Fatma Karume: Yaani leo nimethibitisha Adelardus (AG) hajui Katiba, anadai Serikali ina mihimili mitatu na yeye ndie anasimamia yote

Fatma fungua pingamizi la mgombea wa CCM hajaziliwa Tanzania
 
Mambo mawili;
1. Mwanasheria Mkuu wa Serikali ni Wakili hivyo kwa yeye kuwa mtaalamu wa masuala ya Sheria anaswihi kumshauri mtu/taasisi kuhusu sheria

2. Kwa mujibu wa katiba (sikumbuki kifungu)
Wakili yeyote ni mtaalamu wa sheria lakini siyo mshauri wa mamlaka wewe mwanasheria mkuu unapata wapi mamlaka ya kuwa mshauri wa mahakama ?

Hiyo katiba ya chato ndiyo itakuwa na hicho kifungu ulichokisahau.
 
Fatuma aliwahi kukariri kifungu cha sheria kilichofutwa,katika wanasheria watypu kichwani ni huyo
Mwanasheria makini hawezi kuleta ushahidi uliotolewa dhidi yake huku mitandaoni wakati kuna kesi inaendelea
Fatuma aache unazi,sheria sio historia
 
Dola (kwa kiingereza "State") ndio yenye Mihimili Mitatu ambayo ni 1. Serikali 2. Bunge na 3. Mahakama. Serikali Kuu ( Central Goverment) ni sehemu ya Serikali kama ilivyo Serikali za Mitaa ( Local Government).

Amandla...
Hivi unataka kuniambia legislature maanake bunge!? Na parliament nini? au walikosea kusema legislature badala yake wangeandika parliament?
Watanzania tujifunze hiko ni kiingereza
 
Huyo Fatima hajawahi kujua sheria anatembelea jina la babu
JE KOSA LIKO WAPI HAPO? VIFUNGU ALIVYOWEKA HAPO SIYO SAHIHI AU HAVINA UHUSIANO NA ALICHOKISEMA?

JE KATI YAKE NA HUYO MWANASERIA MKUU NI NANI YUKO SAHIHI?
 
Shangazi fatty Karume mimi siko huko naomba namba yako ya simu tu, mengine tutaongea kwa simu
 
Dola (kwa kiingereza "State") ndio yenye Mihimili Mitatu ambayo ni 1. Serikali 2. Bunge na 3. Mahakama. Serikali Kuu ( Central Goverment) ni sehemu ya Serikali kama ilivyo Serikali za Mitaa ( Local Government).

Amandla...
Kama AG ni wa Executive sasa nauliza AG sio part ya bunge? Mbona Mara nyingi hutoa ufafanuzi wa kisheria bungeni na ndie mwandishi wa sheria baada ya kupitishwa na bunge!
 
Kweli wewe ni mpumbavu. Kwa mujibu wa katiba yetu Rais ni kiongozi wa serikali na pia ni Mkuu wa nchi.

Ndiyo sababu anafanya kazi zote mbili. Kuna nchi ambazo Rais siyo kiongozi wa serikali kama India na Uingereza bali zinaongozwa na Waziri Mkuu. Waziri Mkuu hawezi kumuapisha jaji Mkuu, unalifahamu hilo?
 
Hivi unataka kuniambia legislature maanake bunge!? Na parliament nini? au walikosea kusema legislature badala yake wangeandika parliament?
Watanzania tujifunze hiko ni kiingereza

Shida ni kuwa vijana wa siku hizi mnapenda mno kukimbilia kuwakebehi watu kwenye mambo ambayo hamna ufahamu nao. Fungua kwanza kamusi utafute maana ya ku-legislate.

Amandla...
 
Kama AG ni wa Executive sasa nauliza AG sio part ya bunge? Mbona Mara nyingi hutoa ufafanuzi wa kisheria bungeni na ndie mwandishi wa sheria baada ya kupitishwa na bunge!

AG ni sehemu ya Bunge kama walivyo mawaziri (ambao nao ni sehemu ya Executive) isipokuwa yeye hana haki ya kupiga kura. AG ni Mshauri Mkuu wa serikali kwenye mambo ya sheria. Aidha, ni wajibu wake kuhakikisha kuwa maamuzi na matendo ya serikali hayakizani na sheria. Mshauri Mkuu wa Bunge kuhusu Sheria anaitwa Chief Parliamentary Legal Counsel (CPLC), na ni huyu ndie anatakiwa kutoa ufafanuzi wa masuala yote ya sheria ndani ya Bunge. Labda AG anakaribishwa kutoa ufafanuzi wa kisheria kwa sababu karibu bill zote zinaanzishwa na serikali ( bill huandikwa na Chief Parliamentary Draftsman ambae ni sehemu ya Ofisi ya AG) na yeye anahusika sana katika utayarishaji wake. Tatizo litajitokeza pale ambapo bill binafsi italetwa na Mbunge asie sehemu ya serikali. AG hapo hawezi kutoa ufafanuzi maana hatakuwa amehusika katika utayarishaji wake. Bill ikipitishwa na Bunge, inaandikwa upya na Ofisi ya Katibu wa Bunge ( ikiwa na marekebisho yaliyojitokeza kama yapo). Katibu wa Bunge ndie anaiwasilisha kwa Mheshimiwa Rais ili ipate ridhaa yake kabla ya kuwa sheria. AG hapaswi kuhusika katika uandishi wa bill baada ya kupitishwa na Bunge. Jukumu hilo ni la CPLC.

Amandla...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…