Fastjet amerudisha Airbus zake, kulikoni?

UKWELI NI HUU

JF-Expert Member
Joined
Jul 31, 2016
Posts
262
Reaction score
412
Habari wanajamvi?

Miezi michache iliyopita kampuni ya usafiri wa anga hapa nchini Tanzania FastJet ilisitisha matumizi ya ndege za Airbus A319 na kuamua kutumia ndege ndogo za Embraer E190 kwa kushirikiana na kampuni kutoka Hungary.

Leo hii FastJet kutoka Mwanza kwenda Dar ilikuwa Airbus A319 na hata katika uwanja wa ndege wa JK Nyerere jijini Dar es salaam mchana wa leo kulikuwa na Airbus A319 nyingine mbili.

Ni nini kimetokea hapa katikati?
Wateja wameongezeka tena Tanzania?

Cc barafu
 

Ungewauliza wao, halafu watwambie kwanini wanaleta wahudumu wasiojua Kiswahili ama Kiingereza mwisho wanaishia kutoa ishara zinazoweza leta maana mbaya hasa wakati wa kuuza chai na vitafunwa vingine kwenye ndege zao
 
Ungewauliza wao, halafu watwambie kwanini wanaleta wahudumu wasiojua Kiwahili ama Kiingereza mwisho wananishai kutoa ishara zinazowezakutafsiriwa vibaya hasa wakati wa kuuza chai na vitafunwa vingine kwenye ndege zao

Ni rahisi kupata jibu hapa jukwaani kuliko kuwatafuta wao
 
Wameondoa wabulgeria waliokuwa wanaongea Kiingereza cha kirusi wameleta wazimbabwe sijui watu wa wapi.
Ila abiria wachache
 
hahahahah maana yake biashara ni nzuri sana .....pigo kwa wale waomba mabaya
 
Hawakuziondoa completely, walipunguza tu.
 
Anajiaandaa kibiashara kushindana na wapinzani wake Air Bus iko juu ya bombarded na iko class sawa na Boeing
 
Nilishangaa walipoiondoa. A319 is a "horse" of airtravel.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…