Fani/ujuzi unaoweza kumsaidia mtoto wa kike kujikomboa kiuchumi

Fani/ujuzi unaoweza kumsaidia mtoto wa kike kujikomboa kiuchumi

Kingjr2

JF-Expert Member
Joined
Sep 8, 2018
Posts
644
Reaction score
1,274
Heshima kwenu wanajukwaa

Wahenga waliposema ukubwa ni jalala hawakukosea, walikuwa sahihi kabisa

Niko na wadogo zangu wa kike hapa baada ya kumaliza kidato cha nne hawakufanikiwa kufanya vizuri. Kama mjuavyo jamii imetuaminisha ili ufanikiwe lazima usome upate kazi nzuri hivyo wakajaribu bahati zao tena kwa ku reseat. Hata hivyo hawakuambulia chochote tena

Kwa vile nafahamu uwezo wao kwa masomo haya ya darasani na pia kwa vile nafahamu si lazima kupitia mlango mmoja tu wa mafanikio, ikabidi niwape moyo na kuwashauri watafute fani wanazozipenda

Wote wawili wanaonyesha kutaka ushonaji. Najua ni kwasababu ni wasichana na hawajaona option nyingine. Nami nimejaribu kutafuta fani nyingine naona kichwa kinauma tu

Sido wanafundisha ujuzi wao kwa muda mfupi sana na wamejikita zaidi kwenye usindikaji wa vyakula. Nimejaribu kufuatilia naona wanaendesha mafunzo yao kikanda kwa wiki moja moja tu kitu ambacho kwa begginer ni ngumu ku catch-up

Nakuja kwenu kuomba ushauri kwanza wa fani inayoweza kumsaidia mtoto wa kike kujiajiri na akiweka juhudi atafanikiwa

Na pili kwa yeyeto anayefahamu vikundi au Taasisi zinazoendesha mafunzo ya fani mbalimbali kwa watoto wa kike mbali na VETA na SIDO (VETA interview zao sio rafiki sana hata sijui kwanini mfumo wetu wa elimu unalazimisha haya)

Hata hivyo nitashukuru kupewa mawazo mengine hata nje ya haya

Msaada wenu tahadhari
 
Wapeleke wajifunze kupika...bites..keki vyakula vingine! Waoneshe /ikiwezekana uwapeleke mara kwa mara kwa wadada/wamama waliofanikiwa kupitia hizo ajira
Wakifaulu vyema wafungulie mgahawa! La muhimu wasikilize wanachotaka!
Nb! Kamwe usiwape uhuru wanaoutaka!
 
Biashara,
Kama mtaji upo wafungulie biashara uwaajiri simamia biashara hio kwa ukaribu
Mfano,duka la vipodozi na urembo,duka la nguo n.k

NB:kama hauna uzoefu na biashara utakayowafungulia subiri ushauri mwingine
 
Kwani huo ushonaji waliotaka wao una shida? Mbona ni fani nzuri tu. Wapeleke SSF training institute arusha chuo cha urembo na ushonaji cha waschana tu chenye gharama nafuu na weledi wa hali ya juu.

Tena wana hostel free na mwanafunzi anasoma masomo yote. Mara ya mwisho ada ilikua 60000 kwa mwezi sijui sahv
 
Wapeleke wajifunze kupika...bites..keki vyakula vingine! Waoneshe /ikiwezekana uwapeleke mara kwa mara kwa wadada/wamama waliofanikiwa kupitia hizo ajira
Wakifaulu vyema wafungulie mgahawa! La muhimu wasikilize wanachotaka!
Nb! Kamwe usiwape uhuru wanaoutaka!
Mimi huwa naona wanawake wana wigo mpana na kila wanachofanya kinahitaji mtaji mdogo na vina potential ya kuwa biashara kubwa mfano huo upishi, urembo (make up), ushonaji na vinginevyo

Au ni imaginations zangu tu
 
Mimi huwa naona wanawake wana wigo mpana na kila wanachofanya kinahitaji mtaji mdogo na vina potential ya kuwa biashara kubwa mfano huo upishi, urembo (make up), ushonaji na vinginevyo

Au ni imaginations zangu tu

Uko sahihi..ila ukitia NIA hasahsa! Sio kufanya mradi na wewe uonekane unatoka asbh home kwenda shule/chuo! Unajidanganya!
 
Uko sahihi..ila ukitia NIA hasahsa! Sio kufanya mradi na wewe uonekane unatoka asbh home kwenda shule/chuo! Unajidanganya!

Ni kweli maana kuna wengine wanafanya biashara ya kushona na ndani ya miaka mitano bhasi wana cloth line /brand zao za nguo na kuna wengine walitushonea viraka toka tupo primary ila hadi leo wapo kwenye zile zile cherehani mbili.

Simply sio unachofanya ila unavyokifanya ndo muhimu katika mafanikio au sio !!.
 
Ni kweli maana kuna wengine wanafanya biashara ya kushona na ndani ya miaka mitano bhasi wana cloth line /brand zao za nguo na kuna wengine walitushonea viraka toka tupo primary ila hadi leo wapo kwenye zile zile cherehani mbili.

Simply sio unachofanya ila unavyokifanya ndo muhimu katika mafanikio au sio !!.
Umemaliza!....hapo ni kuadd value aka kujiongeza
 
Kwani huo ushonaji waliotaka wao una shida? Mbona ni fani nzuri tu. Wapeleke SSF training institute arusha chuo cha urembo na ushonaji cha waschana tu chenye gharama nafuu na weledi wa hali ya juu. Tena wana hostel free na mwanafunzi anasoma masomo yote. Mara ya mwisho ada ilikua 60000 kwa mwezi sijui sahv
Nashukuru kwa mchango wako,

Ushonaji hauna shida kabisa na ndiomaana nikaja kwenu kuomba kwa anayefahamu Taasisi au vikundi vilivyorasmi vinavyojishughulisha na mambo kama hayo

Imani yangu ni kwamba wakiwa huko ni rahisi kupata ujuzi mwingi wa vitu mbalimbali kama kushona bidhaa za ngozi, mikoba nk kuliko kuishia kujifunza mtaani kwa mtu tu
 
Upishi pia

Ushonaji wakati huo unaonaje wakapata uzoefu kwa mafundi cherehani moja kwa moja?.!
 
Hapo ufundi cherehani(ushonaji) tu utawatoa. Fani ziingine kwa sasa ni kubahatisha mnoo. Waanzie kwenye cherehani, mambo mengine watajiongeza wenyewe.

Tatizo hapo litakuwa ni wao kuikubali hiyo fani. Mabinti wengi wa kisasa hawataki kujifunza cherehani, wanaona ushamba au aibu fulani hivi.
 
Nashukuru kwa mchango wako,

Ushonaji hauna shida kabisa na ndiomaana nikaja kwenu kuomba kwa anayefahamu Taasisi au vikundi vilivyorasmi vinavyojishughulisha na mambo kama hayo

Imani yangu ni kwamba wakiwa huko ni rahisi kupata ujuzi mwingi wa vitu mbalimbali kama kushona bidhaa za ngozi, mikoba nk kuliko kuishia kujifunza mtaani kwa mtu tu.
Unaweza kuwacheck 0758119650
 
Back
Top Bottom