Fid Q chukua tahadhari, umeshuka sana kimuziki

Old Member (Retired)

JF-Expert Member
Joined
Sep 29, 2012
Posts
3,401
Reaction score
1,610
Fid Q uwezo wako unashuka sana, Fid Q wasasa si Fid Q wa miaka michache iliyopita
Fid Q naheshimu sana uwezo wako wa kuandika japo flow yako si nzuri sana.

Kuhusu kuandika Joh Makini hakwambii kitu lakini flow yako si mbaya sana.

Rudi nyuma angalia ni wapi umekwamba Fid Q, mpaka leo hii umepiga show za fiesta
zisizozidi hata tatu, show kubwa ya Dar hujatia mguu kabisa.

Kidogo watu tumeanza kukusahau, unahitaji kufanya kazi ya ziada ili urudi pale ulipokuwa.

Fid Q rudi zako, enzi zile unaandika mwanza mwanza. Kinyume na hapo tuzo za Kili za 2015 utazisikia bombani.

MCHUNGUZI HURU (Associate Professor)
 
Last edited by a moderator:
Hahahah nadhani humjui fid vizuri.. Bongo hiphop bado ni wimbo wa taifa kwa sasa
 
Kiukweli mziki anaofanya Fid Q ni wa aina yake lakini jamaa bado hajajua namna ya kucheza na soko la sasa sawa ametoa Bongo Hip Hop lakini hauja kick kama ulivyotakiwa kiasi kwamba haujafikia level za Ielewe Mitaa, lakini hata US wasanii wanaofanya Hardcore nao wanahali mbaya mtu kama Mos Def anakaza sana lakini wapi promo zinaishia kwa kina T.I ambao basically wanafanya Trap/Crank. Lakini mwisho wa siku Fid Q ni mahiri katika uandishi lakini Msanii kama Joh Makini yeye anajua soko linaenda wapi na linataka nini.
 
kama ni soko la kuuza muziki, Bongo hakuna hilo soko kwa sasa. hakuna msanii anayeuza single wala album yaani kimsingi soko limeparaganyika.

Labda ni aina ya muziki wanaoutaka Wabongo kuusikia kwa redio ndio shida ya Fid Q. Angepunguza kukaza na afanye ngoma kama "usinikubali haraka" au "ngosha the swaga don" nadhani zile ndio ziko laini fulani hivi lakini bado zilikuwa fresh.
 
Bongo Hiphop mi naukubali kuliko nyimbo zake zote alizotoa miaka mitatu iliyopita
 
Ndo madhara ya kuimba kwa kuiga wanamuziki wa "Unyamwezini".

Ni lazima utakwama tu! Fid Q amekwama.
 
Fid Q mziki wake ni BIG G.

mimi nina album zake mbili "Vina Kati Mwanzo na Mwisho" na "Propaganda". Pia nina album ya Ngwear na mpaka leo nazisikiliza napopata nafasi.

Naomba unitajie nani mziki wake sio big g kati ya wasanii wa bongo fleva.
 
mimi nina album zake mbili "Vina Kati Mwanzo na Mwisho" na "Propaganda". Pia nina album ya Ngwear na mpaka leo nazisikiliza napopata nafasi.

Naomba unitajie nani mziki wake sio big g kati ya wasanii wa bongo fleva.

Same to me bra ..!
Propaganda, vina mwanzo kati na mwisho NA aka mimi hakuna ngoma ambayo naweza kusema eti "nifoward "....noma sana!!
 
Huyo ngosha apunguze mapozi sawa anaandika mistari mikali ila ananata sana kiuhalisia.

Ana mwonekano wa hiphop ila moyoni u jux umemtawala. Vinginevyo Weuuuuusiiiiiiii tutazizoa sana hizo tunzo kudadeki
 
Bongo Hiphop ni moja ya ngoma kali tatizo la fid hafanyi vi2 kibiashara, hafanyii ngoma zake promo ya kutosha, hajiwek karibu na mashabiki kuona wanachopenda kwa wakati husika! Kifupi anafanya kile kilichowafanya wasanii wengi wa ARUSHA wafe njaa huku wakisifiwa hiphop city!
 
Huyo ngosha apunguze mapozi sawa anaandika mistari mikali ila ananata sana kiuhalisia.

Ana mwonekano wa hiphop ila moyoni u jux umemtawala. Vinginevyo Weuuuuusiiiiiiii tutazizoa sana hizo tunzo kudadeki

Acha Roho ya kwanini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…