijana huyo, wamesema tangu kutokea kwa tukio hilo, hakuna hatua zilizochukuliwa kwa mtuhumiwa, ikiwemo kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili.

Akizungumzia suala hilo, Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha, Justine Masejo amesema bado suala hilo linashughulikiwa katika hatua za awali na likikamilika hatua za kimahakama zitafuata.

“Tunashughulikia, bado liko ngazi za chini na likikamilika litafikishwa ngazi ya kimahakama, hivyo subirini tu,” amesema Kamanda Masejo.

Soma Pia:

Bibi wa kijana huyo, Getrude Mollel (61) ameiomba Serikali kuchukua hatua za kisheria, ili mjukuu wake apate haki na pia iwe fundisho kwa wengine.

 
Nilimchongea mzee mmoja alikuwa akiuza bangi, sasa kaka yangu alikuwa mteja wake alimharibu kaka yangu. Nikaita police wamkamate lakini wao waliuza bangi wakagawana fedha ya mauzo. Polisi wengine sio watiifu wa kazi
 
Nilimchongea mzee mmoja alikuwa akiuza bangi, sasa kaka yangu alikuwa mteja wake alimharibu kaka yangu. Nikaita police wamkamate lakini wao waliuza bangi wakagawana fedha ya mauzo. Polisi wengine sio watiifu wa kazi
Unoko huo... kaka yako alikuwa anafuata bange mwenyewe hakulazimishwa
 
Familia ya kijana aliyedai kupigwa hadi kuvunjwa mguu na askari polisi ndani ya chumba cha mahojiano, wamelitaka Jeshi la Polisi kumfikisha mahakamani mtuhumiwa huyo, ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yake...
Ni chumba cha mahojioano au chumba cha mateso?.Maana humo kwa ajili ya mateso inaweza sababisha mtu kukiri uongo ili aachiwe
 
Nilimchongea mzee mmoja alikuwa akiuza bangi, sasa kaka yangu alikuwa mteja wake alimharibu kaka yangu. Nikaita police wamkamate lakini wao waliuza bangi wakagawana fedha ya mauzo. Polisi wengine sio watiifu wa kazi
Pole Alice
 
Familia ya kijana aliyedai kupigwa hadi kuvunjwa mguu na askari polisi ndani ya chumba cha mahojiano, wamelitaka Jeshi la Polisi kumfikisha mahakamani mtuhumiwa huyo, ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yake.

Kijana huyo, Peter Charles (21), mkazi wa kata ya Daraja Mbili jijini Arusha, alidai kupigwa hadi kuvunjwa mguu na askari polisi, akimlazimisha kukiri kosa la kujihusisha na kucheza kamari.

Mei 29, 2024 saa moja usiku, wakiwa watatu nyumbani kwa mmoja wa rafiki yao wakitazama runinga, askari waligonga mlango na kuingia, wakajitambulisha kuwa wao ni askari, wakawabeba kuwaingiza kwenye gari walilokuja nalo.

Akizungumza na Mwananchi nyumbani kwao, leo Septemba 18, 2024, walezi wa kijana huyo, wamesema tangu kutokea kwa tukio hilo, hakuna hatua zilizochukuliwa kwa mtuhumiwa, ikiwemo kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili.

Akizungumzia suala hilo, Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha, Justine Masejo amesema bado suala hilo linashughulikiwa katika hatua za awali na likikamilika hatua za kimahakama zitafuata.

“Tunashughulikia, bado liko ngazi za chini na likikamilika litafikishwa ngazi ya kimahakama, hivyo subirini tu,” amesema Kamanda Masejo.

Soma Pia:

Bibi wa kijana huyo, Getrude Mollel (61) ameiomba Serikali kuchukua hatua za kisheria, ili mjukuu wake apate haki na pia iwe fundisho kwa wengine.

Kisasi ni haki kwa wale Watu ambao wamedhulumiwa haki zao.
 
Nilimchongea mzee mmoja alikuwa akiuza bangi, sasa kaka yangu alikuwa mteja wake alimharibu kaka yangu. Nikaita police wamkamate lakini wao waliuza bangi wakagawana fedha ya mauzo. Polisi wengine sio watiifu wa kazi
Ushuhuda Wako Ni Mzuri.
Lakini Usipende Sana kujihusisha na Mambo ya watu.
 
Back
Top Bottom