FastJet: Mwanza - Kilimanjaro nauli tsh 32,000... (Bila VAT)

Wi-Fi

JF-Expert Member
Joined
Aug 30, 2011
Posts
2,091
Reaction score
1,381
Hii ni kampuni mpya inayoanza safari za ndege, nauli ni bila VAT.

Kwa Dar office zipo mitaa ya Samora opp Wizara ya Nishati na madini karibu na Steers.
 
mkuu hebu pitia vizuri hizo bei ,maana ata bus luxury sio hio bei
 
Usafiri wa ndege unaweza kuwa rahisi hapa Tz kama kungekuwa na ndege nyingi kuleta ushindani. Lakini bei inakuwa kubwa kwa sababu ya kutokuwepo ushindani. Kumbukeni ile ndege ya akina Diallo ilikuwa 75000 MWZ - DAR lakini waliihujumu, sasa ni grounded!
 
Tutasafiri wote Smile, ngoja nikakubukie siti ya dirishani.
Hakuna cha siti ya dirishani wala ya mbele Smile atakaa kwa kebini ya rubani kabisaa tutaongeza nauli kidogo kama cha juu kwa rubani ...lol
 
Last edited by a moderator:
Nilikuwa nasikiliza afisa wao clouds fm asubuhi, anasema chakula ndani ya ndege ni cha kulipia ila unaruhusiwa kuingia na chakula chako ambacho hakitawaudhi abiria wenzanako. Mizigo nayo itakuwa inalipiwa; kilo ishirini za mwanzo ni shilingi elfu nane na kila kilo inayozidi ni shilingi elfu nane.
 
Hizo ndio ndege ambazo wanasema ni za bei rahisi
Sasa nnahisi kabisa kuwa humu ndani badala ya kupewa sandwich tutakuwa tunapewa UBUYU
 
mkuu ushuru upo, hiyo 32,000tshs ni nauli tu bila ushuru. Pia mzigo wa 20kg unalipiwa 8000tsh, vivyo hivyo na kwa kila kilogramu moja inayoongezeka inalipiwa 8000tshs.
 
Jamani naomben ukweli katika hii nami nipande ndege kidigo nitie baraka maisha yangu npo mwanza familia ipo dar
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…