Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,809
- 15,421
Hebu chukulia kwamba umeoa au kuolewa na umeishi na mkeo au mumeo huyo kwa miaka nane, na mna watoto wawili katika ndoa yenu. Inatokea mnakubaliana mnunue kiwanja kutokana na kuchoshwa na nyumba za kupanga, hivyo mnaweka lengo la pamoja kuwa mtafute fedha kwa ajili ya kutimiza lengo lenu.
Inatokea kazini kwenu inajitokeza Benki moja inaingia makubaliano na kampuni yenu kwa ajili a kutoa mikopo ya muda mrefu yaani mikopo ya miaka mpaka miwili, na unaamua kukopa kiasi cha Milioni tatu baada ya kushauriana na mwenzio.Baada ya kupata fedha hizo mnatafuta Kiwanja na hatimaye mnakipata, na mnakubaliana kukilipia siku inayofuata kwa sababu mlikuwa hamtembei na hizo fedha.
Mnaporudi nyumbani unamkabidhi mwenzio hizo fedha akalipie hicho kiwanja kwa sababu wewe utakuwa bize kazini. Baadaye unakuja kugundua kuwa mwenzio hakulipia kile kiwanja kama mlivyokubaliana na hujui fedha kazipeleka wapi……….unapomdadisi anakujibu kwa kugomba, 'bwanae usinibabaishe na vijihela vyako, nitakutafutia na kukurudishia. Wewe ulinipa nikalipie kiwanja, sasa ni kiherehere gani kilikupeleka huko kwenda kuuliza, ina maana hatuaminiani siku hizi?
Hebu niambie kama ni wewe utafanya nini?
Inatokea kazini kwenu inajitokeza Benki moja inaingia makubaliano na kampuni yenu kwa ajili a kutoa mikopo ya muda mrefu yaani mikopo ya miaka mpaka miwili, na unaamua kukopa kiasi cha Milioni tatu baada ya kushauriana na mwenzio.Baada ya kupata fedha hizo mnatafuta Kiwanja na hatimaye mnakipata, na mnakubaliana kukilipia siku inayofuata kwa sababu mlikuwa hamtembei na hizo fedha.
Mnaporudi nyumbani unamkabidhi mwenzio hizo fedha akalipie hicho kiwanja kwa sababu wewe utakuwa bize kazini. Baadaye unakuja kugundua kuwa mwenzio hakulipia kile kiwanja kama mlivyokubaliana na hujui fedha kazipeleka wapi……….unapomdadisi anakujibu kwa kugomba, 'bwanae usinibabaishe na vijihela vyako, nitakutafutia na kukurudishia. Wewe ulinipa nikalipie kiwanja, sasa ni kiherehere gani kilikupeleka huko kwenda kuuliza, ina maana hatuaminiani siku hizi?
Hebu niambie kama ni wewe utafanya nini?