FC Genk yakataa dau la Euro milioni 13 kwa Mbwana Samatta kutoka Cardiff City ya Uingereza

Richard

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2006
Posts
15,692
Reaction score
23,038

Mshambuliaji wa kimataifa wa timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars na FC Genk ya Ubelgiji, Mbwana Samatta.

Klabu ya Genk ya Ubelgiji imekataa dau la Euro milioni 13 kutoka kwa timu ya Cardiff City ya Wales.

Dau hilo ambalo liliwekwa jana jioni lilikuwa ni la kwanza kufanywa na haijulikani kama Cardiff City wataongeza dau hilo.

Cardiff City wanatafuta mshambuliaji na pia wanamfuatilia mshambuliaji wa Nantes ya Ufaransa Emiliano Sala ambapo bado timu hizo wanazungumza.

NB:
Habari hizi ni kutoka vyanzo mbalimbali vya uhakika.

Picha kwa hisani ya Photonews kupitia Getty Images.
 
Hili sio dil maana akishuka daraja atapoteza ubora

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi Samatta na Lukaku nani bora..povu ruksa
 
Akipata shavu epl itakuwa hatua kubwa sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…