Fei Toto anahitaji msaada wa maombi

Fei Toto anahitaji msaada wa maombi

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Kijana amevurugwa kichwa, wenye hela wamemvuruga moyo, pepo la fedha nyingi za ghafla likamrukia shingoni.

Hapo alipofikia Sasa hahitaji msaada wa wanasheria bali wanamaombi ili kumtoa pepo la tamaa na choyo lililomfunika. Wanasheria watamharibia zaidi kipaji chache.

Fei Toto anahitaji watu neutral wampatie utulivu wa akili kabla ya kumuelewesha pale alipokosea na afanye nini kuokoa kilichobaki kabla ya Mei 2024.

Familia ya Fei washauriwe watafute njia nyingine za kujikimu ili Fei aende polepole kufika kule waliko akina Chama, Mbwana, Mayele, Saido, Bangala, Inonga, na akina Manula na Diara. Kuna mchakato wa kufikia hatua hizi na sio kwa kufunga magoli 3 tU kwenye mechi ngumu za timu.

Kama TFF wangeamua kwa hovyo kesi hii basi timu ndogo zote zingenyang'anywa wachezaji wao wazuri kwenda timu kubwa kiholela. Kama Yanga imenyang'anywa kwa aina hii itakuwa ruvu shooting na mlandege FC?

Ni bora TFF imeuona upuuzi huu mapema, hongera sana TFF kwa malezi haya. Kinachofuata ni adhabu Kali kwa wote walioko nyuma ya upuuzi huu unaoelekea kwenda kuua kipaji Cha mtoto anaeinukia kisoka. Walidhani wataambiwa walipe faini tu kwa kuvunja mkataba kimakosa ili kuondoka na Fei, lakini hesabu zao zimegonga ukuta. kama ingekuwa rahisi hivyo hata akina mbappe, halaand, messi, Pogba na Ronaldo wangeshasepea kwingine fasta kufuata pesa nyingi kwa matajiri

Tunajua kwamba Yanga Haina shida na kumuachia Fei aondoke zake, lakini kama watafanya hivyo watakuwa wamekosea sana Leo na hata kesho. Watashindwa kufanya vinginevyo kwa case itakayofanana na hii huko mbele.

Kila mtu mwenye ujuzi na karama ya kutuliza pepo mchafu amsaidie kijana wetu.
 
Fei anatakiwa kupewa haki yake, kulazimisha kumlipa mshahara ni kama njia ya kumtongoza, ili kuwafichia aibu utopolo wasiojua kuingia mikataba na wachezaji na wadhamini wao.
 
Mpaka Sasa fei toto hapewi mshahara wowote ...

Asipokuwa makin ataanza kula unga wa sembe maana hata huo ugali na sukari hatavipata ...
 
Fei anatakiwa kupewa haki yake, kulazimisha kumlipa mshahara ni kama njia ya kumtongoza, ili kuwafichia aibu utopolo wasiojua kuingia mikataba na wachezaji na wadhamini wao.
Ushaur Kama huu ndio utampoteza kabisa kijana

Mkataba hauvunjwi Kama kuni mkuu kumbuka mkataba una vigezo na masharti lazima vifuatwe Tena kwa taratibu

Msahurini kijana vizuri

Tatizo siasa za Simba na yanga zimewabrain wash had weled.mmeuweka pembeni

Nadhan Sasa mtaelewa namna ya kuheshimu mikataba

Unadhan wachezaj wote wakifanya Kama fei toto basi vilabu havitabaki na wachezaj

Tff lazma wakomeshe upuuzi huu Kuna watu wapo nyuma ya sakata hili nao lazma wajulikane pia

Wengi wenu mnadhan viongozi wa tff n vilaza wanajua wanachokifanya hata waende fifa.lazma wareview ya tff
 
Fei anatakiwa kupewa haki yake, kulazimisha kumlipa mshahara ni kama njia ya kumtongoza, ili kuwafichia aibu utopolo wasiojua kuingia mikataba na wachezaji na wadhamini wao.
kama hana mkataba na Yanga si aende sasa anakohitajiwa?
 
Mpaka Sasa fei toto hapewi mshahara wowote ...

Asipokuwa makin ataanza kula unga wa sembe maana hata huo ugali na sukari hatavipata ...
Timu iliyomsababishia yote haya haiwezi kumuacha hivihivi, itamtunza bila kucheza. Hesabu zao zimebuma, walidhani watapewa adhabu ya kulipa faini kwa kuvunja mkataba isivyo halali, nyashu hawa.
 
Fei anatakiwa kupewa haki yake, kulazimisha kumlipa mshahara ni kama njia ya kumtongoza, ili kuwafichia aibu utopolo wasiojua kuingia mikataba na wachezaji na wadhamini wao.
Mkuu ruling ya namna hiyo kwenye mchezo wa soka haipo kokote Duniani. Kwa kifupi duniani kote hakuna kipengele kigumu kwenye mikataba ya wachezaji kama kuvunja mikataba. Utapewa option au clause fulani ya kuvunja mkataba, hata hivyo ni muhimu ukosoma vipengele vyote vya mkataba na uvielewe ndio uanze mchakato wa kuvunja mkataba. Kwa kesi ya Faisal ni ngumu kutoka Yanga kama hatarudi Yanga na kuwaomba wakae Mezani ili wamruhusu anunuliwe na timu nyingine. Ungekuwa na nafasi ya kuongea na Wakala wa Bangala na Djuma Shabani Bw. Faustin Mukandila ungeelewa ninachokuambia maana akisema mtu wa hapa Bongo waweza sema ni uongo.
 
