Pre GE2025 Faris Buruhani Aongoza Bonanza la Mtani wa Jadi, SIMBA vs YANGA Kata ya Nyakibimbili

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301
Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Kagera Ndugu Faris Buruhani, ameongoza BONANZA la mpira wa miguu kati ya timu za mashabiki wa Simba na mashabiki wa Yanga iliyochezwa katika uwanja wa shule ya Msingi Lyamahoro, katika kata ya Nyakibimbili.


Ndugu Faris, amelitumia Bonanza hilo kuwashukuru wananchi wa Nyakibimbili kwa kuendelea kuiamini CCM katika Uchaguzi uliopita wa Serikali za Mitaa, huku akiwaomba kuendelea kuichagua CCM katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu 2025.


Ndugu Faris amekabidhi zawadi ya Mbuzi watatu kwa timu mbili zilizoshiriki Bonanza hilo huku akimshukuru Mwenyekiti wa UVCCM kata ya Nyakibimbili na kamati yake ya Utekelezaji kwa kuendelea kuwaunganisha vijana wa kata yao kupitia michezo.

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…