Felista Njau: Bajeti haijazungumzia Diplomasia ya Uchumi

Felista Njau: Bajeti haijazungumzia Diplomasia ya Uchumi

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
1655510372283.png

Picha> Mbunge Felista Njau akitoa hoja bungeni

Felista Njau, Mbunge wa viti maalum akiwa Bungeni leo ametoa mchango wake kuhusu bajeti huku akisisitiza kuwa bajeti imeacha kipengele muhimu cha Diplomasia ya uchumi katika kufafanua jambo hili alisema:

"Katika bajeti sijaona kipengele muhimu nacho ni diplomasia ya uchumi, Rais Samia Suluhu ameonekana kama mtu wa kutoa pasi za mwisho za kufunga katika eneo la diplomasia, hivyo wanapaswa wapatikane wafungaji. Kila mtu acheze kwenye nafasi yake".

"Wakati tukiimba Royal Tour inaleta matokeo, ni lazima twende kwenye diplomasia ya uchumi kujiuliza namna gani tutapata watalii zaidi, wawekezaji na kufungua fursa mbalimbali kwa Taifa letu, katika hilo Rais Samia

amecheza nafasi yake nasi tucheze nafasi zetu".

"Katika balozi zetu hakuna kitengo cha habari, ukiangalia blogs mbalimbali za Wizara na mitandao ya kijamii ya balozi huoni wakitangaza bidhaa zetu. Tunahitajika kujipambanua kama Watanzania, na sio kusubiri mtu mmoja atangulie mbele na kisha sisi turudi nyuma".

Nini mtazamo wako kuhusu hoja zilizotolewa na Bi. Felista Njau
 
Sasa huyu mbunge yuko bungeni kufanya nini? Alitaka waziri amalize kila kitu yeye akosoe/apongeze tu?

Baada ya kuona mapungufu hayo alipaswa kutoa mchango wake wa mawazo ili kuborsha.

Yaani analalamikia mapishi wakati yupo jikoni? Shubamiti!
 
Huyu amechangia ili mradi na yeye aonekane amechangia tu. Hiyo diplomasi ya uchumi ni maneno ya mbwembwe na kufurahisa tu.
 
Back
Top Bottom