Ushaur Kama huu ndio utampoteza kabisa kijana

Mkataba hauvunjwi Kama kuni mkuu kumbuka mkataba una vigezo na masharti lazima vifuatwe Tena kwa taratibu

Msahurini kijana vizuri

Tatizo siasa za Simba na yanga zimewabrain wash had weled.mmeuweka pembeni

Nadhan Sasa mtaelewa namna ya kuheshimu mikataba

Unadhan wachezaj wote wakifanya Kama fei toto basi vilabu havitabaki na wachezaj

Tff lazma wakomeshe upuuzi huu Kuna watu wapo nyuma ya sakata hili nao lazma wajulikane pia

Wengi wenu mnadhan viongozi wa tff n vilaza wanajua wanachokifanya hata waende fifa.lazma wareview ya tff
Hata muda wa kukata rufaa umekwisha (time barred), kijana afanyiwe maombi ya nguvu ili kunusuru kipaji chake. hata kwa shingo upande na huzuni kubwa Fei lazima arudi Yanga kusema "I am Sorry" mbele ya camera ili kujaribu njia nyingine mpya ya kutoka Yanga. Na ile timu inayomtaka Fei ije Yanga na kusema "I am sorry" ili kujaribu njia mpya ya kumpata Fei. Hakuna short cut. Maana kama Fei atafanikiwa kuondoka kipuuzi hivi atakaepitia uchochoro huo kuondoka yanga anaweza kuwa Job, then Msheli, then Kibwana, then Farid, then Mwamnyeto, then Mudathir baada ya kuifunga TP Mazembe. Prof atauziba uchochoro huo kwa kuhakikisha kuwa wazawa hawapewi nafasi kucheza ili kuepuka kufunga magoli na kudai mshahara mkubwa.
 
Hata muda wa kukata rufaa umekwisha (time barred), kijana afanyiwe maombi ya nguvu ili kunusuru kipaji chake. hata kwa shingo upande na huzuni kubwa Fei lazima arudi Yanga kusema "I am Sorry" mbele ya camera ili kujaribu njia nyingine mpya ya kutoka Yanga. Na ile timu inayomtaka Fei ije Yanga na kusema "I am sorry" ili kujaribu njia mpya ya kumpata Fei. Hakuna short cut. Maana kama Fei atafanikiwa kuondoka kipuuzi hivi atakaepitia uchochoro huo kuondoka yanga anaweza kuwa Job, then Msheli, then Kibwana, then Farid, then Mwamnyeto, then Mudathir baada ya kuifunga TP Mazembe. Prof atauziba uchochoro huo kwa kuhakikisha kuwa wazawa hawapewi nafasi kucheza ili kuepuka kufunga magoli na kudai mshahara mkubwa.
Yanga ni timu kubwa sana kuendeshwa kwa hisia kama Fei na mama yake wanavyotaka iwe. Hii ni fursa muhimu kwa wachezaji na timu nyingine kujifunza namna ya kuisoma na kuingia mkikaba. Hii ni fursa nyingine muhimu kwa mpira wetu. hata hawa mawakala wetu wa wachezaji kuna jambo pia wanajifunzi. TFF kwenye hili wameupiga mwingi sana kwa mpira wao. Kilichobakia ni kutoa adhabu kubwa zaidi inayokuwa fundisho kwa watu/timu zinazohitaji saini za wachezaji kwa njia za kipuuzi.
 
Fei anatakiwa kupewa haki yake, kulazimisha kumlipa mshahara ni kama njia ya kumtongoza, ili kuwafichia aibu utopolo wasiojua kuingia mikataba na wachezaji na wadhamini wao.
Haki zake ni zipi hebu zitaje
 
Fei anatakiwa kupewa haki yake, kulazimisha kumlipa mshahara ni kama njia ya kumtongoza, ili kuwafichia aibu utopolo wasiojua kuingia mikataba na wachezaji na wadhamini wao.
HEBU ziorodheshe hizo haki zake anazostahili kupewa. Unajuwa, Yanga sio mali ya Eng. Hersi, ingawa na yeye anaweza kuwa na uchugu kama aliokuwanao mama yake Fei kwa mwanawe lakini kwa mustakabali wa timu ya Yanga na mpira nchini hazwezi kutoa maamuzi kwa kutumia hisia zake binafsi. kama akifanya hivyo hata yeye kesho haifiki akiwa ofisini. The least evil is for faisal to bow down before the yanga management to ask them for forgiveness, nothing more nothing less than that. Hata mama yake Fei angemsaidia mwanawe kwa kumkana mwanawe alichokifanya na kuunga mkono Yanga kwa kitendo kibaya alichofanya mwanawe katikati ya ligi wakati Yanga ikikabiliwa na mechi ngumu ya Azam, ligi, FA na mashindano ya caf. Huu ni usaliti wa hali ya juu kabisa kwa kocha wake Nabi, Yanga, management na wadau wote wa Yanga. Kijana amefanya kosa baya sana la mpira wa miguu alipaswa kukemewa na wadau wote wa mpira badala ya kumtetea.
 
Back
Top Bottom