Fiesta 2016, Clouds media inaweza ina nini. Serikali haiwezi ina nini?

Jacobus

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2011
Posts
4,703
Reaction score
1,724
Wakuu, hivi sasa Clouds media ina utaratibu wa Fiesta takriban nchi nzima, kilichonifurahisha ni kuweza kupata vikundi vya ngoma za asili kila wapitapo.
Najiuliza hawa Clouds wamewezaje kuandaa mpaka vikundi mikoani ilhali wizara ya utamaduni wanamaofisa mikoani lakini hatusikii mpango wowote wa kuendeleza ngoma zetu za asili japo kwa kuandaa tu kama hawa Clouds.
Tatizo ni nini?
 
Aulizwe Nape Nnauye , anapokuwa katibu mwenezi wa ccm anakusanya kila ngoma kwenye kampeni , lakini akiwa waziri hawezi !
 
Aulizwe Nape Nnauye , anapokuwa katibu mwenezi wa ccm anakusanya kila ngoma kwenye kampeni , lakini akiwa waziri hawezi !
Kweli mkuu, inavoonekana utamaduni wetu nao umegeuzwa siasa hasa wakati wa kampeni na upokeaji wageni (Marais) toka nje ya nchi.
 
Clouds wanatengeneza pesa hapo...lakini kumbuka serikali haiwezi kufanya yote taasisi binafsi kama clouds pia ni wadau wa maendeleo ya nyanja tofauti tofauti kama utamaduni..
 
Clouds wanatengeneza pesa hapo...lakini kumbuka serikali haiwezi kufanya yote taasisi binafsi kama clouds pia ni wadau wa maendeleo ya nyanja tofauti tofauti kama utamaduni..
Sawa mkuu lakini mantiki ya uundwaji wa wizara hiyo ilikuwa nini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…