Fid Q, Nilistahili Kushinda Tuzo ya Kill

wamefanya kumpa tu kutoa lawama,maana umri wake unaenda alistahili hii tuzo kitambo si sasa

tuzo hii sio ya kwanza kwa fid...na fid ata leo bado anakalisha watoto wote kwenye hiphop..
 
Nyimbo za Fareed zinatungwa kwa ajili ya wale wanaotumia vichwa vyao Kufikiri,Wanaotumia kufugia nywele huwa hawamuelewi.

Sio lazima unachokiamini wewe na mimi niamini ,Amini kuna vitu vinavyonivutia mimi lakini wewe havikuvutii.!!
 

Yaah hata Ally choki nae pia ana rap hii unaizungumziaje mkuu?
 
Hujui kitu mkuu, hujui hip hop. U much know ndiyo umekukaa kwenye akili yako. Fid q kapewa tu kwa sababu walimbania miaka ya nyuma. Lakini uhalisia fid q hakustahili hata category.

We ndio hujui kitu John makin ana rapa kama akina Ally choki au marapa wengine wa kwenye sebene,kama hujui kitu omba watalaam wakujuze.
 
Napenda sana hip hop, ila nyimbo za FidQ mara nyingi sizielawagi.

Hip hop sio kama taarab,Hip Hop neno moja linabeba wimbo mzima wa taarabu,we endelea kusikiliza taarabu tu Hip Hop tuachie wenye kufikilisha vichwa.
 
Naomba unipe somo kidogo. FidQ kawa msanii bora hiphop wa mwaka 2013/2014 kwa wimbo wake wa "i am a professional", au sio.. Lakini huu wimbo mbona sio wa huu mwaka, infact niwa kitambo kidogo?
Au mimi ndo sielewi mambo haya? Cc Money Stunna


Wimbo uliomfanya Fid Q aingie kwenye tuzo ni Siri ya Mchezo feat Juma Nature.. Ile I'm Professional ilikuwa ni kionjo tu kilichowekwa wakati anatajwa mshindi wa Msanii Bora wa Hip Hop na Mtunzi Bora. Angeshinda wimbo bora wa Hip Hop wangeweka ule uliomfanya akaingia kwenye category.
 
Ukweli lazima usemwe amezidi deko.

Mkuu Jide kwa sasa naanza kumfananisha na Chama flani cha siasa hapa nchini ambacho kila siku kinahisi kinahujumiwa tuu na hata kinapotenda makosa ya wazi kabisa huwa kinakimbilia kusema kinahujumiwa na wafuasi wake wengi wamerithi hiyo tabia Mda wote wanajiona wako sawa na wote walio na mawazo tofauti na wao wanaonekana si lolote
BACK TO THE TOPIC
Jide naye amelewa na Sapoti anayopewa na mashabiki anajiona sasa anaweza akafanya lolote na akaendelea kupata Sapoti kama awali Mimi Nakumbuka mwaka jana Jide hakuhudhuria kwenye sherehe za utoaji wa tuzo Lakini kwenye matamasha yaliyooandaliwa kwa ajili ya washindi wa KTMA hakukosa show hata moja hapa kuna nini¿¿¿
 

Mkuu umetisha Sana nimekuelewa vya Kutosha
 

Asante kwa kunifungua macho mkuu mi nilikuwa sielewi maana ile nyimbo ni ya long kumbe anayo nyingine mpya
 
Ushindi wa Tunzo ya msanii bora wa Hip Hop wa Fid Q kiuhalisia umetokana na yeye kufanyiwa campaign kubwa na marafiki wasanii, watu wa media na mashabiki walioona Fid Q hakushinda Tunzo miaka ya nyuma lakini si kwamba yeye ndio mwanaHip Hop bora wa mwaka 2013 may be ya mtunzi bora. Ngoja nikupe sababu kwa mtizamo wangu lakini. Ili ushinde Tuzo hiyo inabidi uwe umefanya ngoma ambazo ni heats zaidi ya wenzako. Kushirikishwa katika ngoma mbali mbali ambazo ni heats, kufanya shows nyingi zaidi ya wenzako n.k hayo yote kwa ujumla ndo kigezo kikubwa cha mtu kuweza kushinda. Kwa mwaka 2013 Fid Q ametoa ngoma moja tu ya siri ya mtungi ft Juma Nature, ambayo pia ilikua katika category ya nyimbo bora ya Hip na haikushinda. Kwa wafuatiliaji wa Hip Hop hamtabisha kua ngoma hiyo haikupata airtime ya kutosha. Kosa ambalo KTMA walifanya sijui kwa nini ni kutomuweka Joh Makini in nomination ya msanii bora wa Hip Hop. Haijalishi wanaosema Joh hafanyi Hip Hop lakini mziki anaofanya according to KTMA ni Hip Hop(not according to Hardcore Hip Hop lovers). Kwangu Joh Makini ndo msanii bora wa Hip Hop 2013 kwa nini? According to Dj Choka ni kua Joh Makini ni msanii wa Hip Hop aliefanya show nyingi zaidi kwa mwaka 2013 kuliko mwanaHipHop yoyote. Joh Makini kwa mwaka 2013 amefanya ngoma kali kama Sijutii na Nikumbatie pia amefanya ngoma ambazo zimeingia kwenye nominations KTMA ambazo ni Bei ya mkaa na Nje ya Box(imeshinda nyimbo bora ya Hip Hop), pia kundi lake la WEUSI lilikua kwenye nomination za kundi bora la mwaka-kizazi kipya (likashinda). Kwa sababu za Hapo juu Joh Makini ndo alistahili kuwa msanii bora wa Hip Hop 2013. Fid Q alishinda kwa huruma tu za mashabiki tu
 
Hujui kitu mkuu, hujui hip hop. U much know ndiyo umekukaa kwenye akili yako. Fid q kapewa tu kwa sababu walimbania miaka ya nyuma. Lakini uhalisia fid q hakustahili hata category.

Wewe umeongea point, wengi humu wanaleta mapenzi tu na sio kwa kuangalia Fid Q kafanya nini 2013. Sio kwamba simkubali Fid Q namkubali sana. Inaezekana nikawa namsikiliza na kumuelewa sana kuliko hata nyie mnaokataa ukweli kisa mnamkubali Fid laki ukweli lazima usemwa. Fid Q ni msanii bora wa Hip Hop tanzania kwa miaka 5 ya nyuma kwa ujumla, lakini kwa mwaka 2013 hakufanya kitu bora ambacho kinamfanya awe msanii bora kwa mwaka huo. Wengi wamempigia kura Fid Q kama msanii bora wa Hip Hop bila kuangalia mwaka.
 
We ndio hujui kitu John makin ana rapa kama akina Ally choki au marapa wengine wa kwenye sebene,kama hujui kitu omba watalaam wakujuze.

Wataalam nani? Mtaalam unajiita, sema unachokijua tusikie, huna tofauti na muhongo, mtaalam mtaalam.
 

Mkuu upo sahihi, upo sahihi. Naona wengine wanaleta ujuaji kwenye jumba lisilo hitaji ujuaji zaidi ya facts.
 

Anayesimamia shughuli na event ya utoaji tuzo ni demu wa Ruge ...aliyesimamia matamasha ya kili baada ya tuzo ni east Africa...nafikiri ukitumia akili unaweza kuelewa kinachoendelea.
 
anayesimamia shughuli na event ya utoaji tuzo ni demu wa ruge ...aliyesimamia matamasha ya kili baada ya tuzo ni east africa...nafikiri ukitumia akili unaweza kuelewa.
huyo demu wa ruge ndo aliyempa hizo tuzo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…